steveachi
JF-Expert Member
- Nov 7, 2011
- 11,342
- 13,364
Habari wakuu,
Mimi ni mtumiaji wa hiki king'amuzi cha Startimes. Kuna hiki kifurushi kipya kilichoingia sokoni hivi karibuni kinachoitwa 'Nyota', Kiukweli kifurushi hiki kimejali hali ya mtu wachini kabisa kwani bei yake ni poa ni Tshs.4,000/= tu kwa mwezi.
Nawapa pongezi Startimes kwa kuangalia suala hilo. Kilichonisukuma kuweka uzi huu ni kuwa, nimejaribu kuangalia kwenye Facebook Page ya Startimes, tovuti ya Startimes, sijaona maelezo yoyote ya kutosha yanayoonyesha chaneli zilizopo katika kifurushi hiki.
Ombi langu kwenu ambao mnatumia king'amuzi hiki, naomba kujulishwa hiki kifurushi kina chaneli zipi ili kama vipi nijisubscribe huko nikiona zinanifaa.
Pia ushauri wangu kwa hii kampuni ya Startimes ni kuwa, wawe na taarifa za kutosha katika tovuti yao juu ya huduma mbalimbali wanazotoa kuliko kuja humu na kujaza seva ya JF tu kama nilivyofanya hapa wakati maelezo nayoyataka nilipaswa kuyapata katika tovuti yao. Tovuti yao ina taarifa za zamani sana tokea kifurushi cha 'KILI' kilipokuwa hakipo.
Ni vema watu wao wa IT wafanye kazi yao sio wanalipwa mishahara tu huku tovuti ikiwa haina masuala ya msingi mteja anayopaswa ataarifiwe..
Naomba kuwasilisha na karibuni kwa kuniambia chaneli zilizopo kwenye kifurushi cha 'NYOTA'.
Mimi ni mtumiaji wa hiki king'amuzi cha Startimes. Kuna hiki kifurushi kipya kilichoingia sokoni hivi karibuni kinachoitwa 'Nyota', Kiukweli kifurushi hiki kimejali hali ya mtu wachini kabisa kwani bei yake ni poa ni Tshs.4,000/= tu kwa mwezi.
Nawapa pongezi Startimes kwa kuangalia suala hilo. Kilichonisukuma kuweka uzi huu ni kuwa, nimejaribu kuangalia kwenye Facebook Page ya Startimes, tovuti ya Startimes, sijaona maelezo yoyote ya kutosha yanayoonyesha chaneli zilizopo katika kifurushi hiki.
Ombi langu kwenu ambao mnatumia king'amuzi hiki, naomba kujulishwa hiki kifurushi kina chaneli zipi ili kama vipi nijisubscribe huko nikiona zinanifaa.
Pia ushauri wangu kwa hii kampuni ya Startimes ni kuwa, wawe na taarifa za kutosha katika tovuti yao juu ya huduma mbalimbali wanazotoa kuliko kuja humu na kujaza seva ya JF tu kama nilivyofanya hapa wakati maelezo nayoyataka nilipaswa kuyapata katika tovuti yao. Tovuti yao ina taarifa za zamani sana tokea kifurushi cha 'KILI' kilipokuwa hakipo.
Ni vema watu wao wa IT wafanye kazi yao sio wanalipwa mishahara tu huku tovuti ikiwa haina masuala ya msingi mteja anayopaswa ataarifiwe..
Naomba kuwasilisha na karibuni kwa kuniambia chaneli zilizopo kwenye kifurushi cha 'NYOTA'.