walianza na HALI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA..................Ikachuja mda mfupi baada ya kikwete kuwa rais. MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA..................Ikachuja mda mfupi baada ya kikwete kuwa rais. tena vijana wakikisikia unaisema wanaweza kukupiga mawe. ikaja SERIKALI YETU NI SIKIVU...........ikachuja baada ya kikao cha bunge la bajeti, wahubiri wakuu wabunge wa ccm, spika wa bunge na mawaziri. TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE. ikachuja baada ya maadhimisho ya uhuru. hii haoikupata mafanikio sana maana waliokuwa wakijitahidi kuihubiri ni wale waliokuwa wakifaidika nayo kama mawaziri, wabunge wa ccm,wakubwa wa mashirika ya umma na wale walijipeleka siku ya maadhimisho ya uhuru kuona ndege zinavyoruka angani, huku wenzetu wakituma vyombo angani ss bado tunaenda kushuhudia ndege za kivita zikiruk kwenye nchi yenye amani ya kijinga. wamekuja na kauli mbiu nyingine, KUKATAA KOO ZA WATU(Steve Nyerere), kufatilia mahusiano ya watu (Dr na Josephine), kupakazia watu, kutengeneza nyaraka mbalimbali za uongo na kuhubiri matusi. ................hizi zimetokea arumeru. Ongezea na wewe............................. na unahisi watakuja na ipi sa hv.