sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
Kanisa katoliki nchini,limesema kamwe halitarudi nyuma kutumia rasilimali zake katika kuwekeza kwenye elimu kwa kujenga shule nyingi za sekondari ili kulisaidia taifa kuwa na vijana wengi wasomi.
Kauli hiyo ilimetolewa juzi jijini mwanza na rais wa baraza la maaskofu nchini(TEC)Jude Thadaeus Ruwaichi wakati alipo kuwa akizungumza kwenye mahafali ya 50 ya shule ya msingi Nyakahoja ya jijini mwanza. Kwa mujibu wa askofu Ruwaichi kanisa hilo lipo mstari wa mbele kupigania maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla,hivyo litaendelea kuwekeza kwa kujenga sekondari za wavulana na wasichana nchini.
Kanisa litatumia rasilimali zake kuwekeza sana kwenye sekta ya elimu kwa kujenga shule nyingi za sekondari,miaka 20 iliyopita tumejenga sana sekondari kwa wasichana.Kazi hii tutaendelea nayo kwa lengo moja tu la kusaidia nchi na vijana wetu katika kuwa na wasomi wenye elimu bora.
Ruwaichi ambaye pia ni askofu wa jimbo kuu la Mwanza ,alisema mwaka huu kanisa hilo litaanza kujenga shule ya sekondari ya wavulana jijini Mwanza.Hata hivyo Ruwaichi aliagiza mchakato wa ujenzi huo ufanyike haraka ikiwa ni pamoja na kuandaa mchoro wa shule hiyo.
Kauli hiyo ilimetolewa juzi jijini mwanza na rais wa baraza la maaskofu nchini(TEC)Jude Thadaeus Ruwaichi wakati alipo kuwa akizungumza kwenye mahafali ya 50 ya shule ya msingi Nyakahoja ya jijini mwanza. Kwa mujibu wa askofu Ruwaichi kanisa hilo lipo mstari wa mbele kupigania maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla,hivyo litaendelea kuwekeza kwa kujenga sekondari za wavulana na wasichana nchini.
Kanisa litatumia rasilimali zake kuwekeza sana kwenye sekta ya elimu kwa kujenga shule nyingi za sekondari,miaka 20 iliyopita tumejenga sana sekondari kwa wasichana.Kazi hii tutaendelea nayo kwa lengo moja tu la kusaidia nchi na vijana wetu katika kuwa na wasomi wenye elimu bora.
Ruwaichi ambaye pia ni askofu wa jimbo kuu la Mwanza ,alisema mwaka huu kanisa hilo litaanza kujenga shule ya sekondari ya wavulana jijini Mwanza.Hata hivyo Ruwaichi aliagiza mchakato wa ujenzi huo ufanyike haraka ikiwa ni pamoja na kuandaa mchoro wa shule hiyo.