Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Kesho kutakuwa na Kongamano la Katiba mpya kujadili changamoto zinazoukabili mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya hapa Tanzania. Kongamano hili litakalorushwa moja kwa moja na ITV, litafanyika katika Ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo Plaza-Dar es Salaam.
Watoa mada katika Kongamano hilo watakuwa waliokuwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Sinde Warioba, Profesa Mwesiga Baregu na Ndugu Awadh Ali Said. Kesho itakuwa ni zamu ya Wajumbe hawa wa zamani wa Tume kusema 'neno' juu ya Maoni ya Wananchi wa Tanzania waliyoyatoa na kuwekwa kwenye Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa katika Bunge Malum la Katiba.
Tayari,walishajitokeza mara kadhaa Wajumbe wengineo wa Tume ya Katiba na kutetea bila kupepesa macho maoni hayo ya wananchi. Wa kwanza ni Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Joseph Sinde Warioba.Jaji Warioba alifuatiwa na Prof.Palamagamba J.A.M.Kabudi na Ndugu Humphrey Polepole.
Mjadala unaendelea na wananchi wote mnakaribishwa.....
Watoa mada katika Kongamano hilo watakuwa waliokuwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Sinde Warioba, Profesa Mwesiga Baregu na Ndugu Awadh Ali Said. Kesho itakuwa ni zamu ya Wajumbe hawa wa zamani wa Tume kusema 'neno' juu ya Maoni ya Wananchi wa Tanzania waliyoyatoa na kuwekwa kwenye Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa katika Bunge Malum la Katiba.
Tayari,walishajitokeza mara kadhaa Wajumbe wengineo wa Tume ya Katiba na kutetea bila kupepesa macho maoni hayo ya wananchi. Wa kwanza ni Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Joseph Sinde Warioba.Jaji Warioba alifuatiwa na Prof.Palamagamba J.A.M.Kabudi na Ndugu Humphrey Polepole.
Mjadala unaendelea na wananchi wote mnakaribishwa.....