Taaluma Makini
Senior Member
- Mar 3, 2013
- 111
- 12
katibu mkuu wa chama cha mapinduzi Mzee Kinana kwenye ziara yake ya hivi karibuni mkoani DSM alipokutana na wanachama wa CCM na kupitia vyombo vya habari amekuwa anatoa kauli za kushangaza kama sio kustajaabisha kwa mtu anaye fuatilia siasa za Tanzania.
Kwa mara kadhaa kwenye mikutano yake amekuwa kama anaisuta serikali ya CCM na kimantiki ni kama amekuwa ana msuta raisi Jakaya Kikwete pamoja na serikali yenye mawaziri wote wanao tokana na CCM. Amekuwa anaelezea matatizo ya ajira kana kwamba yeye ni katibu wa chama cha upinzani, anaisuta na kuihoji serikali kwa kushindwa kutengeneza ajira, anaihoji na kuisuta serikali kwa kuweka kodi ambazo ni kikwazo naza manyanyaso kwa wananchi.
Amelalamikia tatizo la miundombinu mibovu ya maji na uhaba wa upatikani wa maji kwenye jiji la DSM kana kwamba hakumbuki kuwa serikali hiihii ya CCM ilileta mradi wa mabomba ya wachina na mpaka sasa ni usanii kama ilivyo usanii mwingine wa CCM na bado wananchi wengi wa DSM wanateseka kwa kero ya maji huku wapiga dili wakiwa wameshapiga dili na mradi umesimama bila uhakika wa maji.
Nimebaki na jiuliza, huyu katibu mkuu wa CCM ambaye serikali iliyo chini ya chama chake chini ya mwenyekiti wake wa chama ambayo kimsingi ndio chanzo cha anayo eleza na kuimba kwenye majukwaa ameamua kuasi na kuanika udhaifu wa serikali ya mwenyekiti wake wa chama?! Au anataka aje amtupie zigo JK kwa kusema kuwa CCM ilisema lakini mwenyekiti aliyekuwa anaongoza serikali ndio alikuwa kikwazo?! Nia yake ni nini haswa?!
Ni mpinzani ndani ya CCM?!
Huyo ndio Kinana! Ndumila kuwili!