Kibiti: Polisi yaua watu wanne(4) wanaodhaniwa kujihusisha na mauaji wilayani humo

Hivi tutadanganywa mpaka lini? Eti saa tatu usiku. Wahalifu halafu hapohapo wanahisiwa. Alikuwaje mhalifu? Alihalifu nini? Mlipiga risasi gizani? Hakuna wananchi jirani walishuhudia tukio? Miili iko wapi? Mbona tunaona picha mchana kweupe halafu tunawaona FFU tu na magari? Hizo silaha walizopata ziko wapi? Jamani hebu acheni kutufanya watoto basi. Hata sisi tunajua kujumlisha au kuunganisha nukta. AAARRRRRGHHHH TOO MUCH SASA
 
Hivi tutadanganywa mpaka lini? Eti saa tatu usiku. Wahalifu halafu hapohapo wanahisiwa. Alikuwaje mhalifu? Alihalifu nini? Mlipiga risasi gizani? Hakuna wananchi jirani walishuhudia tukio? Miili iko wapi? Mbona tunaona picha mchana kweupe halafu tunawaona FFU tu na magari? Hizo silaha walizopata ziko wapi? Jamani hebu acheni kutufanya watoto basi. Hata sisi tunajua kujumlisha au kuunganisha nukta. AAARRRRRGHHHH TOO MUCH SASA
Kwa hio wewe unaweza kutembea na SMG alafu usihisiwe kuwa ni mhalifu;
maana ukiwa na smg either wewe ni askari au wewe ni mhalifu, sio raia.
na vita ni muda wowote kama unataka mchana tu ndo watu waende maporini tutafeli mzee.
mchana ndo watu wameenda kufanya uchunguzi.
kazi isipofanyika unalalamika, ikifanyika unalaumu; Basi nenda wewe kibiti mchana ukarushiane risasi na wahisiwa.
 
ujinga usio na mfano..unaua Raia kwa kuhisi?? mi mwenyewe nikiona POLISI hua nakimbia na sijaiba wala sijakaba mtu ila SARE tu za mapolisi zinanikimbiza..ina mana na mimi ningekua kibiti saivi ningeweza kua mmoja wa WANAODHANIWA..shenzi kabisa!
Kwa hio na wewe una SMG?
acha povu, tafakari.
 
Mmmh! "Kikundi cha watu sita wote kwa pamoja kushambulia polisi alafu wa 4 wakauwawa lakini silaha zilizo kutwa ni 2!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Idadi ya watu katika Kikundi = 6
Silaha zilizokutwa = 2
Idadi ya watu waliokufa = 4.
Jumla ya silaha = 6.
Idadi ya watu waliokimbia = 2.
Silaha zilipotea = 4.
 
raia mwema anarushiana risasi na polisi kweli? tena na SMG?

Mwenyezi Mungu atawasimamia Polisi wetu, na ninaamini kwa 100% kuwa hao polisi hawakukutana na hao watu kwa bahati mbaya, ila ni Mkono wa Kuume wenye Nguvu wa Mwenyezi Mungu ndio uliowaongoza hao polisi!

Ashukuriwe Bwana wa Majeshi kwa kuwa hakuna askari wetu hata mmoja aliyeuwawa!
 
Kwa hio wewe unaweza kutembea na SMG alafu usihisiwe kuwa ni mhalifu;
maana ukiwa na smg either wewe ni askari au wewe ni mhalifu, sio raia.
na vita ni muda wowote kama unataka mchana tu ndo watu waende maporini tutafeli mzee.
mchana ndo watu wameenda kufanya uchunguzi.
kazi isipofanyika unalalamika, ikifanyika unalaumu; Basi nenda wewe kibiti mchana ukarushiane risasi na wahisiwa.
Acha fikra finyu. Jiongeze. Think twice n outside the box acha kuwa brainwashed. Fill the jigsaw puzzle first.
 
Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kuwaua wahalifu wanne wanaosadikiwa kuwa miongoni mwa wahalifu wanaoendesha mauaji katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji katika mapambano yaliyodumu kwa zaidi ya nusu saa katika kijiji cha Pagae wilayani Kibiti mkoani Pwani.



Akielezea tukio hilo Mkuu wa Oparesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas alisema tukio hilo lilitokea siku ya Alhamisi juni 29 majira ya saa tatu usiku kwenye barabara ya vumbi itokayo Pagae kuelekea Nyambunda ambapo Askari Polisi wakiwa doria walikutana na kikundi cha watu kinachokadiriwa kuwa na watu sita ambapo wahalifu hao baada ya kuona gari la Polisi walikimbilia vichakani na kuanza kuwarushia risasi Polisi.

Sabas alisema baada ya hali hiyo kutokea Askari nao kwa ujasiri walijibu na mapambano hayo yalidumu kwa zaidi ya nusu saa ambapo Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu wanne kwa risasi ambao baadaye walifariki dunia wakiwa wanapelekwa hospitali.

"Katika tukio hilo tumefanikiwa kupata silaha mbili aina ya SMG na magazine mbili pamoja na risasi 17 zilizokuwa zinatumiwa na wahalifu hao na hii ni dalili kuwa tunaendelea vizuri na oparesheni yetu ambayo inashirikisha vyombo vingine vya ulinzi na Usalama katika wilaya hizi tatu za Mkuranga, Kibiti, na Rufiji" Alisema Sabas.

Aidha Sabas ametoa wito kwa wahalifu wengine kuacha mara moja kufanya vitendo hivyo kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kufanya jitihada zote za kuhakikisha kuwa maeneo hayo yanakuwa salama na wananchi wanaishi katika hali ya amani na usalama.

Vilevile amewataka wananchi kutoa taarifa zitakazowezesha kupatikana wahalifu wengine ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anaishi kwa usalama ambapo kwa ambaye atakayetoa taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa wahalifu hao kiasi cha shilingi milioni kumi kitatolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro.


Chanzo: ITV

GOOD JOB,hasa kupatikana kwa silaha na kuwateketeza waliojaribu kuwashambulia askari wetu,wanaobeza hizi juhudi na kama wana mapenzi mema waende wakawasaidie askari wetu huko Kibiti tuone wao watafanya nini pindi watakapokuwa wakiaanza kushambuliwa kwa risasi .
Mungu awasaidie na mshinde vita hii muweze kuokoa damu zisizo na hatia,
 
Ukifikiria kwa makini hakuna anaeshabikia mauaji, sisi tunachotaka maelezo yafanane na ukweli wananchi wapate matumaini kuwa punde kutakuwa shwari, hivi majambazi na hatakama majangili wata take cover na watupe risasi pasipo kujeruhi imagine tendo lenyewe usiku, ok jeshi letu liko makini zaidi wao walipowaona walikuwa wakwanza kuteka cover na kuwapiga adui ndani ya dk 30! Fine adui walikuwa 6 na bunduki 4 ama 2 peke yake! Wawili walifanikiwa kukimbia na siraha ama watupu! Na hakuna technologia ya kujua hizo siraha 2 zimefanya tukio gani na gani?
 
Mpaka waseme wanadhaniwa! Kila kukicha tunaomba jeshi letu tukufu lifanye miujiza liwamalize hao wanaodhaniwa maadui ili watu wetu rufiji waishi kwa amani
 
Acha fikra finyu. Jiongeze. Think twice n outside the box acha kuwa brainwashed. Fill the jigsaw puzzle first.
Unawaza puzzles tu mzee, vitu vingine ni common sense.
You are trying to think too hard ndio maana unapoteza focus.
You are trying to color things that are already black and white in the own form.
 
Kwa jinsi navyowajua wale wauaji WA kibiti kuanzia ktk uvamizi Wao WA vituo vya polisi,ambush zao za magari ya polisi eti wameshambuliwa Bila Wao kumjeruhi hata polisi mmoja?na kwa jinsi navyowafahamu polisi kuanzia kale ka mkasa ka zombe,na siraha wanazotangaza wamezirudisha baada ya kuporwa kwao na kumbe ni uongo,Nina mashaka na Hao waliouawa kama kwel ni wahusika.
 
Hahaa ni Kweli Kabisa jaribu na wewe kubeba machine ili ushuhudie moto wa risasi harafu uje utujuze ukweli.
 
Ukifikiria kwa makini hakuna anaeshabikia mauaji, sisi tunachotaka maelezo yafanane na ukweli wananchi wapate matumaini kuwa punde kutakuwa shwari, hivi majambazi na hatakama majangili wata take cover na watupe risasi pasipo kujeruhi imagine tendo lenyewe usiku, ok jeshi letu liko makini zaidi wao walipowaona walikuwa wakwanza kuteka cover na kuwapiga adui ndani ya dk 30! Fine adui walikuwa 6 na bunduki 4 ama 2 peke yake! Wawili walifanikiwa kukimbia na siraha ama watupu! Na hakuna technologia ya kujua hizo siraha 2 zimefanya tukio gani na gani?
ww unacho taka kujua hapo ni nini haswa?? au HUKUPENDA majambazi kuuwawa??
 
Kwa jinsi navyowajua wale wauaji WA kibiti kuanzia ktk uvamizi Wao WA vituo vya polisi,ambush zao za magari ya polisi eti wameshambuliwa Bila Wao kumjeruhi hata polisi mmoja?na kwa jinsi navyowafahamu polisi kuanzia kale ka mkasa ka zombe,na siraha wanazotangaza wamezirudisha baada ya kuporwa kwao na kumbe ni uongo,Nina mashaka na Hao waliouawa kama kwel ni wahusika.
mashaka yako nini? Polisi wa TZ wapo vizur sana, usije ukaomba kukutana na moto wao mkuu
 
Back
Top Bottom