Kero za huduma ya Simbanking toka CRDB

Kero za huduma ya Simbanking toka CRDB

Good Father

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2014
Posts
10,320
Reaction score
18,595
Mpaka naweka huu uzi yamenikuta na nimeshindwa kuvumilia.

Hi huduma ya simbanking ni hovyo mno kuliko nilivyokua nafikiria, nina visa viwili nitawaambieni.

Kuna siku nilikua nimekwama sana, nikaamua kuhamisha pesa kutoka benki kuleta tigo pesa, ilikua 60,000 TZS, pesa ilikatwa kwenye akaunti ila kwangu haijafika, nikawapigia simu kupitia namba hii 0714 197 700 nikawaeleza wakasema subiri 24hours, baada ya huo muda hakuna kilichotokea, nikapiga tena wakanipiga danadana nikapata hasira sana, niliamua kutafuta pesa kwingine, mpaka waliporudisha hilo 60,000 ni siku saba zilipita.

Kisa kingine kimenitokea juzi, niliamua kulipia bill ya king'amuzi kupitia simbanking, baada ya muda ikaja message hii "DSTV payment of TZS 00000 to 0000000000(namba yangu ya king'amuzi) failed with reason -Request expired 27-12-2017 12:58:27,

kuangalia akaunti pesa wamekata ila haijaenda Dstv, nikawapigia wakasema subiri 24 hours, baada ya 24 hrs nikapiga wakaleta drama zao.
Mpaka hivi ninavyozungumza pesa haijarudi na sijui itarudi lini.

Leo nikaamua kuwapigia kwa namba hii 0755 197 700 walichonijibu hata Sina hamu nao kabisa eti wanasema subiri mpaka Jumanne ya next week, seriously???? Bank kubwa Kama crdb inakua kama chama cha upatu?
Crdb upande wa simbanking mnaboa sana
 
Mimi nilihamisha 87000 siku ya jumatatu mpaka sasa haijarudishwa na walishanizulumu nyingi sana kwa njia hii!!
Hawa jamaa wanaanza kutusafishia njia ya kuwakimbia taratibu.
 
Wajinga sana hao simbanking crdb. Usijaribu huo upuuzi.
Kuna kipindi nilitoa kiasi flan Wakasema system down jaribu tena.
Nikajaribu mara ya kwanza ya pili na ya tatu.
Nikaona niache nikaenda kwenye atm.
Nikatoa pesa.
Jioni yale majaribio yote yakatuma zile pesa.
Wakawa wamekata kamisheni yao.

Nikawapigia kuwa nataka nijitoe simbanking kadada kakaniambia ukishajiunga umejiunga huwezi kutoka.

Nikakaambia pumbavu zako.
Dawa yenu ndogo.
Nikapasuabline nikaenda ku renew.
Ukirenew sim card operations zote sa simbanking zinastop.
Basi hadi leo sitaki huo upuuzi wao
 
Mimi nilihamisha 87000 siku ya jumatatu mpaka sasa haijarudishwa na walishanizulumu nyingi sana kwa njia hii!!
Hawa jamaa wanaanza kutusafishia njia ya kuwakimbia taratibu.
Duh pole mkuu ila Mimi ela yangu sitakubali ipotee kirahisi, ntafatilia mpaka waone kero, watarudisha tu iwe isiwe
 
Pole mkuu hii hutokea japo marachache Sana, milihamisha tsh 600k haikufika kwa Mpesa nikajipa moyo siku kama tatu bila kuona mabadiliko mpesa wala kurudishwa CRDB, zikapita kwa kuwa nilikuwa maeneo ya ndani Sana nikampigia mtu alikuwa town awaeleze kisa changu wakamwambia asiwaze itarudi kweli baada ya SAA kadhaa ikarudi CRDB, mara ya pili ilikuwa 200k this time siku hangaika zaidi ya kutafuta plan B kweli baada ya muda ilirudi so usihofu utarudishiwa!
 
Bas
Wajinga sana hao simbanking crdb. Usijaribu huo upuuzi.
Kuna kipindi nilitoa laki nne. Wakasema system down jaribu tena.
Nikajaribu mara ya kwanza ya pili na ya tatu.
Nikaona niache nikaenda kwenye atm.
Nikatoa pesa.
Jioni yale majaribio yote yakatuma zile pesa.
Wakawa wamekata kamisheni yao.

Nikawapigia kuwa nataka nijitoe simbanking kadada kakaniambia ukishajiunga umejiunga huwezi kutoka.

Nikakaambia pumbavu zako.
Dawa yenu ndogo.
Nikapasuabline nikaenda ku renew.
Ukirenew sim card operations zote sa simbanking zinastop.
Basi hadi leo sitaki huo upuuzi wao
Inategemea NTU na NTU wengine ndio mkobozi wetu, tumieni fahari Huduma ka vipi
 
Ni kweli wateja tumatofautiana sana mbona kwangu iko poa sana tangu nijiunge nao. Mpaka sasa nina miaka 12 wala sijawaza kwenda bank nyingine. Kuna wakati kadi ilisumbua miezi 2 nikawa natumia simbanking tu. Na mishahara unapitia hapo ila transaction zipo juu sana upande wa mpesa.
 
Ni kweli wateja tumatofautiana sana mbona kwangu iko poa sana tangu nijiunge nao. Mpaka sasa nina miaka 12 wala sijawaza kwenda bank nyingine. Kuna wakati kadi ilisumbua miezi 2 nikawa natumia simbanking tu. Na mishahara unapitia hapo ila transaction zipo juu sana upande wa mpesa.
Siku wakikuotea utajuta kuwafahamu.

Siko hapa kuharibu biashara ya mtu ila kwa hali hii ya simbanking wajipange, zama zimebadilika na zinazidi kubadilika wasidhani tuko 1960s
 
Siku wakikuotea utajuta kuwafahamu.

Siko hapa kuharibu biashara ya mtu ila kwa hali hii ya simbanking wajipange, zama zimebadilika na zinazidi kubadilika wasidhani tuko 1960s
Mkuu sina maana kwamba huduma Zao hazina changamoto ila mm sijapata.
 
Ivi kati ya simbaking crdb vs NMB Mobile Bank
IPI huduma ni nzuri angalau
 
Shit happens. Hilo hatukatai japo hatupendelei. Tatizo linakuja kutokea kwenye what I call 'after-shit' support. Yani msaada unaopewa baada ya tatizo kutokea. Inabidi wajitazame hapo.

Kumbuka pia hapa unaongelea interaction ya independent systems mbili: CRDB na Mobile Money. Ni challenge kubwa sana hii. When shot happens, sio kwamba hawataki kukurudishia hela yako - la hasha. Inabidi wajihakikishie kuwa systems zote mbili zinakubaliana kuirudisha hiyo hela kama ilivyo kwa muamala wowote ule. Ninachojaribu kusema ni kuwa inawezekana sio entirely CRDB's fault. Wanaposema usubiri 24 hours ni kwasababu ndani ya hayo masaa 24 special processes zinakuwa zimeshapita na kubalance vitabu vya hizo systems na hivyo zote zinakubaliana kukurudishia hela yako.
 
Mi sijawahi iamini hii huduma, na hapa ndo umenifanya niendelee kuamini nachokiamini
 
Pole mkuu hii hutokea japo marachache Sana, milihamisha tsh 600k haikufika kwa Mpesa nikajipa moyo siku kama tatu bila kuona mabadiliko mpesa wala kurudishwa CRDB, zikapita kwa kuwa nilikuwa maeneo ya ndani Sana nikampigia mtu alikuwa town awaeleze kisa changu wakamwambia asiwaze itarudi kweli baada ya SAA kadhaa ikarudi CRDB, mara ya pili ilikuwa 200k this time siku hangaika zaidi ya kutafuta plan B kweli baada ya muda ilirudi so usihofu utarudishiwa!
Sikatai kwamba hairudi mkuu, ila fikiria Sasa ndo huna plan B yaani hiyo plan ndo ulibakiza Kama plan B yako alafu nayo inabuma chukulia una mgonjwa au unasafiri safari ambayo ni muhimu sana na huwezi kusitisha, fikiria tu una any emergency alafu ni muhim kweli kweli.

Unaweza kujikuta unatembea njia nzima unaongea mwenyewe Kama mwehu
 
Shit happens. Hilo hatukatai japo hatupendelei. Tatizo linakuja kutokea kwenye what I call 'after-shit' support. Yani msaada unaopewa baada ya tatizo kutokea. Inabidi wajitazame hapo.

Kumbuka pia hapa unaongelea interaction ya independent systems mbili: CRDB na Mobile Money. Ni challenge kubwa sana hii. When shot happens, sio kwamba hawataki kukurudishia hela yako - la hasha. Inabidi wajihakikishie kuwa systems zote mbili zinakubaliana kuirudisha hiyo hela kama ilivyo kwa muamala wowote ule. Ninachojaribu kusema ni kuwa inawezekana sio entirely CRDB's fault. Wanaposema usubiri 24 hours ni kwasababu ndani ya hayo masaa 24 special processes zinakuwa zimeshapita na kubalance vitabu vya hizo systems na hivyo zote zinakubaliana kukurudishia hela yako.
Mkuu unaeleza vema sana ila hujui tu, niliwapigia wakasema kweli pesa imekatwa ila haijalipwa Dstv, tunaomba usubiri baada ya 24 hours tutakua tushawasiliana na Dstv tujue unaunganishwa au tunakurudishia pesa yako, 24 hours ni masaa 24 kwa kiswahili Sasa fikiria nililipa tarehe 27 mwezi huu, hayo masaa 24 bado hayajapita? Au mimi ndio sijui kusoma mkuu nisaidie hapo!!! Alafu leo wananiambia nisubiri mpaka Jumanne ina maana wanasema ngoja kwanza sikukuu ipite, hivi hiyo hela ni yangu au nawaomba msaada? Wanaudhi sana hawa watu
 
Back
Top Bottom