Kiapo cha daraja la umason

mshana jr nashangaa kwanini watu mnakomalia kuponda Freemasonry wakati kwa kadiri ninavyo fahamu hawana tofauti kubwa sana na organisations kama Rotary Club, Lions Club etc sema tu freemasonry ina mizizi ya siku nyingi na they are just much more secretive!!! Ila sidhani Freemasonry iko kama tunavyo danganyana huku mtaani..
 
Ivi mason ndo mpinga kristo mwenye alama 666
Freemason anaitwa mpinga Kristo kutokana na laana ya msalaba
Kumbuka maseremala wote(mason)walilaaniwa kwa kosa la kutengeneza misalaba iliyotumika Kuangikwa Yesu Kristo na wafuasi wake wawili waaminifu pale Golgota
Kwahiyo kujikinga na laana hiyo ndio walikuja na ibada ya kuitengua na ndio asili ya neno freemason au wajenzi huru
 
Hawajui tu na ni kweli kabisa freemason ya magazeti ya udaku ni tofauti kabisa na uhalisia wa kitu chenyewe
 
Mkuu mshana jr nadhani nahitaji ufafanuzi zaidi juu ya kulaaniwa maselemara wote??? Hii umeitoa wapi kiongozi??? Alafu kumbuka kuwa mpaka sasa bado kuna argument kubwa kuhusu origin ya Freemasonry na wengine wanaargue kuwa inawezekana imeexist even miaka mingi sana hata kabla ya Yesu..
 

Mkuu...katikati ya MUNGU na shetani inakua ni wapi hapo wapo hao watu?
 
Kwa hiyo hata yoseph babaye YESU hiyo laana ilimpitia
Hapana Soma habari zake mpaka mwisho! Wajenzi walikuja kulaaniwa baada ya kutengeneza misalaba wakati huo Yesu kushakuwa mkubwa tayari
Kitu kingine kipya nimekipata hapa
Wajenzi(mason) ndo waliounda msalaba lakini baba wa Yesu alikuwa mjenzi
 
mason=mwashi
 
Hapana bado hawajui nini maana yake na kama wapo basi ni wastaarabu kupita maelezo
Kinachotia wasiwasi ni hizi ibada zao kama wengi wasemavyo kuwa zinaambatana na kafara za umwagaji damu wa binadamu!..hili kama ni kweli basi hata mazuri yanayoonekana kufanywa nao hayafai sana kusifiwa...
 
Kwanini mason iwe jumuiya ya siri? Na kwanini walianza kwa siri?
 
Haya mambo ya freemanson nilianza kuyasikia miaka ya 90 lkn yalikuwa hayavumi kama sasa tena wa hall lao mitaa ya posta dar kwa Tz.kuna kaka yangu ndie alienza kutueleza ktk familia baada ya mtoto wake kupata ufadhili wa kwenda kusoma Marekani lkn alikitaa asiende huko kijana alikuwa fourm two.hao wafadhili walikuwa na vigezo vyao walikuwa wanangalia perfomance ya mtoto kuanzia chekechea mpk form two ambae anafanya vizuri ktk masomo ya hesabu na sayansi.mtoto wa kaka kichwa yupo vizuri na wala alikuwa hatumii nguvu nyingi kujifunza.kwa kweli familia tulimshangaa ndugu anakaa mtoto asiende Amerika.ndio hapo akatuekeza sababu za kukataa ni hiyo jamii ya freemason kuwa wapo wengi duniani na huwa wana mipango ya muda mrefu kufanikisha mambo yao.Na huwa kuna baadhi ya makundi ya watu wanawanda angali wakiwa wadogo wanawapa elimu na hiyo iman yao,alisema huwa wanahitaji wasanii maarafu,viongozi mahiri kifupi wapo ktk kila sekta.kuna wanajiunga wakiwa wakubwa na wengi wenyewe wana wandaa kwa faida yao.basi kijana alibaki Tz mpk akamaliza form six then akajiunga Kcmc kuchukua MD.sasa ni Dr.
 
Freemasons= mafundi huru

Zamani huko ulaya na mashariki ya mbali(kabla ya kipindi cha enlightenment) mafundi wote wa ujenzi walikua wako bound na master wao mmoja tu,yani hauwezi kufanya kazi kwa mtu mwingine wala kujenga ramani kama hiyo(ndio maana mfalme aliejenga Taj Mahal aliwakata mikono mafundi walivomaliza),chimbuko la ufreemason liko katika harakati za hawa mafundi kudai uhuru wao kutoka kwa masters wao .........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…