karibu kiti Rafiki, unipe japo ushauri!

karibu kiti Rafiki, unipe japo ushauri!

kindikinyer leborosier

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2018
Posts
492
Reaction score
929
Salam za Upendo mwingi kwenu wanajamii,
.
Mimi huyu kindikinyer kijana wenu, ninataka nipate mke nioe! Umri unaenda na sioni sababu ya mimi kubaki hivi! Sasa tatizo linakuja kuna mwanamke nampenda ila simwelewi kwakweli!
.
.
Miaka ya nyuma nilikua namfwatilia akachomoa! Akanitumia mpk picha za mshkaji wake (ambae baadae nilijua hawawezi kuoana yeye mkatoliki jamaa mwislam), nilisononeka sana! Basi nikatulia miaka ikazidi kusonga!
.
.
Ila kila baada ya miezi sita nikawa namtxt "vp mrembooo" "upo poa wewee" au nilikua nikisubiri siku yake ya kuzaliwa au akiwa anafanya mitihani hua namtakia kila la kheri! mwanzo alikuwa akirespond negatively ila miaka mitatu baadae akawa anarespond positivly tunachat vizuri tunataniana hivyo!
.
.
Hajawahi nitafuta hata mara moja! Hali inayonipa msononeko sanaaa! Nikawa namtoa kabisa moyoni, kuna siku nikapewa story niliwahi kwenda msalimia shule kipindi hicho, nikaambiwa alivopata habari kua kuna mtu anaitwa kindikinyer amekuja.. alibeba ndoo ya maji akakimbia bafuni akafungua begi la nguo akamwaga kitandani.. hatimae akavaa ndipo akaja, kiukwel alipendeza,!!😂😂😂
.
.
Baada ya kusikia vile ilinibidi nirudishe mashambulizi... kua kumbe yupo hivi nimekamata tention yake.. lkn nikabaki na maswali why ana ni ignore.. why why?
.
.
Kuhusu mawasiliano hua hapend nione status zake watsap, amefuta namba zangu za watsap, mwanzo nilikuwa kila nikimtafuta lzima nijitambulishe, mwanzo nilikuwa nachukia kweli ila baadae ikanibidi nizoee si napenda bwana.. achana na mapenzi!
.
.
Najua wapo watakaosema mpe helaa!! Mpe helaàaa.. mwanzo niliwahi mtumia kidogo zamani, na alikua akipokea!! Lkn baadae alibadilika kuna siku nilimtumia vocha akaacha hakuiunga!! Doooh! (Kidogo kwao wana uwezo), niliwahi mkabidhi mdogo wangu kwake kipindi wanasoma aisee dogo alipewa heshima zote kama dada yake!(hapa ndo hua nazidi kumpenda) napenda mtu anaependa ndugu zangu.. loh!!
.
.
Kwa sasa tupo mbali yupo Arusha nipo Mwanza.. mwaka jana amehitimu Chuo yupo nyumbani, huyu anaenda kuolewa na nitaumia ila nitazuga nipo ok.
.
.
Mabaharia, wavuvi manahodha marubani woote nifanyaje nipeni maujuzi!
.
Nb. Nitafanyia kazi ushauri wenu na nitakuwa nikileta mrejesho kwa kila hatua!
.
.
Wasalaam Kindikinyer!
.
.
[Mea culpa, mea culpa, mea maxima culpa]
 
Ushauri wangu kwako ni mfupi tu... tumia akili kufanya maamuzi, na sio moyo!

Ukitumia akili, kuna uwezekano mkubwa sana ukafanya maamuzi sahihi ambayo hutakuja kuyajutia mbele ya safari!!

Kinyume chake, ukifanya maamuzi kwa kutumia ushawishi wa moyo peke yake, basi moja ya mambo unayotakiwa kujiandaa nayo ni kama yale yaliyomkumba ndugu yetu The golden anayelazimishwa na mkewe akamuombe msamaha kanisani mbele ya waumimi, ingawaje inaonekana hivi sasa anatumia akili kwenye ku-handle sakata lake!!!

Tumia akili kwa 75% na moyo upe 25% TU!!!
 
Mi nakushauri usubiri kwanza aolewe ili moyo wako upate kuamini kwamba huyo Sasa si wako na hakupendi kwelikweli. Hapo utaweza kumove on.
Ila mwanangu we king'ang'anizi kwelikweli!
 
Mapenzi hayalazimishwi
Mapenzi hayafichiki
Mapenzi hayababaishi
Mapenzi huvumilia
Mapenzi kustiriana

Usiseme unamuoa mtu kwa sababu umempenda


Muoe kwa sababu amekupenda na yupo tayari

Muoe kwa sababu mna chemistry mnaweza kukaa kuzungumza serious issues mkafikia tamati.

Usilazimishe mapenzi
Anaweza kukubali kwa sababu hana option...

Siku chaguo la moyo wake likipatikana nyumba itageuka tanuru.
 
Mapenzi hayalazimishwi
Mapenzi hayafichiki
Mapenzi hayababaishi
Mapenzi huvumilia
Mapenzi kustiriana

Usiseme unamuoa mtu kwa sababu umempenda


Muoe kwa sababu amekupenda na yupo tayari

Muoe kwa sababu mna chemistry mnaweza kukaa kuzungumza serious issues mkafikia tamati.

Usilazimishe mapenzi
Anaweza kukubali kwa sababu hana option...

Siku chaguo la moyo wake likipatikana nyumba itageuka tanuru.
Tatizo vijana wasikuhizi ni wabishi sana
 
Back
Top Bottom