Kapoteza Simu,Kabla Ya Week,Ghafla Kanunua Mpya

Kapoteza Simu,Kabla Ya Week,Ghafla Kanunua Mpya

kuchangumu

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2014
Posts
724
Reaction score
290
Poleni na swaum wana MMU
Kuna swala naomba niwashirikishe mnipe uelewa pale nisipoelewa,
Hivi hawa kina mama wanaojiunga na VICOBA ni mashari gani wanatakiwa kuyafuata wanapokuwa huko,Ili waweze kukopeshwa?
Naitataji kujuwa kwa sababu yupo jamaa mwenzi wake kapoteza Simu baada ya siku mbili akanunua nyingine kwa laki mbili.
Alipoulizwa umepata wapi pesa ya kununua simu kwa haraka namna hiyo?Alijibu ameenda kukopa Vicoba.
Je vicoba wanakopesha muda wowote?
Wanatumia kigezo gani kukupa kiwango cha fedha?
Michango yao wanaikusanya kwa vigezo gani?
Au binti alidhaminiwa na mtu mwingine akatumia kigezo cha Vicoba?
Karibuni kwa elimu ya Vicoba natumai MMU inawana vicoba wengi tu!
 
He he he.......mwanamke marejesho.......mwanamke hisa........
Preta kama unaufafanuzi wowote juu ya vicoba weka hapa mbona tena unapiga bonge la chekooo..!!!
 
Last edited by a moderator:
Huyo wala sio mwanamke wa mtu mwingine, ni wa kwako ila unaona aibu tu kusema hapa watu watakupa ukweli. Haiwezekani awe wa mtu mwingine halafu uanze kutilia shaka vyanzo vya mapato madogo madogo kama sh. laki mbili. Huwa tunatilia shaka mwanamke wa mtu akipata mali kubwa kubwa ghafla kama vile gari la gharama au nyumba kali, lakini sio hela ya simu
 
Huyo wala sio mwanamke wa mtu mwingine, ni wa kwako ila unaona aibu tu kusema hapa watu watakupa ukweli. Haiwezekani awe wa mtu mwingine halafu uanze kutilia shaka vyanzo vya mapato madogo madogo kama sh. laki mbili. Huwa tunatilia shaka mwanamke wa mtu akipata mali kubwa kubwa ghafla kama vile gari la gharama au nyumba kali, lakini sio hela ya simu

Very true!.. Shamba usilolima pilipili yakuwashia nn?
 
...mama anajua mfuko wa mumewe...MUME atalipa taraaaatibuuu
 
kwa taarifa yako ile hela nlipewa na yule baba wa mtaa wa pili hata siyo ya vikoba nlisingizia ili nisibutuliwe.mwanamke kujishughulisha babu eeee!
 
Huyo amepewa na hawara yako(mchepuko) wake sasa kama anaona wewe ni nyota nyota hutaki kumnunulia ya kwake.
 
Unatakiwa kuishi na mwanamke kwa akili sana, mtu anakumbakikia mtoto na ukajikuta unalea mtoto mpaka anakuwa mtu mzima sio watu wa kawaida
 
Vicoba huwa vinakopesha wakati wowote wanapokutana.mara nyingi hukutana kila wiki.Mkopo hutolewa kutokana na hisa zako(fedha ulizoweka)kuzidishwa mara 3.Kama umeweka hisa ya thamani ya elfu 70,wanazidisha mara 3 kwa hiyo unakopeshwa si zaidi ya laki 2 na kumi.Kwa hiyo yawezekana amekopa kweli kwenye VICOBA.
 
kwa taarifa yako ile hela nlipewa na yule baba wa mtaa wa pili hata siyo ya vikoba nlisingizia ili nisibutuliwe.mwanamke kujishughulisha babu eeee!

ha ha ha..kha! uctake ncheke mie kwel jf kuna vituko
 
Huyo wala sio mwanamke wa mtu mwingine, ni wa kwako ila unaona aibu tu kusema hapa watu watakupa ukweli. Haiwezekani awe wa mtu mwingine halafu uanze kutilia shaka vyanzo vya mapato madogo madogo kama sh. laki mbili. Huwa tunatilia shaka mwanamke wa mtu akipata mali kubwa kubwa ghafla kama vile gari la gharama au nyumba kali, lakini sio hela ya simu

Mkuu, kwa mtu mwingine laki mbili si haba. Angalia lugha yake. Baada ya week simu nyingine
 
Huyo kapata vicoba kweli ila si vicoba unayoisemea wewe.. i.e huku mtaani kwetu tuna wakina crdb,posta,nbc,nmb,atm password,vicoba,finca,saccos..N.K hao wote ni watu tu so usishangae huyo vicoba akawa ndo huyu jamaa maana kwa kukopesha tu haitaji malipo ya pesa ila pap.Chi
 
Preta kama unaufafanuzi wowote juu ya vicoba weka hapa mbona tena unapiga bonge la chekooo..!!!

Ufafanuzi ni kwamba........watakuwa wamevunja kikoba chao.........baada ya kununua hisa........kukopa na kurejesha marejesho........mwisho wa siku kuna kugawana faida.................

vicoba hoiyeeeeee..........
 
Back
Top Bottom