Kicheko cha mwisho cha mama yangu

Kicheko cha mwisho cha mama yangu

Joined
Mar 14, 2013
Posts
12
Reaction score
10
Kisa cha kweli..

Tayari kwa kulazimishwa nimekuwa yatima,nilikuwa kwenye msiba wa rafiki yangu mkubwa Mama yangu.ALIPIGANIA maisha yake vya kutosha lakini ugonjwa wa kansa ya matiti ukamshinda nguvu na kumuua na hakuna cha kufanya.

Moyo wangu ulikuwa unauma sana na mara kadhaa nilishindwa kupua vizuri,nakumbuka siku nilipotoka chuo kwenda kumuona mama hospitali,alikua anaumwa sana lakini tabasamu lake usoni liling'aa kama mwezi mwangavu akicheka na kunichekesha lakini akinisisitiza kusoma kwa bidii kuwa na hekma, busara na upendo kwa wakati wote wa maisha yangu.

Nilimsogelea mama kitandani alipokua amelala nikamwambia 'Mama nakupenda sana nataka bado kuishi na wewe usiniache peke yangu please'' ' Mama huku akicheka akaniambia sitakuacha peke yako mwanangu rudi chuo kesho tutaonana tena'' inauma sana kwani hiyo ndiyo siku ya mwisho kuongea na mama yangu kipenzi wakati huo mama ndie alikua ngome yangu kwani baba alikua amekwisha fariki miaka miwili iliyopita.

Nilikuwa namebaki na dada yangu ambae alikua na mtoto mchanga wa miezi miwili na kaka yangu mambae nae ndo kwanza kafunga ndoa wiki moja iliyopita.

Tukiwa kanisani,niliinua macho yangu nikamtazama kaka yangu pembeni sura yake imejaa simanzi mkono wake wa kuume amemshika mke wake,kisha nikamuangalia dada yangu kaweka kichwa chake mabegani mwa mume wake ambae mikono yake ilikuwa imeshika mtoto mchanga kabisa,harafu nikaangalia msaraba uliokuwa umeandikwa ''MAGRETHY'' jina la mama yangu na jeneza lilokuwa mbele yangu... hapana! sikuwa naamini kama kabisa kuwa mama katuacha na hatuko nae tena.

Mara kwa mshangao nikasikia mtu ananishika bega,nikageuka haraka kumtazama nikaona sura ya mwana dada mzuri na mlembo sana akaniambia..''Pole sana Rick,hata mimi mwaka jana nilimpoteza mama yangu kwa ugonjwa huu'' kisha akanikumbatia na kusimama nyuma yangu,nilishangaa sana,sikuwa namjua lakini yeye alionekana kunifamu vizuri

Baada ya misa,tulianza safari ya kwenda makaburini,ndugu,jamaa,marafiki,majirani na watu mbalimbali waliuwa nasi wakitufariji na kutoa mchango wa hali na mali nilishangazwa sana na upendo waliotuonyesha,wanachuo wenzangu na walimu hawakuwa nyuma wote walikuwa pamoja na mimi.

Wakati mgumu na mbaya kwangu ulikuwa ule wakati wa kuondoka baada ya kumaliza mazishi,nilishindwa kuondoka pale kaburini na kumuacha mama peke yake nililia sana sana,nikamulilia Mungu afanye muujiza wa kumfufu mama yangu lakini wapi.. haikuwezekana.

Nikiwa nimeinamia kaburi la mama nilikuwa imezungukwa na watu wengi ngugu zangu,kaka na dada,marafiki na wanachuo wenzangu,mara yule dada(mrembo alinistukiza kanisani) akatokea katikati yao,akaniamusha, akachukua kitambaa chake safi akanifuta machozi yaliyokuwa yakitililika kama maji akanikmbatia huku akinibembeleza kwa sauti ya upole na maneno yenye nguvu za ajabu akaniongoza hadi kwenye gari kurudi nyumbani.

Tulifika nyumbani na mambo ya msiba yaliendelea,baadae ilibidi nimuulize yule dada wewe ni nani na ulinifahamu lini? akajibu..'mimi naitwa MERRY nilikufahamu wakati unakuja kumuona mama yako hospitali,mimi na mama tulikuwa tunafahamiana mama yako alikuwa anamtembelea mama yangu wakati anaumwa na kila alipokuja nymbani alinikuta na hata baada ya mama kufariki mama yako aliendelea kunotembelea na kunijulia hali,alikuwa mtu mwema kwangu'' aliniambia menge sana na akaanza kulia...

Hata hivyo yote kwa yote,tulijipa moyo na Mungu alitupa nguvu katika wakati wa kipindi chote kigumu na kikubwa zaidi kuliko vyoote kwa sasa mimi Rick na Merry ni wachumba tunapendana sana tunatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

Nafikiri pamoja na mambo mengine MERRY ni zawadi kutoka kwa mama yangu na aliposema ''sitakuacha mwenyewe mwanangu'' alimanisha,na kweli hajaniacha peke yangu kaniacha na Merry kipenzi changu.Nampenda sana Merry na yeye ananipenda,Mungu tupe uzima na nguvu.
PUMZIKA KWA AMANI MAGRETHY...
PUMZIKA KWA AMANI MAMA YANGU MPENDWA...NAKUPENDA SANA.

Your son Rick..

LIKE & SHERE & COMMENT kuonyesha heshima na upendo.
 
Hata mimi mama amefariki jan 13 huu mwaka, nakumbuka neno la mwisho aliloniambia ni..............machozi.
 
Pole sana ndugu. Nashukuru mama alikuachia maneno ya busara sana na kama utayafuata utaishi kwa amani na upendo kwenye hii dunia. Mungu ampumzishe kwa amani mama yetu, Amen!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kisa cha kweli..

Tayari kwa kulazimishwa nimekuwa yatima,nilikuwa kwenye msiba wa rafiki
yangu mkubwa Mama yangu.ALIPIGANIA maisha yake vya kutosha lakini
ugonjwa wa kansa ya matiti ukamshinda nguvu na kumuua na hakuna cha
kufanya.

Moyo wangu ulikuwa unauma sana na mara kadhaa nilishindwa kupua
vizuri,nakumbuka siku nilipotoka chuo kwenda kumuona mama
hospitali,alikua anaumwa sana lakini tabasamu lake usoni liling'aa kama
mwezi mwangavu akicheka na kunichekesha lakini akinisisitiza kusoma
kwa bidii kuwa na hekma, busara na upendo kwa wakati wote wa maisha
yangu.

Nilimsogelea mama kitandani alipokua amelala nikamwambia 'Mama
nakupenda sana nataka bado kuishi na wewe usiniache peke yangu please''
' Mama huku akicheka akaniambia sitakuacha peke yako mwanangu rudi
chuo kesho tutaonana tena'' inauma sana kwani hiyo ndiyo siku ya mwisho
kuongea na mama yangu kipenzi wakati huo mama ndie alikua ngome yangu
kwani baba alikua amekwisha fariki miaka miwili iliyopita.

Nilikuwa namebaki na dada yangu ambae alikua na mtoto mchanga wa miezi
miwili na kaka yangu mambae nae ndo kwanza kafunga ndoa wiki moja
iliyopita.

Tukiwa kanisani,niliinua macho yangu nikamtazama kaka yangu pembeni
sura yake imejaa simanzi mkono wake wa kuume amemshika mke wake,kisha
nikamuangalia dada yangu kaweka kichwa chake mabegani mwa mume wake
ambae mikono yake ilikuwa imeshika mtoto mchanga kabisa,harafu
nikaangalia msaraba uliokuwa umeandikwa ''MAGRETHY'' jina la mama yangu
na jeneza lilokuwa mbele yangu... hapana! sikuwa naamini kama kabisa
kuwa mama katuacha na hatuko nae tena.

Mara kwa mshangao nikasikia mtu ananishika bega,nikageuka haraka
kumtazama nikaona sura ya mwana dada mzuri na mlembo sana
akaniambia..''Pole sana Rick,hata mimi mwaka jana nilimpoteza mama
yangu kwa ugonjwa huu'' kisha akanikumbatia na kusimama nyuma
yangu,nilishangaa sana,sikuwa namjua lakini yeye alionekana kunifamu
vizuri

Baada ya misa,tulianza safari ya kwenda
makaburini,ndugu,jamaa,marafiki,majirani na watu mbalimbali waliuwa
nasi wakitufariji na kutoa mchango wa hali na mali nilishangazwa sana
na upendo waliotuonyesha,wanachuo wenzangu na walimu hawakuwa nyuma
wote walikuwa pamoja na mimi.

Wakati mgumu na mbaya kwangu ulikuwa ule wakati wa kuondoka baada ya
kumaliza mazishi,nilishindwa kuondoka pale kaburini na kumuacha mama
peke yake nililia sana sana,nikamulilia Mungu afanye muujiza wa kumfufu
mama yangu lakini wapi.. haikuwezekana.

Nikiwa nimeinamia kaburi la mama nilikuwa imezungukwa na watu wengi
ngugu zangu,kaka na dada,marafiki na wanachuo wenzangu,mara yule
dada(mrembo alinistukiza kanisani) akatokea katikati yao,akaniamusha,
akachukua kitambaa chake safi akanifuta machozi yaliyokuwa yakitililika
kama maji akanikmbatia huku akinibembeleza kwa sauti ya upole na
maneno yenye nguvu za ajabu akaniongoza hadi kwenye gari kurudi
nyumbani.

Tulifika nyumbani na mambo ya msiba yaliendelea,baadae ilibidi
nimuulize yule dada wewe ni nani na ulinifahamu lini? akajibu..'mimi
naitwa MERRY nilikufahamu wakati unakuja kumuona mama yako
hospitali,mimi na mama tulikuwa tunafahamiana mama yako alikuwa
anamtembelea mama yangu wakati anaumwa na kila alipokuja nymbani
alinikuta na hata baada ya mama kufariki mama yako aliendelea
kunotembelea na kunijulia hali,alikuwa mtu mwema kwangu'' aliniambia
menge sana na akaanza kulia...

Hata hivyo yote kwa yote,tulijipa moyo na Mungu alitupa nguvu katika
wakati wa kipindi chote kigumu na kikubwa zaidi kuliko vyoote kwa sasa
mimi Rick na Merry ni wachumba tunapendana sana tunatarajia kufunga
ndoa hivi karibuni.

Nafikiri pamoja na mambo mengine MERRY ni zawadi kutoka kwa mama yangu
na aliposema ''sitakuacha mwenyewe mwanangu'' alimanisha,na kweli
hajaniacha peke yangu kaniacha na Merry kipenzi changu.Nampenda sana
Merry na yeye ananipenda,Mungu tupe uzima na nguvu.
PUMZIKA KWA AMANI MAGRETHY...
PUMZIKA KWA AMANI MAMA YANGU MPENDWA...NAKUPENDA SANA.

Your son Rick..

LIKE & SHERE & COMMENT kuonyesha heshima na upendo.

Kama filamu vile,Mungu awabariki
 
Da! Mungu atusamehe na kutufikisha salama siku saa ikiwadia ..4sure Ricky umeyafanya machozi yajae machoni,poleni sana!
 
Pole kwa msiba, na hongera kwa mchumba, ni vizuri ukatekelea ahadi yako kwa Merry,isije kukufariji leo kesho un amtosa. nakutakia kila la kheri.
 
Umenikumbusha mama yangu mpenzi, alichonambia mwisho, waangalie wadogo zako, bac navyowaangalia mpaka napitiliza sasa
 
Back
Top Bottom