Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 22,178
- 41,706
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu.
Inawezekana itaonekana kuwa ni kitu cha ajabu kwa baadhi ya watu wanaoamini kwenye kufanya mambo kimazoea, lakini ukweli ni kwamba Kamati Kuu ya CHADEMA imepoteza kabisa uhalali wa kuchuja wagombea kwenye uchaguzi unaotarajiwa kuanza kufanyika kuanzia tarehe 13/01/2025.
Kamati kuu hii ambayo imegawanyika na yenye wajumbe wanaopita kwa wajumbe wa mikutano ya uchaguzi, kuwaombea wagombea wanaowaunga mkono kura, inawezaje kufanya maamuzi bila ya kutanguliza mbele maslahi ya wagombea wao?
Kisheria siyo tu haki hutakiwa itendeke, bali pia inatakiwa ionekane imetendeka. Hawa wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wanapungukiwa sifa hiyo ya kuaminika kwamba watatenda haki badala ya kutanguliza maslahi ya wagombea wanaowaunga mkono.
Kwa ushauri wangu Kamati Kuu iangalie mambo tu ya msingi kwa wagombea, na majina ya wagombea WOTE yapelekwe kwenye vikao vya uchaguzi vikachague wagombea kwa jinsi itakavyokuwa.