Katiba Kenya: IGP si lazima awe polisi!

Beso

JF-Expert Member
May 6, 2011
216
59
Kwa mujibu wa itv hbr za afrika mashariki,kutoka kenya ni kwamba mkuu mpya wa jeshi la polisi atakuwa sio lzm awe polisi itategemea timu ya usaili imeona nani anafaa!nawasilisha.
 
Katiba hiyo hiyo inasema mawaziri watakuwa proffesionals na siyo wabunge kama ilivyozoeleka.
 
Wallahi; hili taifa litatisha muda mfupi ujao. I can even predict not only in EA but also within sub-Saharan, Kenya will be the second giant after South Africa in the very very very near future.

Nigeria wao wamekalia udini pamoja na kuwa na wasomi
lukuki matapeli na wala rushwa waliokubuhu pamoja na ma-resources (mafuta) waliyo nayo. Uganda nayo inakuja kwa kasi ya kutisha na hivi karibuni wataanza kuchimba mafuta ila kikwazo ni huyu presidaa wao anayetawala kwa mazoea. Hapa kwetu bado tumekalia ma-politiki ya kipuuzi na maujinga kama yale Nigeria.

Mungu Ibariki Kenya.
 
hapa kwetu umesoma hujasoma bado utakuwa kiongozi

Mkuu naomba nitofautiane na wewe. Kama unamaanisha kiongozi bora basi sifa ya kwanza, kama tukizipanga kwa mtiriko wa umuhimu, ya kiongozi bora sidhani kama ni kiwango chake cha elimu. Nadhani kuna sifa za kwanza na za muhimu kuliko elimu.

Wala kuwa na kiongozi aliyesoma sana kwangu sio la muhimu sana hadi masuala mengine pia yamezingatiwa. UONGOZI unahitaji sifa nyingine za ziada zaidi ya usomi vingenevyo hugeuka UTAWALA.

Nikupe mfano: Hivi karibuni (nadhani umesikia) UTAWALA wa UDSM uliojaa wasomi wa kiwango cha juu kabisa ulivyoamua kuwafukuza "forever" wanafunzi kadhaa tena kwa masharti eti hawaruhusiwi kudahiliwa (admitted) kwenye chuo kingine chochote nchini. Ukilitazama hili suala hata Kikatiba sidhani kama ni sahihi. Huu sasa ni UTAWALA na sio UONGOZI pamoja na usomi wao.
 
Mkuu naomba nitofautiane na wewe. Kama unamaanisha kiongozi bora basi sifa ya kwanza, kama tukizipanga kwa mtiriko wa umuhimu, ya kiongozi bora sidhani kama ni kiwango chake cha elimu. Nadhani kuna sifa za kwanza na za muhimu kuliko elimu.

Wala kuwa na kiongozi aliyesoma sana kwangu sio la muhimu sana hadi masuala mengine pia yamezingatiwa. UONGOZI unahitaji sifa nyingine za ziada zaidi ya usomi vingenevyo hugeuka UTAWALA.

Nikupe mfano: Hivi karibuni (nadhani umesikia) UTAWALA wa UDSM uliojaa wasomi wa kiwango cha juu kabisa ulivyoamua kuwafukuza "forever" wanafunzi kadhaa tena kwa masharti eti hawaruhusiwi kudahiliwa (admitted) kwenye chuo kingine chochote nchini. Ukilitazama hili suala hata Kikatiba sidhani kama ni sahihi. Huu sasa ni UTAWALA na sio UONGOZI pamoja na usomi wao.

Yale ya UDSM ni maamuzi ya kisiasa. Uongozi wote wa chuo unatumika kisiasa kuanzia kwa Mkandara mwenyewe. Wanafunzi wana madai ya msingi lakini utasikia uongozi wa chuo unasema wanafunzi wanatumiwa na vyama vya siasa! Tatizo ni katiba inayompa mamlaka Rais kuwateua viongozi wakuu wa vyuo vya umma. Katiba mpya inabidi iliangalie hilo ili hawa watendaji wakuu wa vyuo vya umma wawe independent kwenye maamuzi. Lakini pia akina Mkandara nao ni wapuuzi na wao wamesoma chuo hicho hicho na wanajua matatizo yanayowakabili wanafunzi.
 
Watu wanashabikia shabikia tu hata upuuzi wanashabikia tu!! Hivi hamuoni kuwa katiba hiyo ni ya kijuha kama walivyo majuha wakenya wengi. Inakuwaje eti waziri awe professional halafu polisi igp anayesimamia amani na usalama wa raia asiwe na profession. Upu....mbafu mtupu baadhi mnashabikia tu shhiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiit!
 
Watu wanashabikia shabikia tu hata upuuzi wanashabikia tu!! Hivi hamuoni kuwa katiba hiyo ni ya kijuha kama walivyo majuha wakenya wengi. Inakuwaje eti waziri awe professional halafu polisi igp anayesimamia amani na usalama wa raia asiwe na profession. Upu....mbafu mtupu baadhi mnashabikia tu shhiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiit!

Kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba kutakuwa na vigezo ambavyo mtu anayetaka kuwa IGP itabidi atimize. Siyo tu kwamba ataibuliwa mtu ambaye hana vigezo kuwa IGP. Mfano ni IGP wao wakati wa kipindi cha vurugu za uchaguzi 2008 alikuwa ni Jenerali wa Jeshi la Kenya. Hata majirani zetu Uganda IGP wao ametokea Jeshini.
 
Back
Top Bottom