Kanuni mpya ya ukokotoaji mafao ni mwiba kwa wastaafu

Dibo10

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,298
1,563
Wiki iliyopita nikiwa safarini nilibahatika kukaa na mzee mmoja,alionekana kukosa uchangamfu huku mawazo yakiwa wazi yameshamiri ktk paji la uso wake, Baada ya kufahamiana na kuzungumza mawili matatu,taratibu tukaanza kushirikishana ktk mambo mbalimbali na mwishoni kabisa aliamua kuutema mwiba uliomkaba kooni. Kilichokuwa kinamsonomesha mzee wa watu ni uchache wa fao lake la kustaafu.Alianiambia hivi ndugu milioni chini ya 50 za mafao atazifanyia nini baada ya kulitumikia Taifa kwa zaidi ya miongo mitatu.

Picha ya yule mzee bado ipo kichwani mwangu, kwa wenzetu wakati wa kustaafu ni wakati wa kula matunda lakini hapa kwetu imekuwa kinyume. Baada ya Kuunganishwa kwa mifuko na kutungwa sheria mpya ya kusimamia tasnia ya hifadhi ya jamii, kanuni za ukokotozi nazo zilifanyiwa mabadiliko makubwa sana.Cha ajabu vyama vya wafanyakazi kazi vimekaa kimya kuhusu jambo hili nyeti sana.

Mamlaka ya kusimamia mifuko ya hifadhi ambayo naskia imebaki kuwa idara iko wapi ktk kuhakikisha mifuko inafanya kazi kwa ufanisi na kuwaongezea wanachama wake mafao badala ya kuyapunguza.?

Tatizo la hii mifuko ni kufanya uwekezaji usio na tija. Wao wanachojua ni kujenga majengo marefu, wengine wamewekeza mpka kwenye madaraja. Wala hauhitaji kuwa mtalaam wa fedha kujua huu ni uwekezaji usio na tija kwa wenye fedha zao ( Wastaafu). Wenyewe wanasema ujenzi wa majengo unaongezea thamani mfuko. Thamani ipi wakati wenye fedha zao wanalalamika mafao kiduchu huku wafanyakazi wa mfuko hasa top management wakiwa wanaogelea ktk ukwasi wa kutisha. Madg ktk mifuko na madf ni watu wasioshikika kila mradi lazima wawe na percent zao na huu ni utaratibu wa kawaida kabisa.

Ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua ya kudhibiti namna mifuko hii inavyofanya uwekezaji wake. Kwa baadhi ya nchi majirani kuna taasis maalum za uwekezaji zinaundwa zikiwa zimesheheni wabobezi wa uwekezaji ,wao ndio wanapewa dhamana za kuwekeza pesa za mifuko ya hifadhi. Leo mfano hai DG wa nssf ni mtu wa law, mtu kama huyu akikosa washauri wazuri chini yake usitarajie mawazo mbadala ya uwekezaji zaidi ya majengo.

Sasa ni wakati wa serikali kupora mamlaka ya uwekezaji kutoka kwa kwa hii mifuko na ziundwe taasis za kufanya kazi kwa niaba ya mifuko vinginevyo kila siku zitakuwa zinatafutwa sababu za kupunguza mafao badala ya kongeza.

Na mwisho serikali ichochee uanzishwaji wa mifuko binafsi ya hifadhi ya jamii. Nina hakika hii itaongeza ushindani na ufanisi ktk utoaji huduma.
 
Wiki iliyopita nikiwa safarini nilibahatika kukaa na mzee mmoja,alionekana kukosa uchangamfu huku mawazo yakiwa wazi yameshamiri ktk paji la uso wake, Baada ya kufahamiana na kuzungumza mawili matatu,taratibu tukaanza kushirikishana ktk mambo mbalimbali na mwishoni kabisa aliamua kuutema mwiba uliomkaba kooni. Kilichokuwa kinamsonomesha mzee wa watu ni uchache wa fao lake la kustaafu.Alianiambia hivi ndugu milioni chini ya 50 za mafao atazifanyia nini baada ya kulitumikia Taifa kwa zaidi ya miongo mitatu.

Picha ya yule mzee bado ipo kichwani mwangu, kwa wenzetu wakati wa kustaafu ni wakati wa kula matunda lakini hapa kwetu imekuwa kinyume. Baada ya Kuunganishwa kwa mifuko na kutungwa sheria mpya ya kusimamia tasnia ya hifadhi ya jamii, kanuni za ukokotozi nazo zilifanyiwa mabadiliko makubwa sana.Cha ajabu vyama vya wafanyakazi kazi vimekaa kimya kuhusu jambo hili nyeti sana.

Mamlaka ya kusimamia mifuko ya hifadhi ambayo naskia imebaki kuwa idara iko wapi ktk kuhakikisha mifuko inafanya kazi kwa ufanisi na kuwaongezea wanachama wake mafao badala ya kuyapunguza.?

Tatizo la hii mifuko ni kufanya uwekezaji usio na tija. Wao wanachojua ni kujenga majengo marefu, wengine wamewekeza mpka kwenye madaraja. Wala hauhitaji kuwa mtalaam wa fedha kujua huu ni uwekezaji usio na tija kwa wenye fedha zao ( Wastaafu). Wenyewe wanasema ujenzi wa majengo unaongezea thamani mfuko. Thamani ipi wakati wenye fedha zao wanalalamika mafao kiduchu huku wafanyakazi wa mfuko hasa top management wakiwa wanaogelea ktk ukwasi wa kutisha. Madg ktk mifuko na madf ni watu wasioshikika kila mradi lazima wawe na percent zao na huu ni utaratibu wa kawaida kabisa.

Ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua ya kudhibiti namna mifuko hii inavyofanya uwekezaji wake. Kwa baadhi ya nchi majirani kuna taasis maalum za uwekezaji zinaundwa zikiwa zimesheheni wabobezi wa uwekezaji ,wao ndio wanapewa dhamana za kuwekeza pesa za mifuko ya hifadhi. Leo mfano hai DG wa nssf ni mtu wa law, mtu kama huyu akikosa washauri wazuri chini yake usitarajie mawazo mbadala ya uwekezaji zaidi ya majengo.

Sasa ni wakati wa serikali kupora mamlaka ya uwekezaji kutoka kwa kwa hii mifuko na ziundwe taasis za kufanya kazi kwa niaba ya mifuko vinginevyo kila siku zitakuwa zinatafutwa sababu za kupunguza mafao badala ya kongeza.

Na mwisho serikali ichochee uanzishwaji wa mifuko binafsi ya hifadhi ya jamii. Nina hakika hii itaongeza ushindani na ufanisi ktk utoaji huduma.
Kuwa na amani maonevu yote na sheria kandamizi zote as from 2015 onward will be scrapped down once democracy is restored
 
Hiyo kanuni ipo wapi, kwani wastaafu wanapewa flat rate si wanaangalia pia kiasi cha uchangiaji mkuu.

Ungeainisha kiasi chake cha mshahara kilivyokuwa na hizo hesabu mpya angalau tungejua tunaanzia wapi, VINGINEVYO.
 
Wanapenda sana kuvaa kjani wacha wanyokepo nao maana kuna watu ukizungumza nchi inapokengeuka wao wanaona hayawahusu
 
Mkuu, huyo ni Mzee miongoni Mwa maelfu elfu wanaoilalamikia mfumo huo mpya wa kukokotoa Mafao ya uzeeni. Yaani ni Majanga.
Watumishi wamekuwa wapweke, vyama vya wafanyakazi vinaendelea kula 2% ya mishahara yao wakati havina msaada wowote.
 
yeah..ni kukomeshwa,yaani ukome kufanya kazi serikalini,kwamba ukifanya kazi serikalini wewe ni msoto tu,mshahara hautoshi,hupandi daraja na mafao wanafyekelea mbaaalii
 
Mkuu, huyo ni Mzee miongoni Mwa maelfu elfu wanaoilalamikia mfumo huo mpya wa kukokotoa Mafao ya uzeeni. Yaani ni Majanga.
Mkuu hali inatisha , waerevu waliokaribia umri wa kustaafu na waliokuwa wanalifahamu sakata hili vizuri walistaafu kwa hiyari mapema kabla kanuni mpya haijaanza kitumika
 
Hiyo kanuni ipo wapi, kwani wastaafu wanapewa flat rate si wanaangalia pia kiasi cha uchangiaji mkuu.

Ungeainisha kiasi chake cha mshahara kilivyokuwa na hizo hesabu mpya angalau tungejua tunaanzia wapi, VINGINEVYO.
ndugu..aliyetakiwa kupata 80m anapata 17m
 
Watumishi wamekuwa wapweke, vyama vya wafanyakazi vinaendelea kula 2% ya mishahara yao wakati havina msaada wowote.
Hivi vyama havina msaada wowote hasa yanapokuja masuala nyeti kama haya, haya ndio mambo ya kuyapigia kelele
 
Wiki iliyopita nikiwa safarini nilibahatika kukaa na mzee mmoja,alionekana kukosa uchangamfu huku mawazo yakiwa wazi yameshamiri ktk paji la uso wake, Baada ya kufahamiana na kuzungumza mawili matatu,taratibu tukaanza kushirikishana ktk mambo mbalimbali na mwishoni kabisa aliamua kuutema mwiba uliomkaba kooni. Kilichokuwa kinamsonomesha mzee wa watu ni uchache wa fao lake la kustaafu.Alianiambia hivi ndugu milioni chini ya 50 za mafao atazifanyia nini baada ya kulitumikia Taifa kwa zaidi ya miongo mitatu.

Picha ya yule mzee bado ipo kichwani mwangu, kwa wenzetu wakati wa kustaafu ni wakati wa kula matunda lakini hapa kwetu imekuwa kinyume. Baada ya Kuunganishwa kwa mifuko na kutungwa sheria mpya ya kusimamia tasnia ya hifadhi ya jamii, kanuni za ukokotozi nazo zilifanyiwa mabadiliko makubwa sana.Cha ajabu vyama vya wafanyakazi kazi vimekaa kimya kuhusu jambo hili nyeti sana.

Mamlaka ya kusimamia mifuko ya hifadhi ambayo naskia imebaki kuwa idara iko wapi ktk kuhakikisha mifuko inafanya kazi kwa ufanisi na kuwaongezea wanachama wake mafao badala ya kuyapunguza.?

Tatizo la hii mifuko ni kufanya uwekezaji usio na tija. Wao wanachojua ni kujenga majengo marefu, wengine wamewekeza mpka kwenye madaraja. Wala hauhitaji kuwa mtalaam wa fedha kujua huu ni uwekezaji usio na tija kwa wenye fedha zao ( Wastaafu). Wenyewe wanasema ujenzi wa majengo unaongezea thamani mfuko. Thamani ipi wakati wenye fedha zao wanalalamika mafao kiduchu huku wafanyakazi wa mfuko hasa top management wakiwa wanaogelea ktk ukwasi wa kutisha. Madg ktk mifuko na madf ni watu wasioshikika kila mradi lazima wawe na percent zao na huu ni utaratibu wa kawaida kabisa.

Ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua ya kudhibiti namna mifuko hii inavyofanya uwekezaji wake. Kwa baadhi ya nchi majirani kuna taasis maalum za uwekezaji zinaundwa zikiwa zimesheheni wabobezi wa uwekezaji ,wao ndio wanapewa dhamana za kuwekeza pesa za mifuko ya hifadhi. Leo mfano hai DG wa nssf ni mtu wa law, mtu kama huyu akikosa washauri wazuri chini yake usitarajie mawazo mbadala ya uwekezaji zaidi ya majengo.

Sasa ni wakati wa serikali kupora mamlaka ya uwekezaji kutoka kwa kwa hii mifuko na ziundwe taasis za kufanya kazi kwa niaba ya mifuko vinginevyo kila siku zitakuwa zinatafutwa sababu za kupunguza mafao badala ya kongeza.

Na mwisho serikali ichochee uanzishwaji wa mifuko binafsi ya hifadhi ya jamii. Nina hakika hii itaongeza ushindani na ufanisi ktk utoaji huduma.
Mkuu nilitegemea uweke hizo Kanuni Mpya ili tuzione lakini nimekutana na gazeti refuu!! Siasa nyingiii... Watz bhana!
 
Mzee wangu mmoja nilikua nafanya nae kazi kabla hajaamua kuomba kustaafu mwaka 2014 akiwa na miaka 48 na pensheni yake ilikua million 21 tu kwani mimi ndie niliempelekea cheki yake.
Ndani ya hii miaka michache aiseee ni hakamatiki mpaka namuonea wivu tukikutana maeneo yetu ya walevi anatucheka sanaa mzee ana costa moja noah moja zote hizi ni za biashara kijijini kwao pale kwake panatisha si nyumba ni hekalu liko pale
 
yeah..ni kukomeshwa,yaani ukome kufanya kazi serikalini,kwamba ukifanya kazi serikalini wewe ni msoto tu,mshahara hautoshi,hupandi daraja na mafao wanafyekelea mbaaalii
Ukiwa mfanyakazi sasa ni muhimu kuhakikisha una kila kitu cha kukusastaini pindi utapokuja kustaafu. Nyakati za kusubiri neema za mafao umeisha
 
Back
Top Bottom