Katiba Mpya: NCCR a perfect case for change!

LAT huhitaji PhD kujua kwamba vyama vikubwa vya siasa ni CCM na CDM, sasa kilichobaki ni Muswaada tu wa kuua huu utitiri wa vyama vya matumbo vyote vijiunge na hivyo vikuu viwili na kuwepo na wagombea huru!

Willy badala ya kutumia rungu kuviua ni vyema kuongeza upana wa uhalali wa vyama vya siasa kuendelea kuwepo. Lets say kama chama cha siasa hakijapata uwakilishi ndani ya chaguzi mbili kuanzia udiwani na ubunge kiwe domant. Kusiwe tena na ruzuku kwa vyama vya siasa. Hakika yake vitakufa vingi vyenyewe na wanasiasa biashara watapotea wenyewe.

Mimi naunga mkono kufukuzwa uanachama wa mwanachama yeyote ndani ya chama cha siasa pale sheria na kanuni zote pamoja na haki na uwanja wa kukata rufaa mahakamni kuwepo ili asionewe mtu. Ila swala la kutokuwa na adhabu silikubali kwani binadamu huwa ananidhamu akijua hukumu.

Nchi zote zilizoendelea zinaheshimu sheria zao kwa sababu zinawashughulikia wote wanaozivunja bila kujali aliyezivunja ni nani. kama ingekuwa Tanzania Enron leaders wangekuwa mtaani kama walivyo wa EPA kwani tunaogopa kuwajibishana. Ningefurahi Kafulila angeenda mahakamani ili kumuumbua Mbatia au kujiumbua mwenyewe. Wao ni watunga sheria lazima wawe mfano.
 
Mkuu hoja yangu ya msingi ni safe heaven for the Kafulillas ambao ni wengi kwenye vyama vyetu, ni muhimu tukawa na wagombea huru. Otherwise adhabu kwenye vyama irrelevant kama NCCR ni hasara kwa taifa na hasa stability ya Upinzani in our fragile Democracy sasa tutahitaji kuwa na uchaguzi mdogo wa bunge it is insane man look at what happened in Igunga I mean hatuwezi kuwa na the right mind kuwa na chaguzi kama zile all the times kisa kanuni za mediocre party kama NCCR! That is why we need to get rid of the nonsense I mean wewe tell me what is CUF? Opposition or a ruling party? How in the hell you defend this dysfunctional political party sytem? I mean Please!
 
Inashangaza kuona watanzania wanakuwa washabiki badala ya kuwa objective. Kilichofanywa na NCCR-Mageuzi ni kitendo ambacho kina set precence mbaya sana kwa watu ambao wanatokea kutofautiana na wenyeviti wa vyama. Hili linatufanya turudi kule kule kwa zidumu fikra sahihi na inashangaza sana vijana kufurahia what has happended kwa Kafulila. Tunailalamikia CCM na serikali yake jinsi inavyo toa nguvu ya maamuzi kwa mtu au kikundi cha watu wachache and we on the other side doing the same thing..

Nashindwa kuielewa attitude ya watanzania uswahili umezidi kupita kipimo!

Willy inawezekana Watanzania wakawa wako sawa au wanakosea. Je nini amefanya Kafulila na je alikosea au alikuwa sawa? Na nini amefanya Mbatia dhidi ya Kafulila je alikosea au alikuwa sawa? Tungejikita kujadili taratibu na makosa yaliyotokea kama yapo. Mimi ningependa kusikia mjadala wenye mafunzo badala ya kutokea makundi yenye ushabiki bila susbstance.

Kama Kafulila alivunja sheria za chama chao ni zipi na zinaadhabu gani? Na je Mwenyekiti kama kavunja sheria kwa kutoa adhabu bila kanuni na katiba ya chama chao ni zipi??
Je malalamiko ya Kafulila ni kweli yalivunja sheria za chama husika. Je Kafulila alipewa nafasi ya kudhibitisha madai yake kuwa mwenyekiti wake ni pandikizi la CCM? Je Kafulila alipewa nafasi ya kuonyesha kwamba kweli alikuwa na nia ya kumtoa Mbatia na kumwingiza Zitto NCCR ili awe mwenyekiti then mgombea wa uraisi.
Je ni siri zipi ambazo NCCR walidai Kafulila kaziuza nje bila mpangilio?

Mimi nafikiri tungejadili yaliyojiri kama ya kutoa hukumu na lawama. Ninaamini ukivunja kanuni na sheria za sehemu ya kazi, chama, madaraka na kama hukumu yake ni termination sioni kama hapo kuna wa kumlalamikia hata tukibadili katiba. CCM inalalamikiwa kwa kushindwa kuwaleta wananchi maendeleo, kushindwa kuwachulia wahalifu, wahujumu hukumu kutoka na sheria. Kubembeleza wezi na wahujumu kwa kuwaogopa. Ningependa serikali yenye haki, nidhamu na inayofuta sheria na katiba bila kuonea mtu wala kumuogopa mtu. Nidhamu ya kufuata sheria lazima ianzie makazini, vyama vya siasa na Serikali.

Badala ya kuanza kulaumu je haki ilitendeka au la? Nani kavunja sheria za NCCR???
Je katiba ya NCCR ina haki au kandamizi??? Hii katiba ilishindwa kumfukuza Mrema, ila alikimbia mwenyewe? Je NCCR ni chama cha siasa au ni kambia ya Usalama wa taifa???

Je katiba mpya italinda wanachama wa vyama vya siasa hata wakivunja sheria za vyama vyao. Mfumo wa vyama vya siasa ni wa kidekta??? Je si kwamba wote Kafulila na Mbatia wanatamaa ya madaraka na ni mapandikizi ya watu wa nje Mmoja CCM na mwingine anakundi lake?

Je vita ni kati ya Kafulila na NCCR au Mbatia au ni kati ya Kafulila( waliomtuma) na Mbatia (CCM) ndani ya NCCR??
Mimi ningependa kuujua ukweli badala ya kutetea au kulaumu. Ili tuwe na mfumo mzuri ni lazima kufunua kila jiwe. Lazima tujue nia za viongozi hawa. Ningependa kuwahoji Kafulila na Mbatia pamoja na Dr Mvungi ambaye alikuwa mwenyekiti siku ile ya hukumu.

Kwa nini Kafulila alimpigia Mbatia Magoti na kumwomba msamaha kama anaamini anasimamia haki na alikuwa anasema kweli. Je Mbatia alipona vipi kwenye kitimoto kile au Dr Mvungi alimbeba ili wafanye mazingaombwe???

Willy Mfumo wa vyama vingi vya siasa duniani ni vikao na vikao vya maamuzi. je kwenye kutenda haki mfumo huu tunauonaje, haufai kwani demokrasia ya vyama vya siasa ni kura. Je mfumo huu unaaminika au hauaminiki?? Je Kafulila aliisoma katiba ya NCCR ?? Ni mfumo upi wa kuendesha vyama vya siasa ndani utakuwa huru na wenye demokrasia zaidi. Kama vyama vilivyopo vina katiba ambazo vijana wanaona haziendani na uhuru wa kidemokrasia ya kweli pamoja na uhuru wa habari; kwanini ujasiri huu usiendani na kuanzishwa kwa chama cha siasa chenye katiba huru yenye mvuto kwa kizazi cha sasa iliyojaa uhuru wa habri, haki ya kujieleza, haki ya kukataa maamuzi ya vikao halali ya vyama, katiba itakayotamka wazi hakuna mwanachama atakayefuzwa chama, adhabu kama hiyo haitakuwepo kamwe. Adhabu ya kumnyang'anya kadi mwanachama ni sawa na adhabu ya kifo.

Vile vile upande mwingine wa shilingi inauma sana pale chama kinapopoteza mbunge kwa kurudisha kadi kama Mpendezoe alivyowafanyia Magamba.
Ni nani akitendwa ni haki na akitendewa sio haki? Chama au mwanachama????

Je ni nani mwenye jukumu la kulinda chama husika cha siasa dhidi ya viwavi ambao kazi yao ni kutibua mfumo na ustawi wa chama husika cha siasa? Ni chama gani kiko tayari kufa kwa kushindwa kumwadhibu mtu mmoja? Je kiongozi akiogopa lawama ataweza kutoa maamuzi magumu.

Ni haki ya kila raia kutoa maoni mawazo, kukubali au kutokubaliana na mawazo mwenendo. Viongozi wanawajibu wakutokuwakandamiza wanaowaongoza kwa kutumia vibaya madaraka yao. Vijana tunakazi ya kuilinda demokrasia kwa kuheshimiana na kuheshimu sheria na taratibu.
 
Hamtatenda haki kwa vyama vingine; UDP, TADEA, TLP, UPDP, UMD, NLD, SAU, NRA nk. vyote vinakubalika na watanzania; Iachane demokrasia ichukue mkondo.

Kubakiza vyma vitatu siyo ufumbuzi wa matatizo yanayotokea katika vyama vya siasa tulivyonavyo, bali ni aina ya wanasiasa ambao wote ni zao la CCM wakiwa na mawazo mgando. Tusubiri kizazi chao kipite, huko zao la sekondari kata litakuja na mawazo mapya ya DIGITAL
 
Mkuu hoja yangu ya msingi ni safe heaven for the Kafulillas ambao ni wengi kwenye vyama vyetu, ni muhimu tukawa na wagombea huru. Otherwise adhabu kwenye vyama irrelevant kama NCCR ni hasara kwa taifa na hasa stability ya Upinzani in our fragile Democracy sasa tutahitaji kuwa na uchaguzi mdogo wa bunge it is insane man look at what happened in Igunga I mean hatuwezi kuwa na the right mind kuwa na chaguzi kama zile all the times kisa kanuni za mediocre party kama NCCR! That is why we need to get rid of the nonsense I mean wewe tell me what is CUF? Opposition or a ruling party? How in the hell you defend this dysfunctional political party sytem? I mean Please!

Chaguzi ndogo zinasababishwa na mambo mengi kushindwa kwenye kesi, vifo, Mbunge kuacha ubunge kwa hiari yake, kufukuzwa uanachama nk.
Kwa katiba iliyopo hata tukiwa na Independent Candidate akiamua kuacha Ubunge au akifa au akishindwa kesi ya uchaguzi bado tutarudi kwenye uchaguzi, na gharama zitakuwa kwetu walipa kodi.

Kwa maani hii tatizo sio vyama vya siasa na mifumo yao ya uongozi au mizuri au mibaya ya kufukuzana au la. Tatizo hapa ni katiba yetu. Nafikiri kwasababu tumejifunza kwenye chaguzi ndogo kuwa zinagharama badala ya kuanza kushurutisha vyama vya siasa nini wafanye ndani ya vyama vyao wakati tatizo lilopo ni la kurudiwa kwa chaguzi na sababu ni nyingi za kurudia chaguzi sio kufukuzwa tu uanachama inatupasa kutafuta suluhisho kwa sababu zote.

Tukisema chama kichague mbunge mwingine pale nafasi inapobaki wazi kwa kifo, kushindwa kesi ya uchaguzi, kunyang'anywa kadi nk kwa demokrasia ilivyo changa wengi watakuwa wahanga wa kuonewa.

Mimi napendekeza chama kilichoshinda kifanye uchaguzi huru wa ndani ili primary like, kureplace mbunge ambae kwa sababu yeyote amepoteza sifa za ubunge. Kwenye kesi za Uchaguzi, Lazima mahakama ziwe huru, kesi lazima iwe ina fair hukumu then alieshinda kesi kama ni mgombea wa pili apewe ubunge badala ya kurudi kwenye uchaguzi.
Kuhusu Mgombea binafsi kama yeye ndiye kafa, kaacha ubunge au kapoteza kwa sababu yeyote ile vyama vilivyopata kura ambazo nyingi viwili ama viwakilishe muda uliobaki kwa kupokezana au chama kilichopata kura nyingi zaidi kumalizia term ama kutafutwe njia nyingine inayofaa ambayo haitaweza kuleta kudhuriwa kwa mgombea huru kwa uchu wa madaraka.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom