Katiba Mpya ni kwa maslahi ya wanasiasa kujiwekea mazingira ya kutawala na si kusaidia wananchi

Kevomu

Member
Apr 24, 2017
33
32
Mjadala wa katiba mpya unapiganiwa na wanaharakati wa kisiasa wakishinikiza wananchi kuwaunga mkono, lengo lake kuu si kuwasaidia wananchi (wamachinga,mama ntilie, wafanyakazi) bali ni kuawasaidia wanasiasa hao kushika hatamu za uongozi kwa maslahi yao na familia zao, na pia kuongeza nafasi za uongozi, kuvunja muungano, kuifanya Tanzania kuwa nchi ambayo si salama kuishi, nchi ya maandamano.

Kuna vipengele vichache katika rasimu ya katiba ambavyo vinatolewa macho na wanasiasa kwa kushirikiana baadhi ya wafadhili wao wasioitakia mema nchi yetu ambapo wanaamini vikibadilishwa Tanzania itakuwa si nchi salama kuishi, nchi ya maandamano yanayopelekea watu wengi kuuliwa hovyo kama Kenya, nchi ya kuapishwa marais wawili kama Kenya, nchi isiyo na utulivu kwa wananchi wake kama, Iraq,Libya, Somalia, Syria, Palestina,Kongo, Nigeria, Sudan, Ethiopia na nyingine nyingi.

Wanaamini vipengele hivyo vikibadilishwa watavitumia kwa kuwashawishi wananchi kufanya fujo na maandamano ili wao walazimishe kupata uongozi baada ya watu kufa (si wao wala familia zao bali wamachinga, bodaboda, mama ntilie) huku wafadhili wao wakiamini fujo hizo zitawasaidia wao kuiba rasili mali zetu kama gesi , madini, wanyama pia watanufaika endapo kupitia viongozi hao wa kisiasa wanao watumia kuvuruga Amani ya nchi kwa kivuli cha demokrasia.

VIPENGELE PEKEE VYA RASIMU YA KATIBA WANAVYOPIGANIWA NA SABABU YA UHITAJI WA KILA KIPENGELE
  1. KIPENGELE CHA 73(4) KIMEBAINISHA NA KUSEMA,

    “Katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ibara hii,
    Rais ataepuka kujinasibisha, kwa namna yoyote ile, na chama chochote cha siasa au kundi lolote kwa namna ambayo inaathiri umoja wa wananchi.”

    Hichi ni kipengele mojawapo kinachopiganiwa na wasioitakia mema Tanzania.

    Kipengele hichi kinamsaidiaje mwanannchi wa kawaida? (hakina msaada wowote)
  • Wananchi hapo wametumika kama kinga na kukipa nguvu kipengele hiki, ila lengo kuu la kipengele hiki ni kumnyima mamlaka rais juu ya udhibiti wa vyama vya siasa vitakayoamua kuyafanya kuvuruga Amani ya nchi, kupitia kipengele hichi kutakuwa na maandamano kila siku na kazi hazitofanyika.
2. KIPENGELE CHA MUUNDO WA SERIKALI

Katika kipengele hichi muundo wa serikali, wanasiasa hawa wanalazimisha uwepo wa serikali tatu (3) badala ya mbili zilizopo sasa.

Serikali tatu(3) zina msaada gani kwa mmachinga na mwananchi mwingine? (hakina msaada wowote)

  • Lengo kuu la kudai serikali tatu ni kudhoofisha muungano wa nchi yetu na kuongeza nafasi za uongozi wa kisiasa, athari zake ni muungano dhaifu na gharama kubwa za uendeshaji wa serikali ktokana na uwepo wa marais watatu na serikali zao.

    Wanasisa hawa pamoja na wafadhili wao wanaamini kupitia serikali tatu rais wa jamhuri ya muungano hatokuwa na nguvu yeyote kiuongozi na hivyo kupelekea kuvunjika kwa muungano ili wao kushika uongozi (divide and rule) , hali hii itaifanya nchi yetu kukosa ushirikiano na umoja kama inavyotokea katika muungano wa visiwa vya Anjuan na mayote (Comoro) ambapo walimpindua rais sababu ya serikali tatu na Tanzania ndio iliwasaidia.

3. TUME HURU YA UCHAGUZI NA KUHOJIWA MATOKEO YA URAIS MAHAKANI.

Kipengele hichi kiko wazi kabisa kudhihirisha malengo ya wanansiasa hawa kuwa wanachohitaji ni wao kutimiza haja zao za kiuongozi na si kumsaidia mwananchi wa kawaida.

Hakuna kipengele hata kimoja tofauti na hivi ambavyo utawasikia wakiongelea katika majukwaa yao.

NI Kipengele kipi kati ya hivi wanavyopigania kinagusa na kuleta unafuu wa maisha ya mtaanzania ya kila siku Zaidi ya kuuhadaa uma kwa maslahi yao, familia zao na vyama yao?

Tuwapinge kwa nguvu zetu zote , tusiwaunge mkono na badala yake tujikite kwenye shughuli zetu za uzalishaji kwa maslahi ya familia zetu na taifa letu.
 
Wee vipi? katiba ni kwa kila mtu! sio wanasiasa tu hata wewe hapo maisha yako ya kila siku yanaongozwa na wanasiasa wanaotegemewa kuongoza kwa katiba tuliojiwekea! kwani kiongozi anatoka wapi!? mbinguni au!? inaonekana hutaki kabisa katiba mpya pole, kwa kua huu ndio muda muafaka wa katiba mpya ili izae tume ya uchaguzi ulio huru! hutaki kula kona huna ishu buku saba!
 
Nataman kujua vpi kuhusu katiba iliyopo unaona inakidhi vigezo vipi labda kiasi hatuitaji kuibadilishaa
katiba iliyopo ina sehemu nyingi za kubadilisha ambazo zina impact kwenye maisha ya wananchi wa kawaida hasa wa kada ya kati na kada ya chini ila huwezi kumsikia mwanasiasa hata siku moja akiizungumzia
 
Mjadala wa katiba mpya unapiganiwa na wanaharakati wa kisiasa wakishinikiza wananchi kuwaunga mkono, lengo lake kuu si kuwasaidia wananchi (wamachinga,mama ntilie, wafanyakazi) bali ni kuawasaidia wanasiasa hao kushika hatamu za uongozi kwa maslahi yao na familia zao, na pia kuongeza nafasi za uongozi, kuvunja muungano, kuifanya Tanzania kuwa nchi ambayo si salama kuishi, nchi ya maandamano.

Kuna vipengele vichache katika rasimu ya katiba ambavyo vinatolewa macho na wanasiasa kwa kushirikiana baadhi ya wafadhili wao wasioitakia mema nchi yetu ambapo wanaamini vikibadilishwa Tanzania itakuwa si nchi salama kuishi, nchi ya maandamano yanayopelekea watu wengi kuuliwa hovyo kama Kenya, nchi ya kuapishwa marais wawili kama Kenya, nchi isiyo na utulivu kwa wananchi wake kama, Iraq,Libya, Somalia, Syria, Palestina,Kongo, Nigeria, Sudan, Ethiopia na nyingine nyingi.

Wanaamini vipengele hivyo vikibadilishwa watavitumia kwa kuwashawishi wananchi kufanya fujo na maandamano ili wao walazimishe kupata uongozi baada ya watu kufa (si wao wala familia zao bali wamachinga, bodaboda, mama ntilie) huku wafadhili wao wakiamini fujo hizo zitawasaidia wao kuiba rasili mali zetu kama gesi , madini, wanyama pia watanufaika endapo kupitia viongozi hao wa kisiasa wanao watumia kuvuruga Amani ya nchi kwa kivuli cha demokrasia.

VIPENGELE PEKEE VYA RASIMU YA KATIBA WANAVYOPIGANIWA NA SABABU YA UHITAJI WA KILA KIPENGELE
  1. KIPENGELE CHA 73(4) KIMEBAINISHA NA KUSEMA,

    “Katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ibara hii,
    Rais ataepuka kujinasibisha, kwa namna yoyote ile, na chama chochote cha siasa au kundi lolote kwa namna ambayo inaathiri umoja wa wananchi.”

    Hichi ni kipengele mojawapo kinachopiganiwa na wasioitakia mema Tanzania.

    Kipengele hichi kinamsaidiaje mwanannchi wa kawaida? (hakina msaada wowote)
  • Wananchi hapo wametumika kama kinga na kukipa nguvu kipengele hiki, ila lengo kuu la kipengele hiki ni kumnyima mamlaka rais juu ya udhibiti wa vyama vya siasa vitakayoamua kuyafanya kuvuruga Amani ya nchi, kupitia kipengele hichi kutakuwa na maandamano kila siku na kazi hazitofanyika.
2. KIPENGELE CHA MUUNDO WA SERIKALI

Katika kipengele hichi muundo wa serikali, wanasiasa hawa wanalazimisha uwepo wa serikali tatu (3) badala ya mbili zilizopo sasa.

Serikali tatu(3) zina msaada gani kwa mmachinga na mwananchi mwingine? (hakina msaada wowote)

  • Lengo kuu la kudai serikali tatu ni kudhoofisha muungano wa nchi yetu na kuongeza nafasi za uongozi wa kisiasa, athari zake ni muungano dhaifu na gharama kubwa za uendeshaji wa serikali ktokana na uwepo wa marais watatu na serikali zao.

    Wanasisa hawa pamoja na wafadhili wao wanaamini kupitia serikali tatu rais wa jamhuri ya muungano hatokuwa na nguvu yeyote kiuongozi na hivyo kupelekea kuvunjika kwa muungano ili wao kushika uongozi (divide and rule) , hali hii itaifanya nchi yetu kukosa ushirikiano na umoja kama inavyotokea katika muungano wa visiwa vya Anjuan na mayote (Comoro) ambapo walimpindua rais sababu ya serikali tatu na Tanzania ndio iliwasaidia.

3. TUME HURU YA UCHAGUZI NA KUHOJIWA MATOKEO YA URAIS MAHAKANI.

Kipengele hichi kiko wazi kabisa kudhihirisha malengo ya wanansiasa hawa kuwa wanachohitaji ni wao kutimiza haja zao za kiuongozi na si kumsaidia mwananchi wa kawaida.

Hakuna kipengele hata kimoja tofauti na hivi ambavyo utawasikia wakiongelea katika majukwaa yao.

NI Kipengele kipi kati ya hivi wanavyopigania kinagusa na kuleta unafuu wa maisha ya mtaanzania ya kila siku Zaidi ya kuuhadaa uma kwa maslahi yao, familia zao na vyama yao?

Tuwapinge kwa nguvu zetu zote , tusiwaunge mkono na badala yake tujikite kwenye shughuli zetu za uzalishaji kwa maslahi ya familia zetu na taifa letu.
Ningependa kujua hii ya sasa inamnufaisha vipi mama ntilie, mmachingaa au dereva bodaboda?

Pia ningependa kujua tunapozungumzia wananchi, tunalenga wananchi wapi? Wakulima, wafanyabiashara, wanasiasa au watu gani?

Alafu ningependa kujua huu uongozi wa sasa unapata mamlaka kutoka kwa nani?
 
Nadhani kuna kitu ukijui au unafanya kusudi kwanza tambua hakuna binadamu aliyezaliwa mwanasiasa inatokea kutokana na mazingira na wakati uliopo, kwa mfano tu Mchungaji Peter Msigwa( MP) aliwahi kuwa machinga. Rais aliwahi kuwa Mwalimu.

2. Kwa chochote unachofanya au kufanyiwa kina uhusiano wa karibu au moja kwa moja na sera na sheria za nchi ambazo kimsingi zinatungwa na kupitishwa na wanasiasa hivyo utake au usitake siasa haiepukiki kwenye maisha yako.

Katiba mpya ni muhimu uwe mkulima uwe mpishi au mfanyakazi uwe chizi au kichaa kwa sababu hii iliyopo haiwezi tena kuleta usawa katika jamii
 
Ningependa kujua hii ya sasa inamnufaisha vipi mama ntilie, mmachingaa au dereva bodaboda?

Pia ningependa kujua tunapozungumzia wananchi, tunalenga wananchi wapi? Wakulima, wafanyabiashara, wanasiasa au watu gani?

Alafu ningependa kujua huu uongozi wa sasa unapata mamlaka kutoka kwa nani?
Hii ya sasa bado haijamnufaisha mkulima, mfanyakazi na mfanyabisahara kwa kiasi kikubwa tu ndio maana kwa nia njema ya Rais Kikwete alitaka ifanyiwe marekebisho na kuja na katiba mpya.

Hapo ndipo wanasiasa waliitumia hiyo fursa kama opportnuity ya kutaka kuharibu baadhi ya misingi ambayo ukiingusa kuirekebisha kwake inaweza ikachukua hata miongo kadhaa.....ni kweli baadhi ya misingi inahitaji marekebisho ....ila lazima kwanza ujenge uchumi wako na uhakikishe kuwa society yako ipo mature enough kuweza kuyapokea hayo mabadiliko...mfano wa mabadiliko hayo ni muundo wa serikali ya muungano.....

"Pia ningependa kujua tunapozungumzia wananchi, tunalenga wananchi wapi? Wakulima, wafanyabiashara, wanasiasa au watu gani?" ni wananchi wote but with special focus kwa wakulima, wafanyabiashara na wafanyakazi ambao ndio majority group na ndio wanao run the economy

uongozi wa sasa unapata mamlaka kutoka kwenye katiba iliyopo
 
Sasa cha ajabu unaweza kuta huyu mleta mada ni msomi wa chuo kikuu lakini haya ndo mawazo yake kwa kifupi vitu alivyovisema anaviona vinatatizo sababu vitaweka ukomo kwenye huu mfumo wa kua na mungu mtu Tanzania
 
Nadhani kuna kitu ukijui au unafanya kusudi kwanza tambua hakuna binadamu aliyezaliwa mwanasiasa inatokea kutokana na mazingira na wakati uliopo, kwa mfano tu Mchungaji Peter Msigwa( MP) aliwahi kuwa machinga. Rais aliwahi kuwa Mwalimu.

2. Kwa chochote unachofanya au kufanyiwa kina uhusiano wa karibu au moja kwa moja na sera na sheria za nchi ambazo kimsingi zinatungwa na kupitishwa na wanasiasa hivyo utake au usitake siasa haiepukiki kwenye maisha yako.

Katiba mpya ni muhimu uwe mkulima uwe mpishi au mfanyakazi uwe chizi au kichaa kwa sababu hii iliyopo haiwezi tena kuleta usawa katika jamii
nadhani unatoka nje ya mada....kama umemwelewa mtoa post concern yake ni kuwa hao wanasiasa kwenye katiba mpya wanajadiri zaidi vipengele vyenye maslai yao ya kisiasa na sio maslai ya wanachi wa kawaida....mbaya zaidi vipengele wanavyojaribu kuvijadiri vinaweza kuwa na long term effect kama society haipo matured....mfano ni ishu ya serikali tatu....huwezi kubadilisha muundo wa serikali katika nchi kama tanzania ambayo society yake haijakomaa kuwa na uwezo wa kuyapokea hayo mabadiliko
 
Sasa cha ajabu unaweza kuta huyu mleta mada ni msomi wa chuo kikuu lakini haya ndo mawazo yake kwa kifupi vitu alivyovisema anaviona vinatatizo sababu vitaweka ukomo kwenye huu mfumo wa kua na mungu mtu Tanzania
how ....embu elezea zaidi....maana mada yake ipo very clear
 
Back
Top Bottom