Katiba Na Ukungu Kwenye Kioo

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?

Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?

Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?

Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.

Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.

Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.

Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.

Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.

Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.
 
Yaani inzi kutoka chooni katua kwenye msosi halafu wewe unapendekeza tule tu kwa maana tuna njaa sana!
 
Kilichobakia sasa ni kupiga kura tu, hakuna majadiliano. Na hili ndilo tatizo. Kutakuwepo na kuelimishana lakini angalizo ni elimu kutoka makundi mawili pinzani- moja Rasimu ya Katiba na lingine Katibu Iliyopendekezwa.

Ni nafasi iliyopotea!
 
Unachekesha kweli wewe, haya pita Lumumba ukachukue bahasha yako ili uendeleze uchumia tumbo wako.



Ndugu zangu,
Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?
Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?
Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?
Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.
Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.
Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.
Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.
Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.
Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.
 
Kwahio hata kama kioo kina matatizo na hakionyeshi picha halisi tuendelee kujidanganya kujiangalia sababu kimetumia gharama na waliotengeneza baadhi walikuwa na dhamira nzuri ?

Ungejua kwamba Katiba ni maridhiano wala si mashindano..., na inabidi ipate baraka bila chembechembe ya hata wachache kuona kwamba wameonewa usingesema hayo uyasemayo.

Hao unaowapa heko walikosea sana kwenye sensitive issue zingepigiwa kura tangia mwanzo (mfano muundo wa serikali na muungano) ili kuanzia mwanzo ijulikane inaandikwa Katiba ya aina gani.., pili hawa watawala / wabunge wasingepewa automatic ticket ya kuingia Bunge Maalumu sababu huwezi kutegemea watakubali Katiba inayowabana. (Refer kilichofanyika sasa, hakuna kikomo cha wabunge na wakuu wa wilaya, mkoa as well as number ya wapokea posho kuongezeka badala ya kupungua)
 
Huyu jamaa ni kilaza siku zote, ila nilimdharahu zaidi alipo husika na lile tukio la kuteka mwahariri wa gazeti la Mtanzania.
 
Chamsingi hapa ni kuikubali hii kwani kodi zetu zilizotumika kuindaa katiba si ndogo.
 
maggid ile ni katiba ya ccm, sio yetu.
nimeona umeandika kutokea Nairobi hebu waulize hao hapo kama walifanya kituko kama hiki kilichofanyika hapa. imagine katiba ambayo haitaki hata kuhoji uadilifu wa viongozi. jitathimini Maggid.

Ndugu zangu,

Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?

Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?

Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?

Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.

Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.

Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.

Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.

Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.

Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.
 
Ndugu zangu,

Leo Watanzania tutashuhudia Rais wa Jamhuri akikikabidhiwa Katiba Pendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Kitakachofuatia ni Katiba Pendekezwa kupigiwa kura na Wananchi. Na Katiba ya Nchi ni sawa na Kioo cha Nchi. Tunajitazama kupitia katiba. Na tunafanyaje kama kioo kimeingia ukungu?

Mwingine atasema tukivunje, tutafute kipya. Lakini, kwa vile ukungu kwenye jamii utaendelea kuwepo daima na hatuwezi kuuzuia , je,tutavunja vioo vingapi?

Naam, mchakato wa katiba umefikia ulipofikia, na bado haujakamilika. Ukungu ungalipo, na mwingine unakuja. Na lipi lililo jema, kuvunja kioo au kufuta ukungu?

Tukitanguliza hekima na busara, tukitanguliza mapenzi kwa nchi tuliyozaliwa. Hivyo, uzalendo kwa nchi yetu. Basi, tutauona mchakato wa Katiba kama 'Mchakato Wa Kujifunza'. Tumejifunza mengi na tunaendelea kujifunza kama taifa. Tumeuona udhaifu wetu ambao huko nyuma hatukuuona. Tumeziona nguvu zetu pia. Tumeanza kujitambua zaidi.

Kuna wanaohangaika kumtafuta mshindi na mshindwa kwenye mchakato huu. Hao ni majuha, maana waliuangalia mchakato huu kwa rangi za vyama vyao na makundi yao.

Maana, hapa tulipofikia, pamoja na ukungu uliopo, bado Watanzania wote ni washindi. Wote walioshiriki kufanikisha kutufikisha hapa wamefanya kazi njema. Na tuamini, kuwa wengi wao walikuwa na nia njema, akiwamo Rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato huu.

Na hapa naungana na alichosema Waziri Mkuu Mizengo Pinda pale Bungeni, kuwa ingekuwa vema pia, kama Katiba hii pendekezwa ingepigiwa kura na wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, maana, nami naamini, wananchi tusingependa kusubiri sana kutoa kauli yetu kuhusiana na katiba, kwa kupitia sanduku la kura.

Naam, tulipofikia kama Taifa, hatuna namna yeyote ya kufanya, bali Kusonga Mbele, kwa kuendelea kujadiliana, na si kuandamana.

Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.
Maggid kuna wakati nilikupigia simu na kuongea nawe kwa kirefu.Nakumbuka ulisema wewe ni mwandishi wa habari na si REPORTER!!!
Nasoma sana makala zako na kwa ujumla ni mpenzi wa uandishi wako ila kwenye siasa kuna wakati unaogopa kuonyesha msimamo na hata kukosoa hasa inapoguswa serikali na CCM.
Umekaa Ulaya sana na leo unasema tujadiliane na si MAANDAMANO!!! Maggid kuwa mkweli kwa CCM hii na uongozi huu majadiliano yana nafasi gani?
Ushindi kwa gharama yoyote ndiyo jambo muhimu kwani kama ingekuwa majadiliano Rais angeacha majadiliano yachukue nafasi lakini akaingiza msimamo wake na wa Chama chake,umeona yaliyotokea mpaka kina Komba wanamtukana Warioba.
Dhamira itakusuta sana kwa kuujua ukweli lakini ukaamua kuuficha,tuhurumie wasomaji wa makala zako!!!
 
Kama wachambuzi wetu tena wenye kuonekana kwenye gazeti tutegemee nini?
 
Maishani uikiruhusu kutumika kama Toilet paper ugopa sana safari yako mbele si ndefu sana.Na mwisho unakuwa kama hivi.
Kitu kimoja kiafya kiko wazi kuwa afya ya akili ni muhimu na maana yake akili itumike kwa vilivyo halisia kimaisha na si uhalifu.
Kuna uhalifu wa aina mbalimbali -kutumia mwili na kutumia akili.



jpg.gif
1412772602623.jpg

 
Back
Top Bottom