Anko Sam
JF-Expert Member
- Jun 30, 2010
- 3,200
- 820
Kwa mapendekezo yangu Katiba Mpya inatakiwa iweke wazi mambo yafuatayo:-
Hapa ni kwa nafasi za Urais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakurugenzi wa Wizara/Mikoa na Wilaya, Mkuu wa Mkoa/Wilaya, Wabunge, Madiwani,
1: Katiba itamke upatikanaji wa kiongozi huyo.
-Je, niwakuchaguliwa au niwakuteuliwa ama wakuomba kazi kwa barua!
2: Itoe Madaraka na Mamlaka kwa kiongozi husika:
-Mipaka ya Madaraka, Mamlaka na Uwajibikaji wake uainishwe kwenye kitabu
kingine kitakacho chambua na kuweka mipaka ya utendaji wake. (Maadili nayo
yawe humo)
2: Katiba iweke muda maalumu wa kiongozi huyo kukaa madarakani.
-Awe na ukomo wa vipindi au la.
3: Katiba iweke WAZI jinsi ya kumuondoa Madarakani kiongozi huyo.
-Kama atakuwa amevuja kifungu chochote cha Katiba hiyo au Kiapo chake.
-Kama atakuwa ametuhumiwa au kutenda kosa lolote la jinai.
Kwa hiyo kuwe na katiba na vitabu vingine vitakavyo kuwa na nguvu ya kisheria vikielezea kwa undani vifungu vya Katiba Mpya.
Wananchi nao haki zao za msingi na wajibu wao kwa Taifa zitatamkwe na kutambuliwa na Katiba Mpya.
1: Haki ya kuishi kwa Raia Mwema
- Kama Mtu akivunja haki ya mtu mwingine, kama kuiba, kuumiza mwili, kutishia
nk, mtu huyo anstahili naye haki zake zivunjwe!
2: Raia awe na haki ya kuchagua ama kuchaguliwa kuwa kiongozi wa kisiasa.
- Asilazimishwe kujiunga na genge fulani la kisiasa ndiyo achague ama
kuchaguliwa kuwa kiongozi wa jamii husika.
3: Raia awe huru kuandamana ama kukusanyika na kujadili mambo yao bila
kubughudhiwa.
-Kama jamii moja ina amua kwa pamoja kukusanyika na kuandamana kwenda
kwenye eneo la kuzungumzia, wawe huru na wasizuiliwe kwa namna yeyote ile.
Mihimili ya Dola, yaani Serikali, Bunge na Mahakama visi-ingiliwe katika utendaji wake. Ila Bunge ndo sauti ya wananchi liwe na MAMRAKA ya kuhoji utendaji wa mihimili mingine.
1: Bunge kwa sababu ni Chombo cha uwakilishi wa wananchi, kitachagua Spika wake.
-Waziri mkuu awe ni kilanja wa shughuli za Serikali bungeni, yaani awe kiongozi wa
mawaziri na makatibu wakuu kuweka mambo sawa serikali inapo banwa na
wabunge. Asiwe mtu wa kuwa kolomea wabunge na kuwapa majibu mepesi kwa
maswali magumu.
2: Rais atapendekeza majina ya Majaji wa Mahakama Kuu/Rufaa wakathibitishwe
na Bunge (Wananchi).
-Bunge ndilo litakuwa na madaraka ya kumuondoa Jaji akionekana hatendi haki.
Vyombo vingine vya maamuzi kama TUME HURU ya Uchaguzi, iwe na wajumbe kutoka kwenye taasisi zinazoheshimika ziwe za kidini, kijamii, Senior citizens, Wanasheria nguli, wanaharakati wa makundi yote nk nk.
Naomba kuwasilisha!
Hapa ni kwa nafasi za Urais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakurugenzi wa Wizara/Mikoa na Wilaya, Mkuu wa Mkoa/Wilaya, Wabunge, Madiwani,
1: Katiba itamke upatikanaji wa kiongozi huyo.
-Je, niwakuchaguliwa au niwakuteuliwa ama wakuomba kazi kwa barua!
2: Itoe Madaraka na Mamlaka kwa kiongozi husika:
-Mipaka ya Madaraka, Mamlaka na Uwajibikaji wake uainishwe kwenye kitabu
kingine kitakacho chambua na kuweka mipaka ya utendaji wake. (Maadili nayo
yawe humo)
2: Katiba iweke muda maalumu wa kiongozi huyo kukaa madarakani.
-Awe na ukomo wa vipindi au la.
3: Katiba iweke WAZI jinsi ya kumuondoa Madarakani kiongozi huyo.
-Kama atakuwa amevuja kifungu chochote cha Katiba hiyo au Kiapo chake.
-Kama atakuwa ametuhumiwa au kutenda kosa lolote la jinai.
Kwa hiyo kuwe na katiba na vitabu vingine vitakavyo kuwa na nguvu ya kisheria vikielezea kwa undani vifungu vya Katiba Mpya.
Wananchi nao haki zao za msingi na wajibu wao kwa Taifa zitatamkwe na kutambuliwa na Katiba Mpya.
1: Haki ya kuishi kwa Raia Mwema
- Kama Mtu akivunja haki ya mtu mwingine, kama kuiba, kuumiza mwili, kutishia
nk, mtu huyo anstahili naye haki zake zivunjwe!
2: Raia awe na haki ya kuchagua ama kuchaguliwa kuwa kiongozi wa kisiasa.
- Asilazimishwe kujiunga na genge fulani la kisiasa ndiyo achague ama
kuchaguliwa kuwa kiongozi wa jamii husika.
3: Raia awe huru kuandamana ama kukusanyika na kujadili mambo yao bila
kubughudhiwa.
-Kama jamii moja ina amua kwa pamoja kukusanyika na kuandamana kwenda
kwenye eneo la kuzungumzia, wawe huru na wasizuiliwe kwa namna yeyote ile.
Mihimili ya Dola, yaani Serikali, Bunge na Mahakama visi-ingiliwe katika utendaji wake. Ila Bunge ndo sauti ya wananchi liwe na MAMRAKA ya kuhoji utendaji wa mihimili mingine.
1: Bunge kwa sababu ni Chombo cha uwakilishi wa wananchi, kitachagua Spika wake.
-Waziri mkuu awe ni kilanja wa shughuli za Serikali bungeni, yaani awe kiongozi wa
mawaziri na makatibu wakuu kuweka mambo sawa serikali inapo banwa na
wabunge. Asiwe mtu wa kuwa kolomea wabunge na kuwapa majibu mepesi kwa
maswali magumu.
2: Rais atapendekeza majina ya Majaji wa Mahakama Kuu/Rufaa wakathibitishwe
na Bunge (Wananchi).
-Bunge ndilo litakuwa na madaraka ya kumuondoa Jaji akionekana hatendi haki.
Vyombo vingine vya maamuzi kama TUME HURU ya Uchaguzi, iwe na wajumbe kutoka kwenye taasisi zinazoheshimika ziwe za kidini, kijamii, Senior citizens, Wanasheria nguli, wanaharakati wa makundi yote nk nk.
Naomba kuwasilisha!