GE2025 Kibonde: Nikiingia ikulu nitanunua Bombadia 70 ili kila Mtanzania apande ajisikie raha

GE2025 Kibonde: Nikiingia ikulu nitanunua Bombadia 70 ili kila Mtanzania apande ajisikie raha

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Makini, Coaster Kibonde, amefika mkoani Tabora kunadi sera za chama hicho, akisema kuwa endapo watapewa ridhaa ya kuongoza nchi, wataimarisha sekta mbalimbali ikiwemo afya na miundombinu ya usafiri wa anga ili kurahisisha shughuli za kiuchumi kwa Watanzania

“Serikali yangu itaenda kuboresha viwanja vya ndege nchi nzima na kuhakikisha Bombardier zinatua kila mkoa. Kwa kuanzia nitaagiza ndege sabini aina ya Bombardier,” ameongeza Kibonde



 
Mi wanachonifurahisha ni kua, wanongea lugha inafanana kabisa na maccm...mara wamsifie,mara wakazane na aman, aman, aman🤔matapeli haya yanatumika kulaghai wenye nchi.
 
Kuna mwingine kasema huko zanzibar akichaguliwa,atawasaidia wanawake kuwatafutia wanaume wa kuwaoa.
 
Mgombea wa urais kupitia tiketi ya Chama cha Makini, Coaster Jimmy, akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Kachoma, mkoani Tabora, ameahidi ndani ya siku mia za uongozi wake atahakikisha nchi inapata ndege 70 aina ya Bombardier zitakazotumika kusafirisha wananchi kwa gharama nafuu.

Amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha miundombinu ya usafiri wa anga nchini na kuongeza upatikanaji wa huduma bora za usafiri kwa Watanzania.

Aidha, Coaster Jimmy amewataka wakazi wa Tabora na Watanzania kwa ujumla kuitunza amani ya nchi na kuwapuuza watu wa mitandaoni wanaochochea migawanyiko, akisisitiza kuwa umoja na mshikamano ni msingi wa maendeleo.
 
Kuna mwingine kasema huko zanzibar akichaguliwa,atawasaidia wanawake kuwatafutia wanaume wa kuwaoa.
E23C89D0-1011-4F9E-AD08-9302704F689F.jpeg
 
Back
Top Bottom