Kauli ya awali ya Kamati Kuu kuhusu njama uchaguzi wa Meya jiji la Dar

Crashwise

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
22,227
8,735
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA UMMA

KAULI YA AWALI YA KAMATI KUU KUHUSU NJAMA UCHAGUZI WA MEYA JIJI LA DARE ES SALAAM NA VITISHO KWA WAWAKILISHI WA WANANCHI

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo imelaani vitendo vya njama za kisiasa zinazofanywa kupora haki ya wananchi katika uchaguzi wa Meya Jiji la Dar es Salaam na kuwa ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea nchini huku ukionekana kuwa na ‘baraka’ za viongozi wakubwa wa nchi, hautavumilika.

Akitoa kauli hiyo ya awali mbele ya waandishi wa habari leo wakati Kamati Kuu ikianza kikao chake jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe amesema kuwa CHADEMA haitakubali kuona Serikali ya awamu ya tano ikitawala kwa kutegemea udhalimu wa kutumia vyombo vya dola huku ikivunja sheria na taratibu nchi.

Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa ni ajabu kuwa watawala wa awamu ya tano ambao wanataka kujinasibu kuwa wanakubalika, wanalazimika kuendesha nchi kwa kuvunja misingi ya demokrasia na kutumia njia za kunyanyasa wapinzani kwa nia ya kuwanyamazisha badala ya kuwa tayari kukosolewa kwa mstakabali sahihi wa maslahi na matakwa ya nchi kwa ujumla.

Amesema kuwa hali hiyo ya sheria kuvunjwa kwa ajili ya kuwashughulikia wapinzani ikiendelea bila kukomeshwa ikiwemo kuwapora wananchi haki yao ya wazi kama inavyotaka kufanyika kwenye umeya wa Dar es Salaam, watawala watachochea moto ambao watashindwa kuuzima.

“Tumelazimika kuzungumza nanyi waandishi wa habari kutoa kauli hii ya awali wakati tunaelekea kuanza kikao cha Kamati Kuu kwa sababu ya matukio ya hila, njama na mipango ovu ya kisiasa inayopangwa na Serikali ya CCM ili kujihalalishia mambo kinyume na sheria za nchi.

“Ipo mikakati ya siri ambayo imeanza kutekelezwa kwa vitendo vya kuwakamata na kuwashushia hadhi na kuwadhalilisha wawakilishi wa wananchi wakiwemo wabunge na madiwani ambao kama inavyoendelea kufanyika Jiji la Dar es Salaam,” amesema Mwenyekiti Mbowe.

Ameongeza kusema kuwa njama zinazoendelea za kuwakamata, kuwaweka chini ya ulinzi na kuwanyima dhamana wabunge na madiwani wa CHADEMA katika Jiji la Dar es Salaam ni sehemu ya mkakati mkubwa wa Serikali ya CCM kutaka kupora uchaguzi wa meya na kulinda ufisadi mkubwa katika jiji hilo.

“Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam unasuasua kwa miezi minne na siku tano hadi leo. Wananchi walifanya maamuzi ya kuchagua madiwani wengi wa UKAWA wakaikataa CCM. Chama chochote makini kilipaswa kuheshimu maamuzi hayo ya wananchi.

“Temeke ambako CCM wana madiwani wengi hakukuwa na tatizo katika kumpata meya ambaye anatokana na CCM. Lakini katika maeneo yote ambako CHADEMA au Ukawa tumeshinda wenzetu hawa wamekataa kukubali, kila mahali imekuwa ni shida kweli kweli…”

“Huko Kyerwa ambako tulikuwa na madiwani wengi, madiwani wetu walikamatwa siku ya kupiga kura na kubambikiwa kesi, huko Kilombero hata leo tu mbunge wa jimbo amekamatwa na kudhalilishwa asiingie ukumbi wa kupiga kura.

“Tunapozungumza hapa Mbunge Mdee anashikiliwa na polisi, wanamshikilia Mbunge Waitara, wanamtafuta Kubenea, wanawashikilia madiwani wetu na wanachama bila sababu zote za msingi, lakini lengo ni kuhujumu uchaguzi wa meya,” amesema Mwenyekiti na kuongeza;

“Wakati watu wetu wanakamatwa, yule RAS aliyesoma zuio la mahakama la kughushi na kuharibu uchaguzi na kusababisha vurugu yuko huru. Haya yote yanafanyika Rais Magufuli ambaye ndiye Waziri wa TAMISEMI anajua, Waziri Mkuu anajua, Sefue anajua, CCM wanasheherekea na wote hawa ni sehemu ya uchakachuaji huu unaofanyika.

Mwenyekiti pia amezungumzia wito wa barua walizoandikiwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA, wakiwemo Godbless Lema, Pauline Gekul na Ester Bulaya kufika mbele ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kwa madai ya kumvunjia heshima Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge siku ya mjadala wa Serikali kuzuia matangazo ya moja kwa moja vikao vya bunge kupitia TBC.

Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa taarifa hiyo ya awali itafuatiwa na tamko la Kamati Kuu ambayo inakutana jijini Dar es Salaam kujadili na kuamua juu ya masuala mbalimbali ikiwemo kuhusu hali ya kisiasa nchini.

Imetolewa leo Jumanne, Machi 1, 2016 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
 
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)


TAARIFA KWA UMMA


KAULI YA AWALI YA KAMATI KUU KUHUSU NJAMA UCHAGUZI WA MEYA JIJI LA DARE ES SALAAM NA VITISHO KWA WAWAKILISHI WA WANANCHI


Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo imelaani vitendo vya njama za kisiasa zinazofanywa kupora haki ya wananchi katika uchaguzi wa Meya Jiji la Dar es Salaam na kuwa ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea nchini huku ukionekana kuwa na ‘baraka’ za viongozi wakubwa wa nchi, hautavumilika.

Akitoa kauli hiyo ya awali mbele ya waandishi wa habari leo wakati Kamati Kuu ikianza kikao chake jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe amesema kuwa CHADEMA haitakubali kuona Serikali ya awamu ya tano ikitawala kwa kutegemea udhalimu wa kutumia vyombo vya dola huku ikivunja sheria na taratibu nchi.

Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa ni ajabu kuwa watawala wa awamu ya tano ambao wanataka kujinasibu kuwa wanakubalika, wanalazimika kuendesha nchi kwa kuvunja misingi ya demokrasia na kutumia njia za kunyanyasa wapinzani kwa nia ya kuwanyamazisha badala ya kuwa tayari kukosolewa kwa mstakabali sahihi wa maslahi na matakwa ya nchi kwa ujumla.

Amesema kuwa hali hiyo ya sheria kuvunjwa kwa ajili ya kuwashughulikia wapinzani ikiendelea bila kukomeshwa ikiwemo kuwapora wananchi haki yao ya wazi kama inavyotaka kufanyika kwenye umeya wa Dar es Salaam, watawala watachochea moto ambao watashindwa kuuzima.

“Tumelazimika kuzungumza nanyi waandishi wa habari kutoa kauli hii ya awali wakati tunaelekea kuanza kikao cha Kamati Kuu kwa sababu ya matukio ya hila, njama na mipango ovu ya kisiasa inayopangwa na Serikali ya CCM ili kujihalalishia mambo kinyume na sheria za nchi.

“Ipo mikakati ya siri ambayo imeanza kutekelezwa kwa vitendo vya kuwakamata na kuwashushia hadhi na kuwadhalilisha wawakilishi wa wananchi wakiwemo wabunge na madiwani ambao kama inavyoendelea kufanyika Jiji la Dar es Salaam,” amesema Mwenyekiti Mbowe.

Ameongeza kusema kuwa njama zinazoendelea za kuwakamata, kuwaweka chini ya ulinzi na kuwanyima dhamana wabunge na madiwani wa CHADEMA katika Jiji la Dar es Salaam ni sehemu ya mkakati mkubwa wa Serikali ya CCM kutaka kupora uchaguzi wa meya na kulinda ufisadi mkubwa katika jiji hilo.

“Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam unasuasua kwa miezi minne na siku tano hadi leo. Wananchi walifanya maamuzi ya kuchagua madiwani wengi wa UKAWA wakaikataa CCM. Chama chochote makini kilipaswa kuheshimu maamuzi hayo ya wananchi.

“Temeke ambako CCM wana madiwani wengi hakukuwa na tatizo katika kumpata meya ambaye anatokana na CCM. Lakini katika maeneo yote ambako CHADEMA au Ukawa tumeshinda wenzetu hawa wamekataa kukubali, kila mahali imekuwa ni shida kweli kweli…”

“Huko Kyerwa ambako tulikuwa na madiwani wengi, madiwani wetu walikamatwa siku ya kupiga kura na kubambikiwa kesi, huko Kilombero hata leo tu mbunge wa jimbo amekamatwa na kudhalilishwa asiingie ukumbi wa kupiga kura.

“Tunapozungumza hapa Mbunge Mdee anashikiliwa na polisi, wanamshikilia Mbunge Waitara, wanamtafuta Kubenea, wanawashikilia madiwani wetu na wanachama bila sababu zote za msingi, lakini lengo ni kuhujumu uchaguzi wa meya,” amesema Mwenyekiti na kuongeza;

“Wakati watu wetu wanakamatwa, yule RAS aliyesoma zuio la mahakama la kughushi na kuharibu uchaguzi na kusababisha vurugu yuko huru. Haya yote yanafanyika Rais Magufuli ambaye ndiye Waziri wa TAMISEMI anajua, Waziri Mkuu anajua, Sefue anajua, CCM wanasheherekea na wote hawa ni sehemu ya uchakachuaji huu unaofanyika.

Mwenyekiti pia amezungumzia wito wa barua walizoandikiwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA, wakiwemo Godbless Lema, Pauline Gekul na Ester Bulaya kufika mbele ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kwa madai ya kumvunjia heshima Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge siku ya mjadala wa Serikali kuzuia matangazo ya moja kwa moja vikao vya bunge kupitia TBC.

Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa taarifa hiyo ya awali itafuatiwa na tamko la Kamati Kuu ambayo inakutana jijini Dar es Salaam kujadili na kuamua juu ya masuala mbalimbali ikiwemo kuhusu hali ya kisiasa nchini.


Imetolewa leo Jumanne, Machi 1, 2016 na;


Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Ni vyema wangewafungulia mashitaka polis wote walioshiriki kwenye unyanyasaji huo pia Yule mkurugenzi aliyetangaza Zuio feki na yeye afunguliwe kesi Mahakama kuu angalau itasaidia kuifahamusha Dunia na Taasisi za haki za binadamu kuwa Tanzania ya sasa umeingia kwenye Udikteta .
 
Mnapolalamika kwamba ni njama, ina maana CCM ndio waliwaambia mfanye vurugu? Kwani mngekaa bila kufanya vurugu ni polisi yupi angethubutu kuwakamata na kuwaweka ndani?
 
Siyo utawala wa kidikteta Bali wa kijeshi.Maana nguvu ya jeshi inayotumika ni kubwa mno.
 
Wapeleke kesi The Hague haraka ndipo haki itapatikana lakini kinyume na hapo wataendelea kulaani tu huku watu wanateseka pasipo kupata haki , Laana haiwezi kuzuia Mawazo ya Nape January na wenzao juu ya Ukawa , kuwalaani kamwe hakutamaliza Tatizo lazima vyama vya haki za binadamu viwafungulie kesi wote waliosababisha Tatizo , maana sasa wamekamatwa waliolalamikia Uonevu lakini Yule aliyesababisha Tatizo yupo nyumbani kwake anafurahia mateso ya wengine hakika mungu anambeep mda si mrefu.
 
Mnapolalamika kwamba ni njama, ina maana CCM ndio waliwaambia mfanye vurugu? Kwani mngekaa bila kufanya vurugu ni polisi yupi angethubutu kuwakamata na kuwaweka ndani?
Kama wamekosa kwanini wasifunguliwe mashtaka mahakamani??Mbona hilo kosa kina dhamana??Kuna sababu gani ya kuwanyima dhamana??
 
Duuuh, najaribu kupanga vizur maneno kichwani ili niandke kitu lakn nashndwa jaman, sijui hata niandke nin juu ya hawa mabedui wa magu.
 
Siyo utawala wa kidikteta Bali wa kijeshi.Maana nguvu ya jeshi inayotumika ni kubwa mno.
Kuwanyima watu dhamana Kwa visingizio vya ajabu ni kinyume cha haki za binadamu pia ni kinyume cha Sheria za Tanzania ambazo sasa zinapindishwa makusudi ili kuwakomoa.
 
Published on 1 Mar 2016
Jeshi la polisi limevamia nyumbani kwa mbunge wa jimbo la Kawe Mh. Halima Mdee kwa lengo la kufanya upekuzi wakitafuta faili ambalo lilikuwa na nyaraka muhimu za kikao cha kumchagua meya wa jiji la Dar es Salaam uchaguzi ambao haukuweza kufanyika kutokana na kuwepo kwa taarifa kuwa kuna pingamizi limewekwa mahakamani.

Pia video inaonesha Mh. Freeman Mbowe, Mh. Halima Mdee na wenzake wasimulia hali halisi


Source: ITV TANZANIA youtube
 
Kwa Hali ya sasa ya siasa Za nchi yetu ilivyo Kwa sasa Ina takiwa kipindi hiki Cha mpito mheshimiwa mbowe amkabidhi uwenyekiti wa Chama mheshimiwa Godbless Lema na Katibu mkuu awe Joseph mbilinyi hiyo ndio dawa
 
Mkuu hebu ficha upuuzi wako, usije kutuharibia Mood usiku huu! Ina maana hujui hizo "fujo" zilitokana na nini au unaleta usela mavi tu? Mpuuzi wewe!
Waleta Fujo ni ccm wenyewe na walileta fujo makusudi wakiwa na Lengo la kuwabambikia kesi Ukawa pindi wakipanga udhalimu wao, sasa wamefarijika Kwa kuwabambikia kesi huku Yule aliyetangaza Zuio Feki yupo nyumbani anajiachia Kwa raha zake , fujo za ccm sasa zimegeuzwa kuwa za Ukawa na kutumia fursa hiyo kuwakandamiza Yaani Udikteta ndiyo unaanza sasa mpaka kufika mwakani hali itakuwa mbaya magereza yote yatajaa wapinzani huenda Serikali hii ikarejesha lile gereza la kizuizini lililotumika Kipindi cha awamu ya kwanza.
 
hayo maneno usingeweza kuyaongea muda huu ungekuwa somalia acha kufikiri vitu ambavyo wengine wanaomba kwa mungu wayaepuke.......unaongea pumba zako kwa kuwa unaamani usingekuwa nayo sidhani hata huo muda wakuniita kiroboto na kuongea ujinga wako ungekuwa nao
Acha Ujinga wewe, AMANI ni tunda la HAKI, waambie MACCM wenzio, bila HAKI, hiyo AMANI yenu haitadumu kamwe! Tendeni HAKI..AMANI itaendelea kuwepo! Halafu usiogope ya SOMALIA, wale pia ni binadamu na Amani ilitoweka huko kwa sababu ya majitu majinga majinga kama MACCM.
 
Back
Top Bottom