Idimulwa
JF-Expert Member
- May 27, 2011
- 4,503
- 1,722
Kuna tukio la uvamizi wa mgodi wa North Mara lilitokea na kupelekea mauaji ya raia kufanywa na jeshi la polisi wilayani Tarime.Tukio lile lilisababisha rabsha nyingi kama polisi kuvamia chumba cha maiti hospitalini Tarime na kuzichukua maiti za wahanga na baadaye kuzitelekeza barabarani,nikatika sakata hilohilo tulisikia habari za mbunge wa Tarime Mh.Nyambari kushambuliwa na wananchi kiasi kuchaniwa shati kisha kuokolewa na walinzi wake.Nikadhia hii hii ilipelekea Mbunge Tundu Lisu na wenzake kadhaa kutupwa ndani na kufunguliwa mashitaka,naomba kama kuna anayefahamu mwenendo wa kesi hii anijuze imefikia wapi kwani imekuwa ni muda mrefu sana zaidi inasikika ile kesi ya maandamano ya CHADEMA na ile ya kupinga matokeo ya ubunge kule Arusha.