Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,272
Katika biashara au maisha kukopa na kukopesha ni mambo ya kawaida. Na kwa kawaida wakopaji huwa na lugha nzuri na laini wakati wa kukopa ikiwa imesheheni ahadi tele za kulipa mapema bila usumbufu. Jambo la ajabu wengi wao wakishafanikiwa kupata mkopo hawatimizi ahadi zao na sasa kazi inakuwa kwa mkopeshaji kuanza kumtafuta mdaiwa na kudai deni. Mimi katika shughuli zangu nimekumbana na kauli za hovyo na zisizo za kistaarabu kutoka kwa wadeni wangu na sijui kwanini wakopaji huwa wakorofi na wakali wanapodaiwa. Huenda na ninyi wenzangu mmekumbana na hali hii Mfano baadhi ya kauli nilizokumbana nazo wakati nikiwadai wadeni wangu ni kama:
1. Nitalipa tu mbona hata serikali inadaiwa sembuse mimi?
2. Usinitishe na vijihela vyako uchwala kwani unafikiri ndio vinavyoniweka mjini?
3. Yaani vijisenti hivyo ndivyo vinavyokufanya uje kunigongea mlango?
4. Wangapi wanadaiwa bwana?
5. Nitakulipa nikipata!
Sasa ukiwapigia simu wengine hawajibu au watakwambia wako safarini mara Arusha ,Mwanza, Songea mara wengine wamefiwa ili mradi sasa inakuwa matanga wakati wa kukopa ilikuwa harusi. Wakopaji acheni hizo!
1. Nitalipa tu mbona hata serikali inadaiwa sembuse mimi?
2. Usinitishe na vijihela vyako uchwala kwani unafikiri ndio vinavyoniweka mjini?
3. Yaani vijisenti hivyo ndivyo vinavyokufanya uje kunigongea mlango?
4. Wangapi wanadaiwa bwana?
5. Nitakulipa nikipata!
Sasa ukiwapigia simu wengine hawajibu au watakwambia wako safarini mara Arusha ,Mwanza, Songea mara wengine wamefiwa ili mradi sasa inakuwa matanga wakati wa kukopa ilikuwa harusi. Wakopaji acheni hizo!