Katibu wa CHADEMA Iringa, Jackson Mnyawami akamatwa na Polisi kwa tuhuma ya kutoa lugha ya kuudhi dhidi ya DC Kilolo

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,330
33,954

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah!

Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Iringa Jackson Mnyawami, amekamatwa na Polisi jioni hii na kupelekwa Kituo cha Polisi Mazombe Wilayani Kilolo kwa kutuhuma ya kutoa lugha ya kuudhi mtandaoni dhidi ya Mkuu wa wilaya ya Kilolo.

Inadaiwa kwamba Mnyawami aliweka kwenye kundi la wana Kilolo video yenye nukuu ya majaji wakizungumzia uvunjwaji wa sheria unaofanywa na baadhi ya Wakuu wa Wilaya nchini na kuandika maneno yenye kuonesha kwamba ujumbe huo unamhusu pia Mkuu huyo wa Wilaya.

MUENDELEZO
-------------------
Bw. Mnyawami ameachiwa na Polisi muda mfupi uliopita kwa kujidhamini yeye Mwenyewe!!
 
Kipindi nikiwa kijana nilikuwa nasumbuliwa sana na wanawake ila nilipokuja kuwajua wanawake wanataka nini wala hawanisumbui tena.
 
Demokrasia ni gharama, ninaamini ipo siku yatakwisha, hakuna marefu yasiyo na mwisho, makamanda tuvumilie yote safari yenye mafanikio si nyepesi
 
Ukitaka uyaepuke haya yanayotendeka kwa wakosoaji wa serikali hii na viongozi wake ujitie upuuzi tu wa kushangilia kila jambo toka kwao
 
matayarisho ya 2020 haya - mpaka ikifika upinzani wamesambaratika na wako hoi
 
Hakuna aliye juu ya sheria. Hivi upuuzi anaoongea jiwe mara kwa mara na watu wanapiga makofi. Ukiongea mtu wa kawaida inakuwaje?au sheria ina matabaka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…