Kanye West amtumia Magufuli viatu vya Yeezy 500 vyenye saini yake,kupanda Kilimanjaro 2019

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
May 25, 2015
6,483
20,431
44054398_10156918005519078_3106381229075726336_n.jpg

Rapa kanye West na mkewe Kim West wako Uganda ambapo siku ya leo wamefanya mazungumzo na rais Yoweri Museven. Pamoja na mambo mengine Kanye West ametoa pair 2 za viatu vyake vya Yeezy vyenye saini yake ambapo pair moja amempa rais Museven na nyingine ameituma kwa rais Magufuli,kupitia ubalozi wetu nchini Uganda.
Kanye West amemuomba rais Museven na balozi wetu wamfikishie salamu zake kwa rais Magufuli na kudai kutokana na ufinyu wa muda alionao hawezi kufika Tanzania lakini akitoa ahadi ya kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni mwaka 2019.
Wakuu mimi naona hii ni kama dalili ya Kanye West anajaribu kuwashawishi Adidas kuleta baadhi ya viwanda vyake Afrika Mashariki,hasa hasa Uganda na Tanzania?
 
ni dharau kubwa sana hiyo, viatu!!!! namshauri rais asiruhusu vifike ikulu, kama vipi vibaki hukohuko kwa balozi tena stoo
 
Back
Top Bottom