Kihongosi: CHADEMA inakufa, Mbowe katoka wanagombana Mahakamani

Kihongosi: CHADEMA inakufa, Mbowe katoka wanagombana Mahakamani

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,498
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema ushindi wa chama hicho katika chaguzi unatokana na kuwa na mfumo imara na mtandao mpana wa wanachama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Maswa mkoani Simiyu Machi 7, 2026, Kihongosi amesema Katiba ya CCM inaitaka chama hicho kushinda chaguzi zote, huku akieleza kuwa uimara wa muundo wake ndio msingi wa mafanikio hayo.

Amesema katika ziara yake ametembelea shina lenye wanachama zaidi ya 150 na kubainisha kuwa mkoa wa Simiyu una mashina zaidi ya elfu mbili hadi tatu, hali inayodhihirisha idadi kubwa ya wanachama waliopo ngazi ya chini.

“Mikoani tuna watu, wilaya tuna watu, kwenye kata tuna watu, kwenye matawi tuna watu, kwenye mashina tuna watu na mabalozi tunao. Huwezi kutufananisha na wengine,” amesema.

Kihongosi amedai kuwa vyama vingine vya upinzani havina mfumo mpana wala uongozi thabiti kama CCM, akitaja baadhi ya vyama kuwa vinaendeshwa zaidi kwa ushawishi wa mtu mmoja mmoja badala ya taasisi imara.

Amesisitiza kuwa tofauti na vyama hivyo, CCM inaendeshwa kama taasisi yenye mizizi imara inayotegemea wanachama wake kuanzia ngazi ya chini kabisa.

 
Si tulikubaliana pale chamwino kuwa CHADEMA IMEKUFA sasa mbona tunaiongelea kila wakati?

Chadema iko mioyon mwa watu na hicho ndicho kinachowashangaza CCM chama mmekifanyia kila hila lakn kipo hakifi

Leo.mwanangu wa 7yrs kasema anataka kuwa kiongoz mkubwa wa chadema imagine
 
Huko ni kujitekenya na kucheka mwenyewe. Walishazoea vyama pandikizi sasa wamekutana na chama cha wananchi. CDM ni zaidi ya chama cha siasa, ni platform ya Watanzania wasiokubaliana na CCM, haiwezi kufa.

Anayewadanganya kuwa mumpe fedha ili awasaidie kuua CDM anawapiga kwa ujinga wenu. Mawazo mbadala hayawezi kufa kamwe.
 
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema ushindi wa chama hicho katika chaguzi unatokana na kuwa na mfumo imara na mtandao mpana wa wanachama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Maswa mkoani Simiyu Machi 7, 2026, Kihongosi amesema Katiba ya CCM inaitaka chama hicho kushinda chaguzi zote, huku akieleza kuwa uimara wa muundo wake ndio msingi wa mafanikio hayo.

Amesema katika ziara yake ametembelea shina lenye wanachama zaidi ya 150 na kubainisha kuwa mkoa wa Simiyu una mashina zaidi ya elfu mbili hadi tatu, hali inayodhihirisha idadi kubwa ya wanachama waliopo ngazi ya chini.

“Mikoani tuna watu, wilaya tuna watu, kwenye kata tuna watu, kwenye matawi tuna watu, kwenye mashina tuna watu na mabalozi tunao. Huwezi kutufananisha na wengine,” amesema.

Kihongosi amedai kuwa vyama vingine vya upinzani havina mfumo mpana wala uongozi thabiti kama CCM, akitaja baadhi ya vyama kuwa vinaendeshwa zaidi kwa ushawishi wa mtu mmoja mmoja badala ya taasisi imara.

Amesisitiza kuwa tofauti na vyama hivyo, CCM inaendeshwa kama taasisi yenye mizizi imara inayotegemea wanachama wake kuanzia ngazi ya chini kabisa.

na mmeshinda uRAISI kwa 98% lakini mnawaogopa BAWACHA wakisherehekea siku yao Duniani!
 
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema ushindi wa chama hicho katika chaguzi unatokana na kuwa na mfumo imara na mtandao mpana wa wanachama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Maswa mkoani Simiyu Machi 7, 2026, Kihongosi amesema Katiba ya CCM inaitaka chama hicho kushinda chaguzi zote, huku akieleza kuwa uimara wa muundo wake ndio msingi wa mafanikio hayo.

Amesema katika ziara yake ametembelea shina lenye wanachama zaidi ya 150 na kubainisha kuwa mkoa wa Simiyu una mashina zaidi ya elfu mbili hadi tatu, hali inayodhihirisha idadi kubwa ya wanachama waliopo ngazi ya chini.

“Mikoani tuna watu, wilaya tuna watu, kwenye kata tuna watu, kwenye matawi tuna watu, kwenye mashina tuna watu na mabalozi tunao. Huwezi kutufananisha na wengine,” amesema.

Kihongosi amedai kuwa vyama vingine vya upinzani havina mfumo mpana wala uongozi thabiti kama CCM, akitaja baadhi ya vyama kuwa vinaendeshwa zaidi kwa ushawishi wa mtu mmoja mmoja badala ya taasisi imara.

Amesisitiza kuwa tofauti na vyama hivyo, CCM inaendeshwa kama taasisi yenye mizizi imara inayotegemea wanachama wake kuanzia ngazi ya chini kabisa.

Hao polisi wanaowapiga mabomu wanawake kwenye sherehe ya wanawake ni vichaa.
 
Kwamba ,kuwaagiza wasimamizi uchaguzi vituoni watiki ndo uimara huo
 
Back
Top Bottom