MSAGA SUMU
JF-Expert Member
- May 25, 2015
- 6,483
- 20,431
Rapa kanye West na mkewe Kim West wako Uganda ambapo siku ya leo wamefanya mazungumzo na rais Yoweri Museven. Pamoja na mambo mengine Kanye West ametoa pair 2 za viatu vyake vya Yeezy vyenye saini yake ambapo pair moja amempa rais Museven na nyingine ameituma kwa rais Magufuli,kupitia ubalozi wetu nchini Uganda.
Kanye West amemuomba rais Museven na balozi wetu wamfikishie salamu zake kwa rais Magufuli na kudai kutokana na ufinyu wa muda alionao hawezi kufika Tanzania lakini akitoa ahadi ya kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni mwaka 2019.
Wakuu mimi naona hii ni kama dalili ya Kanye West anajaribu kuwashawishi Adidas kuleta baadhi ya viwanda vyake Afrika Mashariki,hasa hasa Uganda na Tanzania?