ismathew
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 253
- 38
Chadema ielekeze nguvu zake zaidi katika kufanikisha katiba mpya. haswa kuanzia vijijini mpaka katika mikoa yake. hili uwezekano wa katiba mpya uwe kabla Kikwete ajamaliza muda wake yaani ndani ya miaka mitatu. kwa sababu Kikwete anatambua wazi kuwa katiba mpya ndio mwisho wa ccm. na ndio maana analizungusha hilo jambo kufanyika haraka. Kwa kuwa kuna kila sababu za kikwete kuitwa Rais wa mwisho kutoka ccm. na jambo hilo ndilo linalomsumbua akili yake. Kama ccm imemfia mikononi mwake. Jambo la katiba lazima livaliwe njumu. bila hivyo udikteta utakuwa unaendellea tanzania. Miaka hamsini ya uhuru umeme hamna watu wanaumiiza vifua kwa moshi wa koroboi maendeleo yetu yanaenda katika mifuko ya watu wachache.Kwani maendeleo ya nchi ni maadili ya utendaji wa kazi. Kuhakikisha miradi yote pesa inatumika kihalali mpaka senti moja ya mwisho iliyopangiwa. Katiba sasa hivi si jambo la wananchi wote kufanya mchakato vipengele vya katiba.