JokaKuu
Platinum Member
- Jul 31, 2006
- 30,442
- 55,007
Kwa njia moja au nyingine, lazima tutajikuta kwenye ushindani ndani ya hii dunia, haya mambo ya kuogopa ogopa, eti tufunge hapa, tufungue pale, tuzuie hawa, tufungulie wale hayatatufikisha mahali.
Leo hii nipo kwenye mradi fulani na wadau kutokea Mauritius, jamaa wananisimulia jinsi nchi yao imepiga hatua kwa kutozuia zuia.
Afrika yetu hii, tuache uvivu na ujinga, tukumbatie ushindani. Bongo bado inaliwa na kutafunwa pamoja na kwamba mnazuia zuia na kufunga funga.
..interesting observation.
..lakini mimi naona "kufunga hapa" na "kufungulia kule" zote ni mbinu za ushindani.
..sasa hivi Tz tumepata Raisi ambaye hapendi huu ujinga wa nchi yetu kufanywa shamba la bibi. Wacha tuone atatufikisha wapi.