Kauli ya Mwapachu Kuhusu Lowassa

Bukanga

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2010
Posts
2,857
Reaction score
1,937
Ndugu zangu,

Nimekuwa kimya kwa muda mrefu katika mabadilishano ya fikra kwenye mtandao huu ambao kwa hakika, kwa maoni yangu, haubidi kuwa ni wa fikra pevu zisizo shawishika na misimamo ya 'kimalaya ya siasa'. Kama tutaserereka katika msingi huu, basi ni bora Chambi ukafunga virago na kusitish huu mtandao. Nimesoma mabadilishano na mabishano ya fikra kuhusu hali ya siasa nchini mwetu na hususan baada ya Mhe Lowassa kuamua kujiunga na Chadema na kuwa mwakilishi wa UKAWA katika kinyang'ariro cha nafasi ya Urais wa Jamhuri yetu ya Muungano. Sijui nyie wenzangu mmesimama au mmesimamia wapi katika suala hili.

Naomba niseme mwanzoni kabisa kwamba nchi yetu hii leo imefikia mahali ambapo wasomo, wanazuoni kama sisi katika mtandao huu, Hatuna budi kujitokeza na kuhesabika tunamuunga nani mkono katika uchaguzi ujao wa Rais wa Tanzania. Tuwe wakweli na siyo kuendelea kuegemea katika kificho cha 'uhuru' wa wanazuoni katika kutoa maomi na fikra kama vile sisi si wapiga kura au wananchi wanaothamini umuhimu kuhusu uongozi wa nchi yetu. Wakati huo umepitwa na hali halisi ya itikadi na maana muhimu ya uongozi wa Taifa.

Sasa, Mimi binafsi, namuuunga mkono Edward Ngoyai Lowassa. Yako mengi ambayo kazuliwa huyu ndugu yetu; tunaambiwa tangu 1995 wakati Mwalimi Juluis Nyerere alipo tamka kwamba 'huyu kijana ninalo file lake; ana utajiri usiyoelezeka. Ana nyumba kadhaa.' Lakini huyo huyo Baba wa Taifa alimpenda sana Edward na kumpa madaraka ndani ya CCM na baraza la mawaziri. Kama Edward alikwa 'corrupt' swali ni kwaninini Baba wa Taifa hakumchukulia hatua za kisiasa na kisheria? Kwanini aseme hayo aliyoyasema mwaka 1995 wakati Edward Lowassa alikuwa akiongoza kupendwa dani ya CCM, ngazi zote na akitarajiwa ndiye angependekezwa kuw mgombea wa Urais? Jamani, wanazuoni, lazima mtafakari historia na hali halisi ilivyokuwa. Mhe Jakaya Kikwete hakuwa 'the favourite' candidate in 1995. Na Mwalimu alimtaka Ben Mkapa wakati ule awe Rais. Ilibidi Lowassa atoswe ki namna!

Mimi namfahamu Edward. Ninyi mnaujua huo utajiri wake au basi akitoa michango hapa na pale ni pesa zake? Kati yenu mna utajiri zaidi ya Edward. Edward alivumilia na kumsaidia mwenzake (nasita sasa hivi kutumia neno 'rafiki') Jakaya ashinde uteuzi wa mgombea wa CCM hapo 2005. Aliamua hivyo baada ya makubaliano ya 1995. Wapo wengi wa Tanzania waliyojitolea muhanda, wa hali na mali kuungana na Edward kumwezesha Jakaya Kikwete kuwa Rais 2005. Kati yao, ndiyo wamekuwa karibu na Edward katika kinyang'anyiro cha majuzi Dodoma. Imani yao ilikuwa kwamba pamoja na mkanganyiko wa Februari 2008 wa Richmond ambao hauna mashiko yoyote ya ufisadi kwa maana ya rushwa, Rais Kikwete angemfungulia mlango mwenzake Edward kuwa mgombea wa CCM. Badala yake Edward bado akajengewa mzengwe wa utajiri kama Baba wa Taifa alivyofanya 1995. Hivi leo tukichambua nani kati yetu ni tajiri zaidi ya Lowassa tutakuwa na viongozi wanao kidhi mategemeo yetu?

Kuhusu hili swala la Richmond: Hivi baada ya taarifa ya Tume ya Bunge ya Dr Mwakyembe, Serikali litoa majibu. Mbona kwenye tuhum aza Bunge kuhusu Tegeta Escrow imekuwapo taarifa toka kwa Chief Secretary kuhusu suala hilo? Nani aliyejaribu kutoa maelezo ambayo yangemfungisha Lowassa au kumkomboa kwa kitendo chahe cha kujiuzuru kisiasa? Badala yake, wanazuoni wenzangu ambao sidhani kama tunazo facts za kutosha tuanaendelea kumshutumu Lowassa na kuwmona kama vile ni corrupt na kiongozi asiyefaa. It is not fair.

Mimi simlaumu Lowassa kujitoa CCM. Ni haki yake na kajieleza vipasavyo kuhusu maamuzi yake. Je, ni uamuzi wa uroho kuhusu U-Rais? Jamani, wanazuoni, hivi kweli tumefia hatua ya kumwona mtu ana uroho wa Urais? Ili awe au afanye nini ambacho sisi tufunge macho, na siyo tu kutoona, bali pia kuto chukua hatua? Ikifikia hapo, basi hatuna Taifa tena!!

Taifa letu limebahatika kufika hapa lilipofika mwaka huu. Wengi hatukutarajia kwamba yale ambayo tumekuwa tukitafakari na hata kusalia ghafla yameibuka. Sidhani na siamini kwamba ramani ya siasa ya Jamhuri yetu itabaki ilivyo ifikapo Desemba 2015. Ni ishara ya kheri na mwelekeo mwafaka kwa demokrasia ya Taifa letu.Naamini kwa dhati kabisa kwamba Edward Lowassa atakuwa kiongozi ambaye atasaidia ramani hii kuwa na muono mpya.

JV Mwapachu.

Culled From Wanazuoni
 
Wana zuoni lazima ifike wakati tuwe wawazi na wakweli, kwa hali hii ya sasa Lowasa ndo Rais
 
Atutolee unafiki wake hapa.Anaweweseka baada ya kuona fursa ya kupata cheo imekatwa.Hana jipya huyu.Tanga mjini imedorora na alishindwa hata kusapoti kuleta miradi ya maendeleo wakati nduguye alipokuwa mbunge.Alibweteka tu Ulaya.Hii yote ni kutapatapa baada ya kutoswa na JK
 
Mwapachu ni nani?

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"]Amb. Juma Mwapachu - Resume [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

CURRICULUM VITAE OF
AMBASSADOR JUMA VOLTER MWAPACHU
LLB; DIP. International Law; D.Lit; FCMI.


1. PERSONAL DETAILS
Date of Birth : 27 September, 1942
Place of Birth : Mwanza, Tanzania
Marital Status : Married
2. EDUCATIONAL HISTORY
1949 – 1958: Several Primary Schools in Mwanza, Mbeya and Dar-es-Salaam, Tanzania
1959 – 1962: Tabora Boys Secondary School, Tanzania
(O' Levels)
Became Queen's Scout in 1961

1963 – 1964: St. Michael's and St. George's School and Mkwawa High School, Iringa Tanzania.
(A' Levels). Groria Scholae for 1964

1965 – 1969: University of East Africa (at the University College, Dar-es-Salaam) Tanzania.
Obtained a Bachelor of Laws Degree in March 1969

1977 – 1978: Indian Academy of International Law and Diplomacy, New Delhi, India.
Obtained a Post Graduate Diploma in International Law, International Institutions and Diplomacy.

November 2005: Conferred with a Doctor of Literature Degree (Honoris Causa) by the University of Dar-es-Salaam, Tanzania.


3. PROFESSIONAL MEMBERSHIPS
: Fellow, Chartered Management Institute, UK since 1981
: Fellow, Academy of Political Science, USA
: Member, Society for International Development (SID) since 1983: sits on the International Council and is Member of its from 2000

4. CURRENT POSITION: Secretary General, East African Community from April 2006 to present

5. PREVIOUS POSITION: Tanzania Ambassador to France with accreditations to Spain, Portugal, Tunisia, Morocco and Algeria, from July 2002 – April 2006

6. PROFESSIONAL EXPERIENCE
April 1969 – Sept.1969
: First Tanzania Graduate to join the Tanzania Police Force (Asst. Supt. of Police) then reverted to Attorney General's Chambers, Government of Tanzania, (State Attorney)

: Subsequently seconded to the National Bank of Commerce as Assistant Legal Secretary
Oct. 1969 – August 1973
: National Bank of Commerce (Under State Ownership) Held the following positions:

- Assistant Legal Secretary in the Legal and Trustee Department
- Personnel manger heading the Personnel Division of the Bank
- Chief Manpower Manager responsible for all personnel functions (manpower planning, recruitment and salary administration) of the Bank

Sept. 1973 – April 1976
: District Development Director, Government of Tanzania.
(Under the Decentralization Programme introduced in July 1972)

May 1976 – July 1980
: Ministry of Foreign Affairs, Government of Tanzania: Principal Foreign Service Officer

Aug. 1976 – March 1977
: Minister Counsellor and Deputy Head of Mission, Tanzania Embassy, Addis Ababa, Ethiopia

April 1977 – March 1980
: Minister Counsellor, Deputy Head of Mission and Head of Chancery, Tanzania High Commission, New Delhi, India

April – July 1980
: Acting Director, Information, Research and Policy Planning Division in the Ministry of Foreign Affairs

Aug. 1980 – Dec 1982
: Coopers and Lybrand Associates Limited, Tanzania (now PriceWaterhouse Coopers)

1988 – 1996
: Director, Board of Directors of Juthalal Velji Ltd (holding Company of JV Group)

1997 – Present
: Chairman, RJH Investments and Management Services Ltd, (Investment and Management Consultant) Tanzania

1997 – Present
: Director and Shareholder, Rickshaw Travels Limited, Tanzania

1998 – 2002
: Director, Board of Directors of East African Breweries Limited, Kenya

1998 – Present
: Director, Board of Directors Heritage Insurance (Tanzania) Limited

2000 – Present
: Director and Shareholder, Maersk (Tanzania) Limited


7. POSITIONS HELD IN TANZANIA NATIONAL PRIVATE SECTOR INSTITUTIONS AND CIVIL SOCIETY

1980 – 1984: Member of the National Management Committee of Tanzania Red Cross Society

1984 – 1990: Elected the Founding Secretary General of the Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture (TCCIA)

1991 – July 2002: President, Tanzania Chapter of the Society for International Development (SID)

June 1991 – April 1996: Elected Member of the Founding Governing Council of the Confederation of Tanzania Industries (CTI)

8. MEMBERSHIPS IN TANZANIA PRESIDENTIAL COMMISSION OF ENQUIRY

1989 – 1991: Member, Presidential Commission of Enquiry into Public Revenues, Taxation and Expenditure (MTEI Commission)

1991 – 1992: Member, Presidential Commission of Enquiry on One Party or Multi-Party Political System for Tanzania (NYALALI Commission)

1993 – 1994: Member, Presidential Commission to Review the Structure and Expenditure of the Government (KOLIMBA and later MRAMBA Commission)

1996 – 1998: Member of Team of Experts responsible for crafting the Tanzania Development Vision 2025

9. BOARD POSITIONS HELD IN TANZANIA PRIVATE SECTOR COMPANIES

July 2002: As President of Society for International Development (SID) Tanzania Chapter played host to the 23[SUP]rd[/SUP] SID International Congress in Dar-es-Salaam, Tanzania

1988 – 2003: President of Convocation, University of Dar-es-Salaam. As President of the University of Dar-es-Salaam Convocation, have been responsible for spearheading the holding of several key National Symposia between 1991 and 2003 covering the following topics:

- The Crisis of Social Delivery in Tanzania
- The Role of Intellectuals in the Democratization Process
- The Multi-dimensional Crisis of Education in Tanzania
- The Crisis of Multi-party Democracy in Tanzania
- Why is Tanzania Still Poor 40 years after Independence?

1990 – 2002: Vice Chair, University of Dar-es-Salaam Governing Council


10. POSITIONS HELD IN PUBLIC SECTOR INSTITUTIONS

May 1973: Member of the National Committee established by the National Union of Tanzania Workers (NUTA) to recommend an Income and Wages Policy for Tanzania

1985 – 1988: Member, National Planning and Consultative Council established by the Government, representing the Private Sector

1984 – 2002: Member of the Board of Directors, Board of External Trade, Tanzania. Vice Chair of the Board from 1988 to 2002

1986 – 1993: Member, Board of Directors, Tanzania Investment Bank

1988 – 1992: Member, Boards of Directors, Tanzania Audit Corporation

1992 – August, 1995: Chair, Board of Directors, Tanzania Railways Corporation

1994 – July 2002: Chair, Board of Directors, Tanzania Investment Bank

1998 – July 2002: Member, Board of Directors, Tanzania Standard Newspapers Limited, the Government Media Institution that publishes the Daily and Sunday News

2000 – July 2002: Member, Board of Directors of the Business Registration and Licensing Agency (an Executive Agency of the Government)

Feb. 2000 – July 2002: Commissioner in the Presidential Parastatal Sector Reform Commission (institution charged with the responsibility of managing and supervising restructuring and privatization of State owned enterprises)

11. PUBLICATIONS
: Published and edited four books including recent book: 'Confronting New Realities: Reflections on Tanzania's Radical Transformation'.
 
Chadema ishauzwa, sasa ni team Edo. Dr. Slaa kafukuzwa kama mpangaji asiyelipa kodi!!!

Wavivu wa kufikiri kama wewe wakiwa vijana, utu uzima ukiwafika hugeuka wachawi! Kama ndugu yangu uko kwenye utu uzima, kaa chonjo, usinga'e Shinyanga! kuna watu wanawashambulia watuhumiwa!
 
Sijaelewa hizo sentensi. Zinakinzana.

 
hapo umetia chumvi lowassa hakupata kuwa waziri enzi za mwalimu
 

Siasa za kisasa hazitaki ulaghai
 
Yaani Mwapachu anadiriki kusema Nyerere ni muongo ili tu ahalalishe kitendo cha Lowassa kununua nafasi ya kugombea urais Chadema na kumtosa Slaa. Yaani Edo kutoswa CCM kaonewa ila Slaa kutoswa Chadema ni sawa.Kweli pesa mwanaharamu...
Kwani Nyerere hawezi kuwa Mwongo?
 
Bukanga

Hata Mungu alimpenda sana ibilisi kabla hajaasi.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…