Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Baraka Leonard, amethibitisha kuwa kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, marehemu Jenista Mhagama, kimesababishwa na maradhi ya Moyo.
Akizungumza wakati wa Ibada ya Misa ya Kuuaga Mwili wa marehemu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja cha Ndege, Jijini Dodoma, Leonard amesema marehemu alifariki dunia baada ya kusumbuliwa na maradhi hayo.
Leonard ametoa kauli hiyo wakati akisoma wasifu wa marehemu mbele ya waombolezaji, viongozi wa Serikali, wabunge, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria ibada hiyo ya kumuaga kiongozi huyo.
Aidha, amesema marehemu Jenista Mhagama ameacha watoto watano pamoja na familia ambayo imepata pigo kubwa kutokana na kifo chake cha ghafla.
Akizungumza wakati wa Ibada ya Misa ya Kuuaga Mwili wa marehemu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja cha Ndege, Jijini Dodoma, Leonard amesema marehemu alifariki dunia baada ya kusumbuliwa na maradhi hayo.
Leonard ametoa kauli hiyo wakati akisoma wasifu wa marehemu mbele ya waombolezaji, viongozi wa Serikali, wabunge, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria ibada hiyo ya kumuaga kiongozi huyo.
Aidha, amesema marehemu Jenista Mhagama ameacha watoto watano pamoja na familia ambayo imepata pigo kubwa kutokana na kifo chake cha ghafla.