Leonileo8809
Member
- Dec 23, 2012
- 18
- 2
Chadema bwana.fukuza fukuza haikuzi.inadhoofisha.kinachoshangaza hawaoni km mwisho wao umefika wajipange.
unakuta jamaa alipokea zile laki mbili za zitto kwa propaganda kama hizi wakati zitto alipokea bilioni mbili kutoka ccm.
Kutokana na habari hii,nimejiridhisha kwamba huyu jamaa alijiteka mwenyewe na kujiburuza,ili asingizie wenzake aliokuwa na ugomvi naoJUMAMOSI, JANUARI 11, 2014 10:16 NA PATRICIA KIMELEMETA
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Temeke, Joseph Yona ameondolewa hospitali alikokuwa akipatiwa matibabu na kufichwa kusikojulikana. Chanzo cha habari kimelieleza MTANZANIA Jumamosi kwamba, Yona ambaye alikuwa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI), amehamishwa na familia yake kutokana na sababu za kiusalama.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, familia imefikia uamuzi wa kumhamisha baada ya kuona watesi wake (wabaya) wanamfuata Yona hospitalini hapo.
Kutokana na mazingira hayo, familia hiyo ililazimika kumuomba daktari aliyekuwa akimhudumia mgonjwa huyo kumruhusu ili waweze kumtibu nyumbani kwao.
Kutokana na hali hiyo, daktari alimruhusu baada ya kuona hali yake inaendelea kuimarika, licha ya kuwepo kwa majeraha ambayo yasingeweza kumletea matatizo makubwa.
Familia ya Yona ilimuomba daktari aliyekuwa akimtibia kumruhusu kuondoka, ili aweze kutibiwa na daktari binafsi chini ya uangalizi maalumu wa familia, kwa sababu watesi wake walikuwa wakimfuata hospitalini hapo.
Chanzo hicho kilichopo karibu na familia hiyo, kilieleza kuwa Yona alitolewa siku ile ile aliyofikishwa hospitali na kufichwa kusikojulikana kwa sababu za kiusalama, baada ya kuwataja watesi wake hadharani.
Hata hivyo, Ofisa Habari wa MOI, Patrick Mvungi alithibitisha kutolewa kwa mgonjwa huyo siku hiyo alipolazwa na kudai kuwa mgonjwa huyo alikuwa akiendelea vizuri.
Baada ya daktari kumpima na kumuona anaendelea vizuri, wameamua kumruhusu kurudi nyumbani na kwamba mpaka sasa hajarudi tena katika taasisi hiyo, alisema Mvungi.
Yona alitekwa, kupigwa, kuteswa na watu aliodai ni baadhi ya wanachama wenzake wa chama hicho, kwa madai kuwa amekuwa akishirikiana na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Zitto Kabwe.
Baada ya kupigwa, Yona alipelekwa katika eneo la Ununio, Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kuokotwa na wasamaria wema wanaoishi karibu na maeneo hayo.
Kutokana na hali hiyo, mgonjwa huyo alipelekwa MOI kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambapo alipimwa kwa kipimo cha CT-Scan pamoja na kufanyiwa vipimo vingine vya kitabibu.
Awali akielezea mkasa huo, Yona alisema aliingia katika mgogoro huo baada ya kuitisha kikao cha waandishi wa habari na kuiomba Kamati Kuu ya Chadema kuitisha mkutano wa kujadili suala la Zitto na wenzake.
Mbali ya Zitto, watuhumiwa wengine walikuwa ni aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Samson Mwigamba.
Alisema kutokana na hali hiyo, viongozi wakuu wa chama hicho, akiwemo Mwenyekiti, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa walimuita na kumwambia ajitoe ndani ya chama hicho kabla ya kumfukuza, jambo ambalo alilipinga.
Hata hivyo, Dk. Slaa amekanusha madai hayo na kueleza kuwa hajawahi kuwasiliana na Yona kwa lengo la kumshinikiza ajiuzulu wadhifa wake huo.
c.c kibogo
Kinachoshangaza ni kwamba Yona alishatoka hospitali (MoI) na alilipiwa matibabu na mratibu wa kanda ya pwani Bw Tugara kiasi cha shilingi elfu 50,000/ na akakodiwa na kulipiwa Tax mpaka nyumbani kwake, Lakini baadae akarudishwa tena na waliokuwa wanapanga njama za ugaidi.
Tanzania haiishi vituko! yaani ugaidi unalazimishwa kwa kupangwa kama mafungu ya nyanya!
Kinachoshangaza ni kwamba Yona alishatoka hospitali (MoI) na alilipiwa matibabu na mratibu wa kanda ya pwani Bw Tugara kiasi cha shilingi elfu 50,000/ na akakodiwa na kulipiwa Tax mpaka nyumbani kwake, Lakini baadae akarudishwa tena na waliokuwa wanapanga njama za ugaidi.
Tanzania haiishi vituko! yaani ugaidi unalazimishwa kwa kupangwa kama mafungu ya nyanya!
Kutokana na habari hii,nimejiridhisha kwamba huyu jamaa alijiteka mwenyewe na kujiburuza,ili asingizie wenzake aliokuwa na ugomvi nao
nasema hivyo kwasababu: wenzake waliotekwa kiukweli Dr,Ulimboka na Kibanda waliumizwa vibaya kiasi cha kupelekwa nje ya nchi,iweje huyu aliruhusiwa siku hiyo hiyo aliyofikishwa hospitali na Daktari anakiri kuwa alikuwa anaendelea vizuri.Naamini watu wote wanaoruhusiwa kurudi nyumbani kitaaluma ya udaktari huwa wanaendelea vizuri au matibabu yameshindikana,sasa huyu tunaambiwa anaendelea vizuri,pili Huyu jamaa tofauti na wenzake kwa maelezo ya kova alisema aliwatambua waliomtesa na kuwaambia palepale kwamba amewafahamu jambo ambalo lingemsababishia kuuawa au kuumizwa vibaya sana,cha kushangaza ndo akaumizwa kidogo akatupwa nje ya mji,akaokotwa na wasamalia na kupelekwa hospitali kisha akaruhusiwa siku hiyo hiyo?
Hadithi nyingine za kupika zinakuwa hazijaiva sawasawa.
JUMAMOSI, JANUARI 11, 2014 10:16 NA PATRICIA KIMELEMETA
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Temeke, Joseph Yona ameondolewa hospitali alikokuwa akipatiwa matibabu na kufichwa kusikojulikana. Chanzo cha habari kimelieleza MTANZANIA Jumamosi kwamba, Yona ambaye alikuwa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI), amehamishwa na familia yake kutokana na sababu za kiusalama.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, familia imefikia uamuzi wa kumhamisha baada ya kuona watesi wake (wabaya) wanamfuata Yona hospitalini hapo.
Kutokana na mazingira hayo, familia hiyo ililazimika kumuomba daktari aliyekuwa akimhudumia mgonjwa huyo kumruhusu ili waweze kumtibu nyumbani kwao.
Kutokana na hali hiyo, daktari alimruhusu baada ya kuona hali yake inaendelea kuimarika, licha ya kuwepo kwa majeraha ambayo yasingeweza kumletea matatizo makubwa.
Familia ya Yona ilimuomba daktari aliyekuwa akimtibia kumruhusu kuondoka, ili aweze kutibiwa na daktari binafsi chini ya uangalizi maalumu wa familia, kwa sababu watesi wake walikuwa wakimfuata hospitalini hapo.
Chanzo hicho kilichopo karibu na familia hiyo, kilieleza kuwa Yona alitolewa siku ile ile aliyofikishwa hospitali na kufichwa kusikojulikana kwa sababu za kiusalama, baada ya kuwataja watesi wake hadharani.
Hata hivyo, Ofisa Habari wa MOI, Patrick Mvungi alithibitisha kutolewa kwa mgonjwa huyo siku hiyo alipolazwa na kudai kuwa mgonjwa huyo alikuwa akiendelea vizuri.
Baada ya daktari kumpima na kumuona anaendelea vizuri, wameamua kumruhusu kurudi nyumbani na kwamba mpaka sasa hajarudi tena katika taasisi hiyo, alisema Mvungi.
Yona alitekwa, kupigwa, kuteswa na watu aliodai ni baadhi ya wanachama wenzake wa chama hicho, kwa madai kuwa amekuwa akishirikiana na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Zitto Kabwe.
Baada ya kupigwa, Yona alipelekwa katika eneo la Ununio, Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kuokotwa na wasamaria wema wanaoishi karibu na maeneo hayo.
Kutokana na hali hiyo, mgonjwa huyo alipelekwa MOI kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambapo alipimwa kwa kipimo cha CT-Scan pamoja na kufanyiwa vipimo vingine vya kitabibu.
Awali akielezea mkasa huo, Yona alisema aliingia katika mgogoro huo baada ya kuitisha kikao cha waandishi wa habari na kuiomba Kamati Kuu ya Chadema kuitisha mkutano wa kujadili suala la Zitto na wenzake.
Mbali ya Zitto, watuhumiwa wengine walikuwa ni aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Samson Mwigamba.
Alisema kutokana na hali hiyo, viongozi wakuu wa chama hicho, akiwemo Mwenyekiti, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa walimuita na kumwambia ajitoe ndani ya chama hicho kabla ya kumfukuza, jambo ambalo alilipinga.
Hata hivyo, Dk. Slaa amekanusha madai hayo na kueleza kuwa hajawahi kuwasiliana na Yona kwa lengo la kumshinikiza ajiuzulu wadhifa wake huo.
c.c kibogo
JUMAMOSI, JANUARI 11, 2014 10:16 NA PATRICIA KIMELEMETA
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Temeke, Joseph Yona ameondolewa hospitali alikokuwa akipatiwa matibabu na kufichwa kusikojulikana. Chanzo cha habari kimelieleza MTANZANIA Jumamosi kwamba, Yona ambaye alikuwa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI), amehamishwa na familia yake kutokana na sababu za kiusalama.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, familia imefikia uamuzi wa kumhamisha baada ya kuona watesi wake (wabaya) wanamfuata Yona hospitalini hapo.
Kutokana na mazingira hayo, familia hiyo ililazimika kumuomba daktari aliyekuwa akimhudumia mgonjwa huyo kumruhusu ili waweze kumtibu nyumbani kwao.
Kutokana na hali hiyo, daktari alimruhusu baada ya kuona hali yake inaendelea kuimarika, licha ya kuwepo kwa majeraha ambayo yasingeweza kumletea matatizo makubwa.
Familia ya Yona ilimuomba daktari aliyekuwa akimtibia kumruhusu kuondoka, ili aweze kutibiwa na daktari binafsi chini ya uangalizi maalumu wa familia, kwa sababu watesi wake walikuwa wakimfuata hospitalini hapo.
Chanzo hicho kilichopo karibu na familia hiyo, kilieleza kuwa Yona alitolewa siku ile ile aliyofikishwa hospitali na kufichwa kusikojulikana kwa sababu za kiusalama, baada ya kuwataja watesi wake hadharani.
Hata hivyo, Ofisa Habari wa MOI, Patrick Mvungi alithibitisha kutolewa kwa mgonjwa huyo siku hiyo alipolazwa na kudai kuwa mgonjwa huyo alikuwa akiendelea vizuri.
Baada ya daktari kumpima na kumuona anaendelea vizuri, wameamua kumruhusu kurudi nyumbani na kwamba mpaka sasa hajarudi tena katika taasisi hiyo, alisema Mvungi.
Yona alitekwa, kupigwa, kuteswa na watu aliodai ni baadhi ya wanachama wenzake wa chama hicho, kwa madai kuwa amekuwa akishirikiana na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Zitto Kabwe.
Baada ya kupigwa, Yona alipelekwa katika eneo la Ununio, Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kuokotwa na wasamaria wema wanaoishi karibu na maeneo hayo.
Kutokana na hali hiyo, mgonjwa huyo alipelekwa MOI kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambapo alipimwa kwa kipimo cha CT-Scan pamoja na kufanyiwa vipimo vingine vya kitabibu.
Awali akielezea mkasa huo, Yona alisema aliingia katika mgogoro huo baada ya kuitisha kikao cha waandishi wa habari na kuiomba Kamati Kuu ya Chadema kuitisha mkutano wa kujadili suala la Zitto na wenzake.
Mbali ya Zitto, watuhumiwa wengine walikuwa ni aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Samson Mwigamba.
Alisema kutokana na hali hiyo, viongozi wakuu wa chama hicho, akiwemo Mwenyekiti, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa walimuita na kumwambia ajitoe ndani ya chama hicho kabla ya kumfukuza, jambo ambalo alilipinga.
Hata hivyo, Dk. Slaa amekanusha madai hayo na kueleza kuwa hajawahi kuwasiliana na Yona kwa lengo la kumshinikiza ajiuzulu wadhifa wake huo.
c.c kibogo