Karibu mtani wangu,
Naomba nikukaribishe kwa swali lifuatalo kuhusu kupanda kwa gharama za ardhi. Nakumbuka katika bunge la bajeti la 2012/13 bunge lilikuruhusu ku-review gharama za ardhi. Nawe bunge lilipoisha ukarudi ofisini na kufanya kazi hiyo. Kinachonisikitisha ni jinsi ulivyopandisha gharama za ardhi zingine kwa zaidi ya asilimia 100,000%.
Wanachi wa kipato cha chini sasa wanakiona. Suala la ardhi sasa ni la wenye nazo. Mfano zamani uliweza kufungua kesi katika baraza la ardhi na nyumba la wilaya kwa fedha kidogo, nadhani elfu 20,000 kutegemea subject matter. Lakini leo ni balaa, kama huna laki huko huchomi na haki yako itapotea. Pia hata aliyeshtakiwa anapaswa kutoa kiasi kisichopungua 20,000/= ili a-file utetezi wake. Yaani mtaani ni balaa maskini atashindwa kwenda katika hilo baraza.
Sasa ukienda pale wizarani ku-register nyaraka kama deed poll etc ambazo tulikuwa tunatumia elfu 10,000 leo ni zaidi ya 50, yaani garama ni balaa. Tukija kwa watu wenye vihamba, kodi kwenye saizi tuseme SQM 1600 zamani ilikuwa kama elfu 15,000 hivi kwa mwaka leo ardhi hiyo hiyo ni zaidi ya elfu 50,000, Mh. mbona umeamua kuwafanya watanzania wa kawaida waogope ardhi yao?. Sasa swali langu lenye vipengele ni:
Kwanni garama za ardhi zimepanda kwa kiwango kikubwa kiasi hicho tena mara moja
Je huoni ardhi itabaki kuwa ya wanyarubanja wachache
Nani anamtetea maskini ambaye ana ardhi kidogo inayompa mlo mmoja kwa siku, leo nikitaka kumdhulum maskini huyo naenda kwenye baraza ambalo najua atakoswa hela za ku-file utetezi