palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,462
- Binti anayedaiwa kubakwa ahojiwa siku mbili
HATIMAYE binti anayedaiwa kubakwa na Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), amefungua jalada Polisi dhidi ya mbunge huyo.
Habari za kipolisi ambazo gazeti hili limezipata, zinasema kuwa binti huyo ambaye anadai kubakwa na kisha kutishiwa kuuawa na Profesa Kapuya, amefungua jalada namba OB/RB/21124/13 katika Kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Harakati za kufungua jalada hilo zilianza juzi jioni na kuendelea hadi jana ambapo polisi walitumia zaidi ya saa 12 kumhoji binti huyo anayedaiwa kubakwa ili kupata ukweli wa sakata hilo.
Akiwa kituoni hapo, binti huyo alikutana na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi ya Oysterbay (OCD) na OC-CID wake na kutoa maelezo ya awali kabla ya viongozi hao kumruhusu ayaweke malalamiko yake katika maandishi kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alikiri polisi kufungua jalada hilo na kuongeza kwamba hivi sasa wanafanya uchunguzi kubaini kama ujumbe ulio katika simu ya binti anayedai kubakwa na kutishiwa maisha unatoka katika simu ya mbunge huyo.
Tumefungua jalada, lipo kwa ajili ya uchunguzi na tukibaini kuwa ni nani anahusika na tuhuma hizo tutamsaka na kumkamata popote alipo, alisema Wambura.
Habari zaidi zinasema polisi wamechukua namba ya Kapuya inayodaiwa kutumika mara kwa mara kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwa binti huyo, akitishiwa kuuawa.
http://www.freemedia.co.tz/daima/kapuya-aburuzwa-polisi/