Swali langu kwa wana jf wajuvi wa sheria ni kwamba sheria ya ndoa inatambua wahusika wawili tu, na kama endapo mmoja atakiuka mfano kwenda nje ya ndoa au kumkataa mwenzie bila sababu za kimsingi basi upande ambao hautaridhika na maamuzi ya mwenzie anaweza kufungua kesi ya madai ama kupinga maamuzi ya kutengana huko bila kutofautisha ni mume ana mke mwenye haki hiyo, Sasa swali langu kuhusu swala la Mahimbo kufungua kesi dhidi ya Slaa ya Tzs bilioni moja kama fidia ya kunyang'anya mke naona kama sio sahihi maana kwa maelezo hayo Mahimbo alitakiwa kumfungulia Josephine kesi kama hiyo na sio Slaa kama ilivyo sasa maana yeye alifunga ndo na Josephine na ndiye aliye kiuka mkataba, ama mfano kama Mahimbo ndiye ange kiuka na kwenda kuishi na mke mwingine je Josephine nae angeweza kuwa na haki ya kumfungulia kesi mwanamke ange kuwa na mahusiano na Mahimbo na sio Mahimbo kama yeye Mahimbo alivyofanya kwa Slaa