Kuna gari ya CHADEMA ya matangazo inapita jioni hii, kutakuwa na mkutano wa CHADEMA kesho jioni kwenye viwanja vya Mwembetogwa makamanda Godbles Lema na makamanda wengine watakuwepo hapo kuhutubia!
Kwani Iringa mjini na kalenga kuna umbali upi?
OK Kuna wanakalenga wanafanya shughuli zao na wanaishi Iringa Mjini ...
Kichwa umepewa cha kufugia nywele eh?
Yamewashinda ya Jimbo la Kalenga pamoja na kutumia helikopta kwa vile mikutano yao ilikuwa inajaa watoto kwa sasa wanataka wakakusanye watu angalau Iringa Mjini ili walete picha kwenye media mbali mbali kuonyesha kuwa wanakubarika Iringa.
Sera ya CHADEMA ya kuonyesha umati wa watu kama kigezo cha kukubalika imegonga mwamba katika Jimbo la Kalenga na wanachotaka ni kwenda Iringa Mjini ili kuifufua.
Nitashangaa sana kama picha za mkutano wao wa kesho Iringa Mjini hazitajaa kwenye media na hasa hapa Jf kwa sababu kujaza watu kwenye mikutano inayofanyika makao makuu ya mkoa siyo tatizo kwa vile mkutano ni sehemu ya leisure activities.
Huwezi kufanya maamuzi ya kibaguzi ndani ya chama na usalimike mbele ya Law of Karma. Law of Karma inakitafuna CHADEMA kwa sasa pole pole kama ilivyoonyesha kwenye chaguzi za madiwani tarehe 09/02/2014
wahisha rambirambi za kaka yake na mwigulu ulizokusanya! ukizipiga kama za Mwangosi utamtambua gaidi mkuu ni yupi hapa bongo,chezea rambirambi za wengine na si za mchemba!!