Ndugu zangu,
Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?
Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?
Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?
Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.
Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.
Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.
Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.
Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.
Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.
Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?
Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?
Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?
Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.
Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.
Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.
Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.
Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.
Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.