Taifa imara ni intergration ya familia imara na ili uweze kuwa na familia imara basi lazima kuwe na ndoa imara ambayo imejengwa katika misingi halisi ya upendo na ndoa iliyojengwa ktk misingi ya upendo siku zote huwa ya furaha na amani.Ndoa nyingi zipo hoi au zishakufa ,ndio maana siku hizi masingo maza kibao,watoto wamitaani,mitototo yenye tabia mbovu ni output ya ndoa zilizokosa upendo hatimaye kuvunjika.
Ujue wakati mnaingia kwenye ndoa kuna maneno ya viapo wakati wa ndoa ambayo kabla ya kutaka kufunga ndoa lazima ujipime utayaweza kuyashika na kuyaishi "kwa ugonjwa na uzima,utajiri na umasikini",kama huwezi usingie kwenye ndoa kwani utakuwa msalaba ambao utamkosesha mwenzako furaha na amani(utamfanya ahisi yupo kuzimu)..
Tatizo ndoa nyingi zinavunjika sababu wanandoa wenyewe ni wabinafsi na ubinafsi wao wanaingia nao mpaka kwenye ndoa zao mwisho wa siku ndoa chali.Ndoa ni kushare amani,furaha,ufukara,uzima,kipato nk ila kuna watu hao changu changu ,chako changu na kuna wengine wanaingia kwenye ndoa basi ili mradi lkn zipu zao mbovu.
Kitu chengine kinachovunja ndoa hii 50/50 hasa kwa wanawake wenye vipato na elimu kubwa ,hela zao huwapa kiburi.Fanya ufanyavyo huwezi kuenda against na mungu,kwani yeye ndio muasisi wa ndoa, kwa hiyo ili ndoa idumu lazima kila mtu atimize mahukumu yake ya asili aliyopewa na mungu.
Na asikudanganye mtu hakuna maisha magumu kama ya upweke(siku zote wawili ni wawili tu),japo kuna baadhi ya ndugu zangu wana maeno yao ya kishujaa "kwani lazima kuolewa au kuoa".Kuoa au kuolewa si lazima lkn je utaweza kuishi kadri ya mungu alivyotuagiza au utaweza kuzishinda tamaa za kimwili.Usiombee ktk maisha yako ukamkosa mtu wakukushauri,kukufariji,kukuliwaza,kufukurahisha,kukutia nguvu wakati umekata tamaa na kushare nae maumivu ya ndani kotoka katika moyo wako basi utakuwa na msongo wa mawazo na kudondokea kwa wanaume au wanawake mbali mbali mwisho wa siku utu na thamani yako itashuka na utakuwa mtu mwenye maisha ya kutanga tanga.