Bosi Michembe
JF-Expert Member
- Jun 24, 2011
- 271
- 87
Bujibuji mambo gani tena haya kaka yangu? Ile helicopter waliopanda hao viongozi imelipuka angani na kuanguka ikiwa imeharibika, si nzuri kama uliyoonyesha wewe. Na kwa uzuri zaidi mimi kwa wakati huu niko mjini Nairobi katika mihangaiko yangu ya kuitafuta shillingi, na Citizen TV wanaonyesha hiyo crash site ni porini (Kibiku forest, maeneo ya Ngong); na helicopter yenyewe iko nyang'anyang'a.
Ila kuna mambo mengi yanasemwa kuhusu ajali hii hapa Nairobi, mosi, rubani aliyekuwa amepangwa awali kajitoa dakika za mwisho ndipo akateuliwa mwingine (Madam Nancy Githuana) ambaye ndiye amekuja pata ajali na amefariki; pili miili ya waliokuwemo kwenye ndege imeungua haitambulikani, lakini pesa walizokuwa wamebeba kupeleka kwa fund raising hazikuungua kuteketea. Makubwa, lakini ndiyo hivyo, Prof George Saitoti, Naibu wake Orwa Ojode, walinzi wao wawili na marubani wawili wamefariki. Mwenyezi Mungu aweke roho zao mahali pema peponi.
View attachment 56013View attachment 56014
R. I. P. Saitoti. Umekuwa waziri tangu nipo primary hadi nimemaliza chuo na kazi kwa miaka ya kutosha. Angalau Mungu amekuondoa Madarakani maana hata ungefikia miaka mia bado usingeridhika! Umetuthibitishia kuwa ni kweli "binadamu hatosheki" na "Mungu ndiye muweza wa yote". Byebye.
kookolikoo
kumbe huwa unasikiliza Radio Uhuru ya CCM! Nami nimesikia taarifa hizo.
Mh. Saitoti na Naibu wake Orwa Ojode wamefariki kwenye ajali ya
Helkopter ya Polisi huko Ngong. Mungu aiweke pahala pema peponi roho ya
professor huyu wa Hesabu na mwanasiasa nguri katika siasa za
Kenya.
Kwa hivyo mama mdogo katuingiza choo cha kiume wote sasa?Bujibuji ulitaka kutuingiza choo cha kike,nashukuru wana JF kwa kuwa makini shukrani za pekee kwako mama mdogo kwa kuweka mambo sawa!!!R.I.P wote waliopata ajali.
Acha kudanganya watu helcopter waliodondoka nayo hata vipande havionekani yaani vipo vidogo sana.Wameonyesha citzen exclusive picture ya helcopter yenyewe yaani ni imeisha kabisa.Wewe hiyo ya kwako umeitoa maktaba ya ajali nyingine
RIP Saitoti.WaKenya poleni sana msiba mzito sijui huyu Prof Saitoti alikuwa camp ya Uhuru au Raila isije ikawa ni mikakati ya uchaguzi.
...Filipo, did i get you correctly? It seems unaona afadhali MUNGU amemwondoa duniani kwa kuwa alikua anang'ang'ania vyeo?! kama ndivyo ulivyomaanisha i'm so sorry for you kwani KIFO ndugu yangu sio cha kushangilia hata kama aliyekufa ulikua humpendi vipi!! Kuwa na moyo wa kibinadamu. Kumbuka Prof Saitoti alikua na watoto ndugu marafiki, admirers, etc. Dont hurt their already hurt feelings!.
Nimesikituishwa mno na kifo cha Prof Saitoti, R.I.P. Prof!. Niliwahi kusikia miaka ya nyuma kuwa kuwa huyu jamaa ni mmasai wa TZ japo ameamua ku-base maisha yake zaidi Kenya (yaani wazazi wake walitokea huku wakahamia Kenya). kama kuna anayejua zaidi tueleweshane jamani...