Kiganja alichonyea mtoto hakikatwi

Kiganja alichonyea mtoto hakikatwi

Joined
Sep 29, 2013
Posts
30
Reaction score
22
Leo Mida ya saa saba mchana nilienda kumtembelea jamaangu mmoja kwa mazungmzo zaidi ya kulainisha vyuma hivi vilivyoshikilia,. Nikiwa njiani narud home, nikakutana na zogo. Ipo hivi, nimekuta mzee mmoja anamfukuza binti yake wa kumzaa nyumbani kwasababu amegundulika ni mjamzito ilhali anaish nyumbani. Nimeshuhudia kwa macho yangu binti akiwa ameshikilia mlango kwa nguvu huku akilia "BABA NISAMEHE, NITAENDA WAPI MI I?" mzee akimvutia nje. ikanibidi nisogee na kumuuliza mzee kulikoni. Mzee akajibu "HAWA WATOTO WA KIKE NI HASARA, BORA WAKIUME KABISAAA" baada ya mazungmzo marefu na nasaha Za kutosha mzee akakubali japo kishingo upande binti kuingiza virago vyake ndani. Duh binti amenishukuru Sana. Kwani kupita kwangu imekuwa msaada kwake MY TAKE ;hakuna mtoto bora. Hata Hao wa kiume mbona siku hizi MASHOGA kibaooo
 
Mtoto wa kike kupatia mimba nyumbani ni aibu ya familia nzima

Siyakukothamela Sonini na nini
 
Umefanya jambo jema sana.Kwa kweli watoto wote tu teenagers ni mitihani sana.Ukikutana nayo ni balaa.Unamchunga kwa nasaha huyu asivute mibangi na yule kule awe msikivu asiwachekee wanaume.Omba sana usikutwe na bwana Pepsi!Utainywa kama chai-moto.
 
Kweli kabisa,lakini mtoto wa kiume kuwa shoga nako ni majanga tu.Tuombe uzazi mwema mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoto wa kiume tatizo kubwa analoweza kuleta katika familia no ushoga tu? Kuna madawa (hata wa kike), wizi /ujambazi ma hata kila siku kuja kubwagiwa watoto (mama tofauti).
Kwa kweli matatizo ya watoto ni tofauti na mengi na hata sijui lipi unaweza kusema lina afadhali ya lingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto wa kiume tatizo kubwa analoweza kuleta katika familia no ushoga tu? Kuna madawa (hata wa kike), wizi /ujambazi ma hata kila siku kuja kubwagiwa watoto (mama tofauti).
Kwa kweli matatizo ya watoto ni tofauti na mengi na hata sijui lipi unaweza kusema lina afadhali ya lingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuh!mzee mzima unaanza kupeleka mjukuu klinik tena.Anyway hakuna ulezi rahisi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom