Karibu Prof. Mama Anna Tibaijuka ndani ya JamiiForums!

Status
Not open for further replies.
mbona wajameni mimi hamkunikaribishaga hivi? binadamu wote ni sawa na Afrika ni moja --kaulimbiu ya TANU/
 


Mkuu wa kaya yupo sana umu ndani sema nae kajivalisha jina feki.
 
Hawa ndio viongozi wa ccm waliosalia wengine wote wako analojia na taifa haliwataki
 
Mimi nina swali.

Kwa nini wafugaji wa Tanzania hawathaminiwi na hawapewi kipaumbele chochote kuhusu matumizi ya ardhi? Je kuna ulazima gani ardhi yetu kugawiwa wawekezaji wa nje wakati wafugaji wa Tanzania wakirandaranda kama yatima?
 
Karibu mtani wangu,

Naomba nikukaribishe kwa swali lifuatalo kuhusu kupanda kwa gharama za ardhi. Nakumbuka katika bunge la bajeti la 2012/13 bunge lilikuruhusu ku-review gharama za ardhi. Nawe bunge lilipoisha ukarudi ofisini na kufanya kazi hiyo. Kinachonisikitisha ni jinsi ulivyopandisha gharama za ardhi zingine kwa zaidi ya asilimia 100,000%.

Wanachi wa kipato cha chini sasa wanakiona. Suala la ardhi sasa ni la wenye nazo. Mfano zamani uliweza kufungua kesi katika baraza la ardhi na nyumba la wilaya kwa fedha kidogo, nadhani elfu 20,000 kutegemea subject matter. Lakini leo ni balaa, kama huna laki huko huchomi na haki yako itapotea. Pia hata aliyeshtakiwa anapaswa kutoa kiasi kisichopungua 20,000/= ili a-file utetezi wake. Yaani mtaani ni balaa maskini atashindwa kwenda katika hilo baraza.

Sasa ukienda pale wizarani ku-register nyaraka kama deed poll etc ambazo tulikuwa tunatumia elfu 10,000 leo ni zaidi ya 50, yaani garama ni balaa. Tukija kwa watu wenye vihamba, kodi kwenye saizi tuseme SQM 1600 zamani ilikuwa kama elfu 15,000 hivi kwa mwaka leo ardhi hiyo hiyo ni zaidi ya elfu 50,000, Mh. mbona umeamua kuwafanya watanzania wa kawaida waogope ardhi yao?. Sasa swali langu lenye vipengele ni:

Kwanni garama za ardhi zimepanda kwa kiwango kikubwa kiasi hicho tena mara moja
Je huoni ardhi itabaki kuwa ya wanyarubanja wachache
Nani anamtetea maskini ambaye ana ardhi kidogo inayompa mlo mmoja kwa siku, leo nikitaka kumdhulum maskini huyo naenda kwenye baraza ambalo najua atakoswa hela za ku-file utetezi
 
Sasa mbona mnaanza kumtisha prof wa watu jamani?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Karibu...mgeni...wenyeji tushibe........hivi kwanini hukuogopa kuhudhuria kigoda cha Mwalimu? au kwa kuwa ulifundisha UDSM? wenzako wanaogopa kuzomewa....ila ww uliishia kushangiliwa.......ila hapa JF uwe mvumilivu kwa kuwa hatuumi maneno....u mfano wa kuigwa mama yangu.
 
Nami niungane na wana jamvi wenzangu kumpongeza na kumkaribisha Mama Tibaijuka jamvini. Jamvi linazidi kupata popularity na heshima kwa viongozi kama hawa kujiunga nasi tena waziwazi. Karibu sana mama
 
Atanisaidiaje. Nimeomba kiwanja wiizarani kwake najibiwa siwezi kumilikishwa. Swali lini nilipewa?
 
Nimefurahi sana kuingia kwako Profesa Tibaijuka. Ukumbi huu unaogopwa sana na watu wenye makando kando mengi, lakini natambua kuwa wewe si miongoni mwao, ndio maana ukajitokeza wazi kwa ID yako inayotambulika. Karibu sana.

Mkuu.
Heshima yako! Nimefurahi kukusoma hapa jamvini. Ubarikiwe sana!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…