Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,348
- 26,145
Hoja kuu zilizompeleka Zitto Z.Kabwe mahakamani ni mbili.Kwanza, kuizuia Kamati Kuu cha CHADEMA kumjadili juu ya uanachama wake kufuatia barua aliyopokea ikibeba tuhuma 11 dhidi yake.Pili, kuiomba Mahakama imuamuru Katibu Mkuu wa CHADEMA kumpatia Zitto mwenenndo wa shauri lake ndani ya Kamati Kuu(siku alipovuliwa wadhifa wake) ili Zitto aweze kukata rufaa katika Baraza Kuu la CHADEMA.
Kesi hii imekuwa ikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini na nje kwa kukuzwa na kupotoshwa sana. Inazungumzwa kana kwamba ni vita ya kufa au kupona kwa mmoja wa pande za kesi hiyo. Kama si Zitto basi CHADEMA.Kwamba,baada ya hukumu ya leo ya Jaji Utamwa, Zitto au CHADEMA ataibuka kidedea na mwenzake atakuwa ameanguka na kuangamia kabisa.
Upotofu huu ndio uliosababisha yanayoshuhudiwa sasa.Kwamba eti kuna kundi la Zitto na CHADEMA. Kwamba eti kuna vurumai kubwa kati ya makundi hayo. Hakuna haja ya vurugu.Hakuna haja ya sherehe.Hakuna haja ya bifu. HAKUNA haja ya kujipongeza au kusikitika.Haki haihitaji uadui.
Kwa matokeo yoyote ya kimahakama leo, bado michakato ya kichama itaendelea.Kama Mahakama itakubaliana na maombi ya Zitto,basi kikao cha Kamati Kuu hakitamjadili juu ya uanachama wake.Pia, Zitto atapewa mwenenndo na Katibu Mkuu wa CHADEMA na kukata rufaa Baraza Kuu la CHADEMA.
Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.
CHADEMA imeshindwaje? Huo ndio upotofu ninaouzungumziaMbona kuna wanaosema kuwa chadema imeshindwa katika kesi mahakamani leo?ebu tujuzeni mliopo mahakamani.
Mbona kuna wanaosema kuwa chadema imeshindwa katika kesi mahakamani leo?ebu tujuzeni mliopo mahakamani.
U said it all Pal! thank yu!
Issue ni kwamba, kama Mahakama itakubaliana na Zitto ina maana CHADEMA kama tasisi itakuwa imepoteza point muhimu sana. Hukumu hiyo itadhihirisha kuwa CHADEMA si chama cha kufuata taratibu zaidi ya chuki binafsi na kukurupuka licha ya kuwa na katiba na mwanasheria machachari. Hilo halitakuwa jambo jema kwa taasisi inayokua na iyenye kujinasibu kuchukua dola siku za hivi karibuni. Kama kwenye issue ndogo tu ya mgogoro na mtu mmoja au wawili au watatu chama kinakiuka taratibu zake itakuwaje wakikabidhiwa nchi?
Tatizo ni kuwa ZZK kwa cdm bila yeye kuwa mwenyekiti ni bora isiwepo, au ikiwa chini ya Mbowe ni bora isiwepo pia. Na inakera anapowaita baadhi ya viongozi katika chama vifaranga. kiukweli hii inawachukiza wenye akili zao japo inawasaidia kuwadharau watu waliodhaniwa ni wakombozi.Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.
Issue ni kwamba, kama Mahakama itakubaliana na Zitto ina maana CHADEMA kama tasisi itakuwa imepoteza point muhimu sana. Hukumu hiyo itadhihirisha kuwa CHADEMA si chama cha kufuata taratibu zaidi ya chuki binafsi na kukurupuka licha ya kuwa na katiba na mwanasheria machachari. Hilo halitakuwa jambo jema kwa taasisi inayokua na iyenye kujinasibu kuchukua dola siku za hivi karibuni. Kama kwenye issue ndogo tu ya mgogoro na mtu mmoja au wawili au watatu chama kinakiuka taratibu zake itakuwaje wakikabidhiwa nchi?
Nisaidie MkuuHivi kweli umesoma bandiko la mleta mada au umesoma tu title?
Mwenzio anazungumzia matunda we unazungumzia nguo!!!! ----!!!
Hii inathibitisha kuwa wengi hawaelewi matokeo ya hukumu yana implication gani!Mbona kuna wanaosema kuwa chadema imeshindwa katika kesi mahakamani leo?ebu tujuzeni mliopo mahakamani.
Issue ni kwamba, kama Mahakama itakubaliana na Zitto ina maana CHADEMA kama tasisi itakuwa imepoteza point muhimu sana. Hukumu hiyo itadhihirisha kuwa CHADEMA si chama cha kufuata taratibu zaidi ya chuki binafsi na kukurupuka licha ya kuwa na katiba na mwanasheria machachari. Hilo halitakuwa jambo jema kwa taasisi inayokua na iyenye kujinasibu kuchukua dola siku za hivi karibuni. Kama kwenye issue ndogo tu ya mgogoro na mtu mmoja au wawili au watatu chama kinakiuka taratibu zake itakuwaje wakikabidhiwa nchi?
Hoja kuu zilizompeleka Zitto Z.Kabwe mahakamani ni mbili.Kwanza, kuizuia Kamati Kuu ya CHADEMA kumjadili juu ya uanachama wake kufuatia barua aliyopokea ikibeba tuhuma 11 dhidi yake.Pili, kuiomba Mahakama imuamuru Katibu Mkuu wa CHADEMA kumpatia Zitto mwenenndo wa shauri lake ndani ya Kamati Kuu(siku alipovuliwa wadhifa wake) ili Zitto aweze kukata rufaa katika Baraza Kuu la CHADEMA. Hivyo tu. Lakini,kinachoripotiwa ni tofauti. Hatuwezi kunyamazia upotofu.
Kesi hii imekuwa ikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini na nje kwa kukuzwa na kupotoshwa sana. Inazungumzwa kana kwamba ni vita ya kufa au kupona kwa mmoja wa pande za kesi hiyo. Kama si Zitto basi CHADEMA.Kwamba,baada ya hukumu ya leo ya Jaji Utamwa, Zitto au CHADEMA ataibuka kidedea na mwenzake atakuwa ameanguka na kuangamia kabisa.
Upotofu huu ndio uliosababisha yanayoshuhudiwa sasa.Kwamba eti kuna kundi la Zitto na CHADEMA. Kwamba eti kuna vurumai kubwa kati ya makundi hayo. Hakuna haja ya vurugu.Hakuna haja ya sherehe.Hakuna haja ya bifu. HAKUNA haja ya kujipongeza au kusikitika.Haki haihitaji uadui.
Kwa matokeo yoyote ya kimahakama leo, bado michakato ya kichama itaendelea.Kama Mahakama itakubaliana na maombi ya Zitto,basi kikao cha Kamati Kuu hakitamjadili juu ya uanachama wake.Pia, Zitto atapewa mwenenndo na Katibu Mkuu wa CHADEMA na kukata rufaa Baraza Kuu la CHADEMA.
Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.
Hoja kuu zilizompeleka Zitto Z.Kabwe mahakamani ni mbili.Kwanza, kuizuia Kamati Kuu ya CHADEMA kumjadili juu ya uanachama wake kufuatia barua aliyopokea ikibeba tuhuma 11 dhidi yake.Pili, kuiomba Mahakama imuamuru Katibu Mkuu wa CHADEMA kumpatia Zitto mwenenndo wa shauri lake ndani ya Kamati Kuu(siku alipovuliwa wadhifa wake) ili Zitto aweze kukata rufaa katika Baraza Kuu la CHADEMA. Hivyo tu. Lakini,kinachoripotiwa ni tofauti. Hatuwezi kunyamazia upotofu.
Kesi hii imekuwa ikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini na nje kwa kukuzwa na kupotoshwa sana. Inazungumzwa kana kwamba ni vita ya kufa au kupona kwa mmoja wa pande za kesi hiyo. Kama si Zitto basi CHADEMA.Kwamba,baada ya hukumu ya leo ya Jaji Utamwa, Zitto au CHADEMA ataibuka kidedea na mwenzake atakuwa ameanguka na kuangamia kabisa.
Upotofu huu ndio uliosababisha yanayoshuhudiwa sasa.Kwamba eti kuna kundi la Zitto na CHADEMA. Kwamba eti kuna vurumai kubwa kati ya makundi hayo. Hakuna haja ya vurugu.Hakuna haja ya sherehe.Hakuna haja ya bifu. HAKUNA haja ya kujipongeza au kusikitika.Haki haihitaji uadui.
Kwa matokeo yoyote ya kimahakama leo, bado michakato ya kichama itaendelea.Kama Mahakama itakubaliana na maombi ya Zitto,basi kikao cha Kamati Kuu hakitamjadili juu ya uanachama wake.Pia, Zitto atapewa mwenenndo na Katibu Mkuu wa CHADEMA na kukata rufaa Baraza Kuu la CHADEMA.
Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.
Hivi katika haya yooote mienendo yooote ya huyu dogo Z kuna CC na kuna baraza kuu kimaamuzi? namaanisha yaliyoonekana ni makosa katika CC yanaweza kuonekana ni mambo ya kawaida ama mazuri Baraza kuu na maamuzi yakawa Z abaki CDM? ikitokea hivyo mie naachana na siasa na ntajiondoa mwenyewe CDM,siwezi kuwa chama kimoja na msaliti wa hivi.[/quite]
uko sawa na mimi mkuu ikitokea hivyo basi bora niwepowepo tu katika maisha ya siasa lakini siyo mwanachama wa chama chochote