ISMAIL MKIMBIZI
Senior Member
- Jan 13, 2013
- 192
- 23
Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA umekuwa tatizo kuu linalo isumbua CCM kiasi cha kuanza mikakati kudhoofisha jitihada zinazofanywa na umoja huu kivyovyote vile hata kwa kufanya makosa ya jinai, imefahamika mjini hapa. Hii imetokana na ukweli kuwa umoja huo umeonyesha taa ya kijani kwa mafanikio ya kuiondoa CCM madarakani, hivyo kila upande unaoonekana kuhusika na UKAWA kufanyiwa kila aina ya hila. Jinai hizo ni pamoja na kushusha bendera za CHADEMA na NCCR MAGEUZI na kuzichoma moto.
Hali imezidi kuwa mbaya zaidi hapa Kasulu Mjini juzi baada ya kuwasili kwa Mh. Moses Machali ambaye ni Mbunge wa Jimbo hili la Kasulu Mjini, NCCR MAGEUZI akitokea Bungeni Dodoma ambapo alikuwa akihudhuria kuwawakilisha wananchi wa Kasulu katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mh. Moses Machali mbali na kuwa Mbunge pia ni waziri kivuli wizara ya UCHUKUZI akiwakilisha kambi rasmi ya upinzani bungeni, na pia ni Naibu Katibu Mkuu NCCR MAGEUZI TAIFA chama ambacho ni wadau wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA.
Hii imemuongezea maadui mamluki wanaopandikizwa na CCM ili kudhoofisha jitihada zake za mapambano dhidi ya serikali dhalimu ya CCM. Muda mfupi kuanzia sasa ikifika saa 9:00 alasiri atakuwa akizungumza na wafanyabiashara wa Kasulu Mjini katika ukumbi wa COmmunity Centre. Kuna tetesi kuwa agenda kuu ni SERIKALI YA CCM HAITAKIWI IONDOLEWE MADARAKANI, SERIKALI TATU HAZIEPUKIKI, na WAJIBU NA UMUHIMU WA WAFANYABIASHARA KWA MAENDELEO YA KASULU NA TAIFA KWA UJUMLA.
Ujio huu wa Moses Machali umekumbwa na changamoto ya mamluki kushusha bendera iliyokuwa Stand ya Taxi Kasulu Mjini jana jioni. Hivi karibuni ilishushwa ya CHADEMA iliyokuwa Standi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani shughuli ambayo inaratibiwa na UVCCM Kasulu na kutekelezwa na baadhi ya vijana wa kijiwe cha waendesha bodaboda Stand Kuu ya Taxi Kasulu Mjini. Ninawasikitikia ukiwaangalia ni wasakatonge, mguu nje mguu ndani watakuja kujuta kushusha bendera hizo ambazo walizichoma moto.
Hali hiyo inasababishwa na ukweli kwamba hapa Mjini Kasulu hakuna vyama pinzani pasua kichwa kwa CCM kama CHADEMA na NCCR MAGEUZI, hivyo basi kwa kuwa kinafasi ya ubunge Moses anaonekana kuwa ndiye ana nafasi kubwa mpaka sasa ya kurudi Bungeni 2015 wanaendesha hila hizo kukwamisha jitihada za muungano wa UKAWA ukizingatia CCM wanawasiwasi ikiwa UKAWA watasimamisha mgombea ubunge mmoja na kumuunga mkono, Kasulu mjini lazima atakuwa Mh.Moses Machali. Hii inawapasua kichwa CCM hawalali. Mbali na kikao hicho cha ndani Jumamosi tarehe 05/07/2014 atakuwa na mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya stand ya taxi Kasulu Mjini.
VIVA UKAWA, VIVA MACHALI ALUTA CONTINUA.
Hali imezidi kuwa mbaya zaidi hapa Kasulu Mjini juzi baada ya kuwasili kwa Mh. Moses Machali ambaye ni Mbunge wa Jimbo hili la Kasulu Mjini, NCCR MAGEUZI akitokea Bungeni Dodoma ambapo alikuwa akihudhuria kuwawakilisha wananchi wa Kasulu katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mh. Moses Machali mbali na kuwa Mbunge pia ni waziri kivuli wizara ya UCHUKUZI akiwakilisha kambi rasmi ya upinzani bungeni, na pia ni Naibu Katibu Mkuu NCCR MAGEUZI TAIFA chama ambacho ni wadau wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA.
Hii imemuongezea maadui mamluki wanaopandikizwa na CCM ili kudhoofisha jitihada zake za mapambano dhidi ya serikali dhalimu ya CCM. Muda mfupi kuanzia sasa ikifika saa 9:00 alasiri atakuwa akizungumza na wafanyabiashara wa Kasulu Mjini katika ukumbi wa COmmunity Centre. Kuna tetesi kuwa agenda kuu ni SERIKALI YA CCM HAITAKIWI IONDOLEWE MADARAKANI, SERIKALI TATU HAZIEPUKIKI, na WAJIBU NA UMUHIMU WA WAFANYABIASHARA KWA MAENDELEO YA KASULU NA TAIFA KWA UJUMLA.
Ujio huu wa Moses Machali umekumbwa na changamoto ya mamluki kushusha bendera iliyokuwa Stand ya Taxi Kasulu Mjini jana jioni. Hivi karibuni ilishushwa ya CHADEMA iliyokuwa Standi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani shughuli ambayo inaratibiwa na UVCCM Kasulu na kutekelezwa na baadhi ya vijana wa kijiwe cha waendesha bodaboda Stand Kuu ya Taxi Kasulu Mjini. Ninawasikitikia ukiwaangalia ni wasakatonge, mguu nje mguu ndani watakuja kujuta kushusha bendera hizo ambazo walizichoma moto.
Hali hiyo inasababishwa na ukweli kwamba hapa Mjini Kasulu hakuna vyama pinzani pasua kichwa kwa CCM kama CHADEMA na NCCR MAGEUZI, hivyo basi kwa kuwa kinafasi ya ubunge Moses anaonekana kuwa ndiye ana nafasi kubwa mpaka sasa ya kurudi Bungeni 2015 wanaendesha hila hizo kukwamisha jitihada za muungano wa UKAWA ukizingatia CCM wanawasiwasi ikiwa UKAWA watasimamisha mgombea ubunge mmoja na kumuunga mkono, Kasulu mjini lazima atakuwa Mh.Moses Machali. Hii inawapasua kichwa CCM hawalali. Mbali na kikao hicho cha ndani Jumamosi tarehe 05/07/2014 atakuwa na mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya stand ya taxi Kasulu Mjini.
VIVA UKAWA, VIVA MACHALI ALUTA CONTINUA.