GE2025 Katibu wa Watanzania waishio China: Wanaohamasisha vurugu nchini wana sababu binafsi

GE2025 Katibu wa Watanzania waishio China: Wanaohamasisha vurugu nchini wana sababu binafsi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini China Alawi Abdallah amesema Watanzania wote walioko nje ya nchi ambao wamekuwa wakilalamikia mifumo ya uchaguzi na demokrasia nchini Tanzania wamekuwa hawana dhamira ya dhati ya kutaka mabadiliko bali wamekuwa wakiongoza na maslahi binafsi na chuki binafsi kwa baadhi ya Viongozi na Vyama vya siasa vilivyoko nchini Tanzania.

Alawi ametoa kauli hiyo wakati wa Mdahalo wa pamoja ulioandaliwa jijini Dar es Salaam na kuhusisha Wanafunzi wa Vyuo na Vyuo Vikuu nchini, akitolea mfano kwa baadhi ya Watanzania wanaoishi kwenye nchi zenye mfumo wa Malkia na Mfalme na bado wamekuwa wakilalamikia mfumo wa uchaguzi nchini na vile ambavyo chaguzi zimekuwa zikifanyika


 
Back
Top Bottom