Kazi ya Mgambo

Kazi ya Mgambo

Joined
Mar 10, 2015
Posts
17
Reaction score
0
Habari za asubuhi, mchana, jioni,

Natangaliza heshima kwenu na administration nzima ya JF,

Mimi ni askari mgambo nilihitmu mafunzo yangu ya awali mwaka 2013 wilayani Missenyi, mkoani Kagera. Kutokana na tatizo la ajira wilayani na vituo vya police kua finyu niliajiriwa kwenye kampun ya ulinzi hapa Bukoba mjini lakini ukweli ni kwamba haya makampuni wanatuibia sana.

Mkataba na mteja ni 150,000 lakini mi nalipwa 80,000 nazo kwa usumbufu na kucheleweshwa! Tarehe 20 leo bado nadai mshahara wa mwezi wa 4! Nina mpango wa kuacha kazi na kurudi kijijini nikalime tu, siwezi kuwadharau nisiowajua. Naomba panapo nafasi au dili flani nisaidiwe. Nami nitashukuru.
 
mkuu mbona kuna makampuni yanalipa vizuri? eg kk security.......... apply kijana achana na wazinguzi hao....... bt vigezo uwe umemaliza form 4 au 6..........uwe na living certificate form 4 or 6......... vigezo vingine kawaida tu...... pia na urefu aseh
 
mkuu mbona kuna makampuni yanalipa vizuri? eg kk security.......... apply kijana achana na wazinguzi hao....... bt vigezo uwe umemaliza form 4 au 6..........uwe na living certificate form 4 or 6......... vigezo vingine kawaida tu...... pia na urefu aseh

mbona nasikia eti nayo ni walewale tu!
 
mbona nasikia eti nayo ni walewale tu!

Aisee kk security hata mimi nilisikia inalipa vizuri sana, halafu kazini sio kila siku, unaweza kupata muda wa kupumzika hata siku moja kwa wiki, hii niliiona kwa jamaa mmoja; tena nasikia hata bima ya afya unaweza kukatiwa.
 
Back
Top Bottom