Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,236
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah!
Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Iringa Jackson Mnyawami, amekamatwa na Polisi jioni hii na kupelekwa Kituo cha Polisi Mazombe Wilayani Kilolo kwa kutuhuma ya kutoa lugha ya kuudhi mtandaoni dhidi ya Mkuu wa wilaya ya Kilolo.
Inadaiwa kwamba Mnyawami aliweka kwenye kundi la wana Kilolo video yenye nukuu ya majaji wakizungumzia uvunjwaji wa sheria unaofanywa na baadhi ya Wakuu wa Wilaya nchini na kuandika maneno yenye kuonesha kwamba ujumbe huo unamhusu pia Mkuu huyo wa Wilaya.
MUENDELEZO
-------------------
Bw. Mnyawami ameachiwa na Polisi muda mfupi uliopita kwa kujidhamini yeye Mwenyewe!!