WAISRAEL WATOA MAFUNZO KWA WALINZI BINAFSI WA LOWASSA Na Mwandishi Wetu. Taarifa za uhakika zimevuja zikieleza kuwa Kampuni ya MAX SECURITY SOLUTION ya nchini Israel imelipwa milioni 450 za Kitanzania kwa ajili ya tenda ya kuwapatia mafunzo ya ulinzi wa viongozi, walinzi binafsi wa mgombea Urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ndugu Edward Lowassa. Mafunzo hayo yanayoongozwa na Mwalimu wa Kiisrael aliyetajwa kwa jina moja la Shaul yanafanyika katika nyumba iliyoko maeneo ya Mbezi Beach. Baadhi ya vijana ambao wanaendelea kupokea mafunzo hayo ni pamoja na: Evance Benno Munembuka anayetumia namba ya simu ya mkononi (0717 291 979), Keneth Kunambi (0767 838 218, 0716 838 218), Yohana Sitta (0789 918 088), Buhimira Golani Mboje maarufu Spencer (0757 200 002), Kombo Mohamed (0717 030 311) na Saimon Chamila (0752 882 462). Wengine ni Ramadhani Magambo (0719 230 945), Msila Kombo (0713 746 181), Edward Iteba (0754 209 323), Johnstone Malunda (0758 758 183), Josephat Sosphter (0765 073 135) na Mussa Burhan (0786 185 881). Wanyetishaji wamezidi kueleza kuwa miongoni mwa mafunzo ambayo vijana hao wamepewa ni pamoja na namna ya kutengeneza ‘uzio' wa kumzunguka Lowassa akiwa katika halaiki ya watu, ulinzi wa gari lake, jinsi ya kutembea na kiongozi kwenye msongamano wa watu, namna ya kuwasiliana na namna ya kumuokoa kiongozi wao inapotokea ‘hatari ya ghafla'. Hata hivyo, imezidi kunyetishwa kuwa, walinzi hao wanaokaa kwenye Hoteli ya B & B ya Mikocheni huku wakilipwa shilingi laki tano kwa mwezi, wameambiwa wawe ‘tayari hata kutoa roho ya mtu' iwapo mazingira yataruhusu. Ingawa haikuelezwa iwapo kuna hatari yoyote ambayo wanadhani inamkabili kiongozi wao na kwanini tahadhali hiyo isitolewe kwa Jeshi la Polisi iwapo kuna tishio kubwa kama hilo, wanyetishaji wanasema kuwa kambi ya Lowassa imejiapiza kuwa vyovyote iwavyo ni lazima waingie Ikulu. Apson Mwang'onda, mkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, ndiye anatajwa kuwa msimamiaji mkuu wa suala zima la kuletwa kwa wakufunzi hao wa Kiisrael huku walinzi hao wa Lowassa wakipokea maelekezo moja kwa moja kwa kiongozi wao anayetajwa kwa jina la Aloyce Patrick Tendewa. Ni wazi kuwa taarifa hizi ni muendelezo wa taarifa za awali zilizowahi kuripotiwa na baadhi ya magazeti na mitandao ya jamii kuwa katika moja ya mikakati ya muda mrefu ya Lowassa, ni kuandaa kundi la vijana wa kufanya fujo katika maeneo mbalimbali kwa kisingizio cha kulinda kura ifikapo Oktoba 25, mwaka huu. Tayari zipo taarifa kuwa wapo, pia, vijana ambao wamepelekwa maeneo mbali mbali nchini na wengine nchini Rwanda, kwa ajili ya mafunzo ya ‘kuwaweka fiti' ili wawe na uwezo wa hata kusababisha maumivu makubwa ya kimwili na hata uharibifu wa mali kwa wapinzani wao, hususan wale watakaoonekana kuwa ni kikwazo kwa harakati zao za kuingia magogoni.