Kesi ya kupinga wagombea wanaopita bila kupingwa kutangazwa washindi kuanza kusikilizwa leo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,035
144,400
Kesi kuanza kusikilizwa kesho

kesi ya kupinga wagombea wanaopita bila kupingwa kutangazwa washindi bila kupigiwa kura kuanza kusikilizwa kesho
a uliopo sasa unaoruhusu mgombea aliyeteuliwa na mamlaka za uchaguzi, kuwa mgombea pekee na kutangazwa kuwa 'amepita bila kupingwa' kutokana na sababu mbalimbali za kisheria, imepangwa kuanza kusikilizwa siku ya Jumanne, Septemba 3, 2019 mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Shauri hilo ambalo limesajiliwa rasmi wiki iliyopita Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam kwa kupewa namba 20/2019, litakuwa mbele ya majaji; Feleshi J, Masoud J na Maige J, ambapo mpeleka maombi Wakili Gaston Shundo Garubindi anaiomba Mahakama kuu itamke kuwa kifungu cha 44 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na kifungu cha 45(2) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (uchaguzi) Sura ya 292, vinakiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa maombi hayo, vifungu hivyo (44 na 45(2) vya sheria hizo mbili ambazo zinasimamia Uchaguzi Mkuu (Rais na wabunge) na Uchaguzi wa Madiwani mtawalia, na kuruhusu mamlaka ya uchaguzi kumtangaza mgombea pekee kuwa mshindi wa nafasi aliyogombea, bila kupigiwa kura na wananchi wa jimbo au kata husika kwa sababu ni mgombea pekee katika nafasi husika (kupita bila kupingwa), vinakiuka ibara ya 21 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Itakumbukwa kuwa Ibara ya 8 ya Katiba ya Nchi inazungumza kuwa Serikali itapata mamlaka yake kutoka kwa watu, huku ibara ya 21 ikielekeza kuwa watu wote wana haki ya kushiriki katika masuala ya utawala wa nchi, ikiwa ni pamoja na shughuli za uchaguzi ambao unahusisha haki ya kupiga kura na kupigiwa kura. Hivyo kutekelezwa kwa vifungu vya sheria hizo, si tu kunawanyima wananchi haki ya kikatiba ya kupiga kura na kupigiwa kura, bali pia kunaweka mazingira ya wananchi kutawaliwa na mamlaka ambazo hazijatokana na wao, kama Katiba inavyoagiza.

Wajibu maombi katika shauri hilo, ambao tayari wameshapelekewa na kupokea wito wa Mahakama Kuu ni; Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Maombi ya shauri hilo na. 20/2019 yamewasilishwa mahakamani hapo chini ya hati ya dharura na yamepangwa kuanza kusikilizwa kesho saa 3 asubuhi.

Imetolewa leo Jumatatu, Septemba 2, 2019 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
Mkuu samahani kama utakua umenizidi umri..... wewe ni kubwa jinga umetype uuharo tupu
 
Hongereni sana, haki hudaiwa .Tuwe na hoja za kutosha tudai tume huru ya uchaguzi kisha katiba bora.
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
Mbona viongozi wenu ndio wanaoongoza kwa kupigwa mawe?
Au ni kwamba mnakuwa mmetatua kero zaza wananchi hadi mmewafkisha kileleni, na kupigwa kwenu mawe ni matokeo tu ya raha za kufikishwa kileleni?
Maana hata kitandani kuna watu wakifika kileleni lazima wakung'ate hadi ukimbizwe Mloganzila
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
Dogo tatizo akili zako unajua mwenyewe
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
Very poor reasoning from a very poor mind.
 
Vipi kuhusu akina Mbowe kupita uenyekiti wa Chadema bila kupingwa hilo.mleta mada unalionaje?
Wewe ni mwendawazimu mwingine. Hoja iliyopo ni kuwa, hata kama mgimbea ni mmoja, ni haki wananchi wspige kura ya kumkataa au kumkubali.
 
CCM mmejenga ipi? Au ndi hizo zilizojengwa enzi za chama kushika hatamu? Au unazo mpya unazozijua tuwekee humu.
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.
 
CCM hupata uhalali wa kuongoza kutoka kwa wananchi kwakuwa inashughulika na matatizo na kero za watu. Siri ya ushindi wa uchaguzi kwa chama cha siasa ni hiyo na sio kushinda Mahakamani wakati hata kile mlichonacho mmeshindwa kukifanya vizuri, hizo fedha mnazotumia Mahakamani nendeni mjenge ofisi yenu ya Makao Makuu.

Nikukumbaka kipigo walichokipata wasimamizi wa uchaguzi wa cdm katika uchaguzi wa marudio kata fulani, tena kipigo hicho kiliendeshwa na polisi ili mgombea wa ccm atangazwe mshindi, nashindwa kujua msingi wa huu Utetezi wako. Kwa sasa nina ushahidi wa kutosha kwamba mwenyekiti wa ccm anatumia madaraka yake kunajisi box la kura ili mgombea wa ccm atangazwe mshindi, akiamini wanaccm wakichaguliwa kuwa viongozi basi ccm itapendwa. Ukweli ni kuwa kinachoendelea kwenye uchaguzi kwa sasa ni ubakaji wa demokrasia wazi wazi.
 
Back
Top Bottom