Kero ya baadhi ya Benki kukataa kupokea pesa mbovu kutoka kwa wateja wao

siriyaki

Member
Feb 21, 2016
50
47
Wadau, mimi ni wakala wa shughuli za M-Pesa na za kibenki, nimekuwa nikipata shida sana ninapopeleka pesa mbovu benki ambazo nimezipokea kutoka kwa wateja ambao wanakuja kupata huduma ofisini kwangu.

Watu wa benki wanasema pia wao wanahojiwa na BOT pesa mbovu wanazipata wapi? Wakati kiuhalisia pesa mbovu lazima zipo katika mzunguko.

Kwa jinsi ninavyojua Benki yoyote Tanzania ni kama Wakala wa BoT (act as ana agent of BoT) hivyo wateja wao wanapopeleka pesa mbovu inatakiwa wawahudumie. Wanapozikataa sasa wateja wazipeleke wapi? Hili limekuwa Kero sana kwa wateja.

Naomba kujua utaratibu upoje kuhusu hizi pesa mbovu ambazo mtoa huduma wa biashara za kawaida anapokea kutoka kwa wateja azipeleke wapi?
 
Wadau, mm ni wakala wa shughuli za Mpesa na za kibenki ila nimekuwa nikipata shida sana napopeleka pesa mbovu benki ambazo nimezipokea kutoka kwa wateja ambao wanakuja kupata huduma ofisini kwangu. Watu wa benki wao wanasema pia wao wanahojiwa na BOT pesa mbovu wanazipata wapi? wakati kiuhalisia pesa mbovu lazima zipo katika mzunguko.

Kwa jinsi navyojua Benki yoyote Tanzania ni kama wakala wa BOT (act as ana agent of BOT) hivyo wateja wao wanapopeleka hela mbovu inatakiwa wawahudumie wanapozikataa sasa wateja wazipeleke wapi? Hili limekuwa #kero sana kwa wateja.

Naomba kujua utararibu upoje kuhusu hizi pesa mbovu ambazo mtoa huduma wa biashara za kawaida anapokea kutoka kwa wateja azipeleke wap?
Toa taarifa BOT
 
Zamani kidogo wakati naenda kuweka hela benk(helazamadafu)nyingine zinakuwaga mbovu ila walikuwa wanapokea.

Dada mmoja rafiki yangu enzi hizo akaniambia hizo helambovu hazirudi tena kwenye mzunguko zinaenda kukatwa katwa then zinaingizwa mpya kwenye mzunguko.

Sasaivi siendi benki kuweka labda kutoa tuu.

Soo far hata Sheli wanapokea hela mbovu nao wanasema wanazipeleka benki.
 
Wadau, mm ni wakala wa shughuli za Mpesa na za kibenki ila nimekuwa nikipata shida sana napopeleka pesa mbovu benki ambazo nimezipokea kutoka kwa wateja ambao wanakuja kupata huduma ofisini kwangu. Watu wa benki wao wanasema pia wao wanahojiwa na BOT pesa mbovu wanazipata wapi? wakati kiuhalisia pesa mbovu lazima zipo katika mzunguko.

Kwa jinsi navyojua Benki yoyote Tanzania ni kama wakala wa BOT (act as ana agent of BOT) hivyo wateja wao wanapopeleka hela mbovu inatakiwa wawahudumie wanapozikataa sasa wateja wazipeleke wapi? Hili limekuwa #kero sana kwa wateja.

Naomba kujua utararibu upoje kuhusu hizi pesa mbovu ambazo mtoa huduma wa biashara za kawaida anapokea kutoka kwa wateja azipeleke wap?
Nafikiri hayo ni makosa binafsi ya mtoa huduma uliyekutana naye counter. Angalia hapo kwenye tawi la benk unayopata huduma kuna ofisi ya Manager wa tawi umjuze ulicho ambiwa atakusort.

Hata ukiuliza tu mlinzi hapo akuoneshe ofisi ya manager atakusaidia. Pole kwa changamoto uliyopata.
 
Nafikiri hayo ni makosa binafsi ya mtoa huduma uliyekutana naye counter
Angalia hapo kwenye tawi la benk unayopata huduma kuna ofisi ya Manager wa tawi umjuze ulicho ambiwa atakusort. Hata ukiuliza tu mlinzi hapo akuoneshe ofisi ya manager atakusaidia...
Pole kwa changamoto uliyopata na wala huna haja ya kutaja jina la Benki hapa kwani inaonekana kilichotokea ni kosa binafsi la mtoa huduma na sio benki....
Nilifika TCB Tegeta, Afisa msaidizi wa manager akasema wao wanaulizwa na BOT wanatoa wapi pesa mbovu wakati huo nimeenda na Tsh lak 9 wakapokea laki 3 tu.
 
Kuna siku mimi bank walikataa kupokea elf5 zilizokuwa laki5. Eti muda wa kuhesabu haupo, ilikuwa around saa 9.
Yes wana uvivu fulan ambao unakera, kwenye swala hela mbovu wanaweza wakaona uvivu kuhesabu hivyo wakaamua kusema hawapokei
 
Back
Top Bottom