Kero za wapiga debe stendi Mwanza, Kahama Pakinyooka

Kero za wapiga debe stendi Mwanza, Kahama Pakinyooka

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
34,776
Reaction score
46,050
Niliwahi kuleta uzi hapa kuhusiana na wapiga debe Kahama. Nimefika stendi hii juzi mambo ni sawa kabisa. Hakuna bugudha za wapiga debe na kila kitu kipo shwari. Katika kuulizia kulikoni; nikapata habari kuwa, siku chache zilizopita kulifika ugeni mzito katika stendi hii akiwapo afande RPC wa mkoa na kunyoosha mambo ambapo wabugudha abiria kadhaa waliangukia mikononi mwa Polisi:

Kero za Polisi kwenye Stand za Mabasi TAKUKURU mnafahamu?

Sasa hebu angalieni hili la Nyashishi Mwanza katika hii clip ninayoambatanisha. Hapa wapiga debe wanakomaa kiasi cha kutaka kupiga hata mwakilishi mdau wa usafiri. Angalia tamko la Sumatra na la polisi katika sakata hii. Hakuna lolote kuhusiana na hawa wapiga debe. Indirectly si Polisi wala Sumatra Mwanza inayoonekana kujali wala kuhusika na adha ya wapiga debe hawa. Kwa maana nyingine kwa muonekano huo wapiga debe hawa wapo pale kihalali. Hawa wenye mamlaka, hawaoni hata mahusiano ya nauli hizi wanazojaribu kuongelea na tatizo la wapiga debe hawa ambao wako tayari hata kupigana kuhakikisha kuwa wanaendelea kuwapo hapo stendi.

Mwanza jifunzeni kwa njia zilizofuatwa kusuluhisha suala la wapiga debe Kahama. Wapiga debe hawa ni kero na chanzo cha usumbufu wote kwa abiria ikiwamo kuwaibia moja kwa moja au indirectly kwa kupitia katika nauli kama ambavyo sasa mnavyodhania kuwa wenye tatizo na hizo nauli ni hao madereva wa daladala. Kumbukeni kuwa wapiga debe hawa wanajipatia mapato kinyemela tokea katika nauli hizo hizo.

Kazi kwenu Mwanza wakati tunapo wapa pongezi Kahama na kuwatakia kheri kuwa hali ya sasa isije legezewa kamba.
 

Attachments

Hawa jamaa wanapata kiwango cha chini kabida 50,000 hadi 100,000 kwa siku.Ukiangalia kwa mwezi ni 1.5M na kwa mwaka ni 18M.Halafu TRA wanakuja na machine ya EFD kwa muuza duka anayeigiza 14M bila kujali gharama za mtaji,uendeshaji ikiwemo pango la frame,n.k.
Kama haitoshi hawa jamaa wanaonekana wana kipato kidogo na hivyo mtimishi anayelipwa laki 3 tu kwa mwezi anakatwa kodi.
Kuna kazi kubwa yapaswa kufanyika kuzuia mfumuko wa bei za nauli ili kufidia gharama kuwalipa wapiga debe
 
Usilifurahie hilo aisee hao jamaa wameingia mtaani saivi watu wanapigwa nondo kinoma hall sio shwari hata kidogo
 
Hawa jamaa wanapata kiwango cha chini kabida 50,000 hadi 100,000 kwa siku.Ukiangalia kwa mwezi ni 1.5M na kwa mwaka ni 18M.Halafu TRA wanakuja na machine ya EFD kwa muuza duka anayeigiza 14M bila kujali gharama za mtaji,uendeshaji ikiwemo pango la frame,n.k.
Kama haitoshi hawa jamaa wanaonekana wana kipato kidogo na hivyo mtimishi anayelipwa laki 3 tu kwa mwezi anakatwa kodi.
Kuna kazi kubwa yapaswa kufanyika kuzuia mfumuko wa bei za nauli ili kufidia gharama kuwalipa wapiga debe

Hawa jamaa wanajichukulia mapato makubwa sana. Inasemekana wanakula na mamlaka hizi kwa kuwaibia abiria na wenye mabasi. Mapato makubwa wanayohodhi kwa siku ndiyo ngao yao kubwa ya kuendelea kuwapo. Afande RPC Shinyanga bila shaka aliliona hilo na kuamua kuingia mwenyewe Kahama.

Mamlaka ondoeni wapiga debe hawa vinginevyo tunashawishika kuamini kuwa mnakula nao.
 
Usilifurahie hilo aisee hao jamaa wameingia mtaani saivi watu wanapigwa nondo kinoma hall sio shwari hata kidogo

Mkuu kama mtaani kumedoda hili ni jingine. Ila pale stand mkuu waingia na pikipiki yako kama unaingia kituo cha polisi hakuna hata nzi wa kukugusa.
 
Mkuu kama mtaani kumedoda hili ni jingine. Ila pale stand mkuu waingia na pikipiki yako kama unaingia kituo cha polisi hakuna hata nzi wa kukugusa.
Nilipita mwanza pale wamefukuzwa lakini unaambiwa huko mtaani Kila siku misiba miwili au mitatu ya watu waliopigwa nondo majeruhi ndio usiseme
 
Back
Top Bottom