Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
MkuuYapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.
Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.
Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.
Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.
Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.
KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.
KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.
Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu
Ushauri wowote pia napokea.
Chukua mmea wa cactus chukua na kilo tatu ya unga wa mbegu za parachichi chemsha maji lita tano kisha chuja yapoe kidogo anywe nusu lita ahsubuhi na jioni. Hakikisha anatumia mwezi mzima kisha tuletee matokeo kama anaanza kujisikia vyema.
Rudia zoezi kwa miezi mitatu naamini utaanza kuona matokeo. Akipata nafuu okoa maisha ya wengine kuwaambia ukweli. Usilipie huu ushauri