Kigogo aliyefukuzwa ATCL ajibu mapigo

Kigogo aliyefukuzwa ATCL ajibu mapigo

DonJuan

New Member
Joined
Mar 4, 2015
Posts
1
Reaction score
0
KIGOGO mmoja aliyekuwa na dhamana kubwa katika Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), jina tunalo, ameweka mambo hadharani kwa kusema kuwa ametolewa kafara kwa kufukuzwa na kutuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za shirika hilo zinazokadiriwa kufikia Dola za Kimarekani 55,000.

Kigogo huyo alikiambia chanzo chetu jana jijini Dar es Salaam kuwa katika ubadhirifu huo hakuwa peke yake bali alishirikiana na vigogo wenzake wawili ambao mwisho wa siku wamemgeuzia kibao yeye.

Akizungumza kuhusiana na sakata hilo, kigogo huyo alibainisha kuwa alishirikiana na kigogo wa Uhandisi, na wa Rasilimali Watu.

"Mara ya kwanza Novemba 19, yule wa uhandisi alichukua dola 12,100 za mgawo kisha Januari 19 mwaka huu, akachukua tena 2,700 ambazo alisema ni za matibabu ya mwanae aliyepo Urusi baada ya kupata ajali mbaya nchini Ukraine na yule wa rasilimali watu Desemba 22 mwaka jana, alichukua dola 9650, kwajili ya mambo ya kifamilia na ujenzi wa dharura"

"Tulikubaliana kuwa tutaificha menejiment kuhusu uchotaji huo wa fedha na kisha wao wawashe moto kwa kuishtaki kampuni hiyo ya Kenya kwa kukiuka mkataba na kuidhalilisha kampuni yetu, pia hatukukubaliana kuwafukuza wafanyakazi wa chini lakini wamekiuka kwa kumfukuza cashia pasipo hatia" alisema kigogo huyo.

Aidha kigogo huyo alieleza kuwa washirika wake hao kwa pamoja walimgeuka na kumfanya yeye mbuzi wa kafara ilhali wanaufahamu ukweli wa mambo kuwa wote walihusika na walijua kinachotokea wakati wakiidhinisha wa fedha taslim.

"Wamenigeuka. Naomba na wao wachukuliwe hatua stahiki kama ile iliyochukuliwa dhidi yangu bila kupepesa macho. Wao ndiyo walioidhinisha ulipwaji wa pesa hizo ila leo wamenigeuka,"

"Kila kitu wanakifahamu na wao ndiyo waliahidi kuwa watashughulika na kuishawishi menejiment kufungua kesi za madai na fidia. Pia kama haitoshi wakaenda kuiambia bodi kuwa mimi ndiye niliewarubuni. Mungu atawalipa sawa na waliyonitenda mimi " alibainisha kigogo huyo.

Alisema kuwa fedha hizo ni sehemu ya malipo ya ndege waliyoikodisha toka Kenya, ambayo kila mmoja wao alikuwa akitambua kuwa malipo yote hufanyika kwa njia ya hundi na sio kwa fedha taslim.

Pia kigogo huyo alidai kuwa lengo lao lilikuwa kutaka kuishtaki kampuni hiyo, ambayo kesi hiyo ingechukua muda mrefu na hata uchotwaji wa fedha hizo usingejulikana.

"Kulikuwa na mkakati wa kuwasha moto mkubwa kwa kuishtaki kampuni hiyo ya Kenya na kuendesha kesi ambayo ingechukua muda mrefu kujua kama kulikuwa na uchotaji wa fedha hizo, maana katika mzozo huo ambao tungeanzisha kila mmoja wetu angetoa madai yake, hivyo isingekuwa rahisis kujua ni nani anambambikizia mwenzake lakini baada ya kubainika wenzangu wameruka kwenye kikao cha Bodi, hivyo nina amini mungu atanilipia tu" alidai kigogo huyo.

Alisema anashangaa kuona watu wamemgeuzia kibao na kuamua kutoa kwenye vyombo vya habari huku wakijua ukweli wa jambo hilo.
 
Vibaka wametuibia, sasa mhanga anatuambia. Je tufanyeje???
 
Hana lolote mwizi mkubwa huyo siku zote anayeshikwa na ngozi ndie aliyekula nyama
 
kwa hiyo siye tufanye nn? na wewe ulitumia dola hizo kufanya nn? wenzio wamejenga na wewe?
 
kwa hiyo siye tufanye nn? na wewe ulitumia dola hizo kufanya nn? wenzio wamejenga na wewe?

Yeye alichukua mwanamke mpya wa kiarabu:baby: yaani anakubali kosa mwenyewe ngoja mvua imnyeeshee ndio atajua
 
inakera sana hii ya JINA TUNALO

tuwe wawazi tu
 
KIGOGO mmoja aliyekuwa na dhamana kubwa katika Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), jina tunalo, ameweka mambo hadharani kwa kusema kuwa ametolewa kafara kwa kufukuzwa na kutuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za shirika hilo zinazokadiriwa kufikia Dola za Kimarekani 55,000.

Kigogo huyo alikiambia chanzo chetu jana jijini Dar es Salaam kuwa katika ubadhirifu huo hakuwa peke yake bali alishirikiana na vigogo wenzake wawili ambao mwisho wa siku wamemgeuzia kibao yeye.

Akizungumza kuhusiana na sakata hilo, kigogo huyo alibainisha kuwa alishirikiana na kigogo wa Uhandisi, na wa Rasilimali Watu.

"Mara ya kwanza Novemba 19, yule wa uhandisi alichukua dola 12,100 za mgawo kisha Januari 19 mwaka huu, akachukua tena 2,700 ambazo alisema ni za matibabu ya mwanae aliyepo Urusi baada ya kupata ajali mbaya nchini Ukraine na yule wa rasilimali watu Desemba 22 mwaka jana, alichukua dola 9650, kwajili ya mambo ya kifamilia na ujenzi wa dharura"

"Tulikubaliana kuwa tutaificha menejiment kuhusu uchotaji huo wa fedha na kisha wao wawashe moto kwa kuishtaki kampuni hiyo ya Kenya kwa kukiuka mkataba na kuidhalilisha kampuni yetu, pia hatukukubaliana kuwafukuza wafanyakazi wa chini lakini wamekiuka kwa kumfukuza cashia pasipo hatia" alisema kigogo huyo.

Aidha kigogo huyo alieleza kuwa washirika wake hao kwa pamoja walimgeuka na kumfanya yeye mbuzi wa kafara ilhali wanaufahamu ukweli wa mambo kuwa wote walihusika na walijua kinachotokea wakati wakiidhinisha wa fedha taslim.

"Wamenigeuka. Naomba na wao wachukuliwe hatua stahiki kama ile iliyochukuliwa dhidi yangu bila kupepesa macho. Wao ndiyo walioidhinisha ulipwaji wa pesa hizo ila leo wamenigeuka,"

"Kila kitu wanakifahamu na wao ndiyo waliahidi kuwa watashughulika na kuishawishi menejiment kufungua kesi za madai na fidia. Pia kama haitoshi wakaenda kuiambia bodi kuwa mimi ndiye niliewarubuni. Mungu atawalipa sawa na waliyonitenda mimi " alibainisha kigogo huyo.

Alisema kuwa fedha hizo ni sehemu ya malipo ya ndege waliyoikodisha toka Kenya, ambayo kila mmoja wao alikuwa akitambua kuwa malipo yote hufanyika kwa njia ya hundi na sio kwa fedha taslim.

Pia kigogo huyo alidai kuwa lengo lao lilikuwa kutaka kuishtaki kampuni hiyo, ambayo kesi hiyo ingechukua muda mrefu na hata uchotwaji wa fedha hizo usingejulikana.

"Kulikuwa na mkakati wa kuwasha moto mkubwa kwa kuishtaki kampuni hiyo ya Kenya na kuendesha kesi ambayo ingechukua muda mrefu kujua kama kulikuwa na uchotaji wa fedha hizo, maana katika mzozo huo ambao tungeanzisha kila mmoja wetu angetoa madai yake, hivyo isingekuwa rahisis kujua ni nani anambambikizia mwenzake lakini baada ya kubainika wenzangu wameruka kwenye kikao cha Bodi, hivyo nina amini mungu atanilipia tu" alidai kigogo huyo.

Alisema anashangaa kuona watu wamemgeuzia kibao na kuamua kutoa kwenye vyombo vya habari huku wakijua ukweli wa jambo hilo.


attachment.php

Mambo yenyea kama ni haya hata South Sudan watatushinda ikiwa Burundi wamesha tuacha bor
 
kaamua kuwangeleja wenzake ?.

kwa nini hawa watu, hawapelekwi mahakamani kwa wizi ?.

alafu JK yeye anacheka cheka tu.
 
Mnfanya wizi wenu kimya kimya alafu mkishabainika ndo mnaanza kutuzuzua ili kuzima soo...wewe uliyebainika ushughulikiwe kivyako kwanza hizo takataka nyingine zitafata...
 
Nimeona kichefuchefu kumalizia habari hii. Yaani bila aibu anasema wizi wake, sina huruma na watu hawa
 
Soma Vizuri mbona kataja humo,si unajua waandishi wetu makanjanja,jina tunalo halafu analeta story ya aliyefukuzwa kazi at the end wanataja kafukuzwa cashier.

sijaona jina, nimeona anaitwa "kigogo"

Nisaidie basi macho yangu mabovu
 
Only In Tanzania, mwizi bado yupo nje na anawataja wezi wenzake lakini serikali yote kama ipo Air port kusubilia ndege kwenda kubembea.....
 
siasa nyingi TZ yetu hakuna action yyte itakayochukliwa hapo dhidi ya watuhumiwa hao!!!
 
Back
Top Bottom