Kero na Ufumbuzi wa tatizo la usafiri wa UDART

msani

JF-Expert Member
Jun 13, 2011
1,801
1,191
Tatizo la Usafiri DSM bado ni kero kubwa sana.

Serikali ilikuja na mpango wa kutatua tatizo la usafiri dsm kwa kuanzia UDART kwa barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi kivukoni, kariakoo, na Morroco, na hivi majuzi wakaanza kufaulisha kuelekea Muhimbili, na pia kutoka Mbezi hadi kimara mwisho.

Matarajio ya wengi ilikuwa ni kupunguza tatizo lakini kwa tathmini ya haraka kwa yaliyonikuta kimara ingawa sio mkazi wa huko ila jumatatu hii nilianzia safari huko. Kwakweli naomba niseme kuna tatizo kubwa sana limeongezeka.
-Watu wanakaa muda mrefu sana kituoni. Yaani mimi nilikaa lisaa lizima nasubiri gari
-Idadi ya magari ni machache mno
-Watu ni wengi sana sana wanapigania magari na wala sio kugombea tena.
-Upatikanaji wa tiketi ni shida kubwa.

Najua kuna watu watakuwa wanatoka mbezi wanahitaji kufika ubungo au sehemu yoyote isiyozidi ubungo basi nashauri UDART waruhusu gari zao zisiishie Kimara mwisho bali zifike ubungo, yaani kutoka mbezi zishushe hadi ubungo kwani watakuwa wamepunguza tatizo.
Idadi ya magari iongezwe.

Naamini kuna kero nyingi mno mno na sisi watumiaji tunaweza kuwasaidia ili kuboresha hali ya usafiri kupunguza kero kama lilivyokuwa lengo la serikali ya JK.

Tuwashauri tu hapa

Nawasilisha
 
Zungumzia na kuibiwa kwa, tiketi tunazotupa ktk dusty bin zilizo ndani ya muda bado zinarudishwa dirishani na kuuzwa tena.
 
Tatizo la Usafiri DSM bado ni kero kubwa sana.

Serikali ilikuja na mpango wa kutatua tatizo la usafiri dsm kwa kuanzia UDART kwa barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi kivukoni, kariakoo, na Morroco, na hivi majuzi wakaanza kufaulisha kuelekea Muhimbili, na pia kutoka Mbezi hadi kimara mwisho.

Matarajio ya wengi ilikuwa ni kupunguza tatizo lakini kwa tathmini ya haraka kwa yaliyonikuta kimara ingawa sio mkazi wa huko ila jumatatu hii nilianzia safari huko. Kwakweli naomba niseme kuna tatizo kubwa sana limeongezeka.
-Watu wanakaa muda mrefu sana kituoni. Yaani mimi nilikaa lisaa lizima nasubiri gari
-Idadi ya magari ni machache mno
-Watu ni wengi sana sana wanapigania magari na wala sio kugombea tena.
-Upatikanaji wa tiketi ni shida kubwa.

Najua kuna watu watakuwa wanatoka mbezi wanahitaji kufika ubungo au sehemu yoyote isiyozidi ubungo basi nashauri UDART waruhusu gari zao zisiishie Kimara mwisho bali zifike ubungo, yaani kutoka mbezi zishushe hadi ubungo kwani watakuwa wamepunguza tatizo.
Idadi ya magari iongezwe.

Naamini kuna kero nyingi mno mno na sisi watumiaji tunaweza kuwasaidia ili kuboresha hali ya usafiri kupunguza kero kama lilivyokuwa lengo la serikali ya JK.

Tuwashauri tu hapa

Nawasilisha

Licha ya uchache wa mabasi yenyewe jumapili wanayapunguza wanaamini watu wengi hawaendi makazini_ ndo hali inazidi kua mbaya

nauli ya kwenda na kurudi kariakoo ni 2100 tofauti ya zamani kabla ya mwendokasi ilikuwa 1000, kifupi wameongeZa shida
 
Swali langu kwa uongozi wa UDART..Kwanini mmeondoa ruti ya Morocco - Kimara jioni??mnatusababishia matatizo sana sana kwanza abiria tupo wengi tunaoenda Kimara zaidi ya sehemu nyingine yoyote ila cha ajabu mmeifuta root ya Kimara na kutaka kutupeleka ubungo kutubwaga hapo..sio fair kabisa na mabasi ya Morocco - Kimara kwa asubuhi ni machache mnoooo kwani shida ni nini? kwani ni nauli hatulipi au kero hii sababu zake ni zipi??
 
Alafu ukipita pale jangwani unayakuta kibao kwenye yard hao. Yale mabasi ni shida sana aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom