Kanisa Anglikana Tanzania lamuunga mkono Rais Magufuli katika mapamabano ya Ufisadi

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
36,155
29,677
Kanisa la Anglikana Tanzania limepongeza na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wa Tanzania Dkt.John Magufuli katika kupambana na ufisadi huku katika Dayosisi yake ya Ruvuma likiwa limejipanga kufufua mashamba yake ya miwa na kiwanda cha sukari huko lundo Nyasa mkoani Ruvuma ili kupunguza uhaba wa sukari nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Mhashamu Askofu Jacob Chimeledya huko Liuli Wilayani nyasa mkoani Ruvuma wakati wa kuwekwa wakfu na kusimikwa kwa Askofu wa kanisa hilo Dayosisi ya Ruvuma Askofu Raphael Haule anayekuwa Askofu wa nne wa Dayosisi hiyo anayechukua nafasi ya Askofu mstaafu Martenus Kapinga.

Kwa upande wake Naibu waziri wa elimu,Sayansi na Teknoloji Mheshimiwa Stela Manyanya aliyeiwakilisha serikali katika shughuli hiyo amewataka viongozi wa dini kusimamia malezi ya jamii na maadili kwa kuwa maadili mema na mila na desturi za kitanzania zinapita katika wakati mgumu na hatua zisipochukuliwa hali itakuwa mbaya zaidi.

Nao waumini wa kanisa hilo dayosisi ya Ruvuma wamemshauri Askofu wa Dayosisi ya Ruvuma Askofu Jacob Chimeledya kuwaendeleza kielimu wachungaji wa kanisa hilo.


My Take:Zile Sala Zetu ndio hizi
Source ITV

:: Kanisa La Anglikana Lamuunga Mkono Rais Magaufuli Katika Mapambano Ya Ufisadi
 
Hii ni kauli nyeti kutoka kwa waumini wa Anglikana Tanzania ikiwa ni muendelezo wa uungwaji mkono wa Rais Magufuli
 
Ukiwa mkubwa kila mtu atakuunga mkono tu.

Hata ukiachia ushuzi hadharani, watu bado watapiga makofi tu, siku ukitoka madarakani wanakupotezea kama walivyompotezea JK na Mwinyi.

Kuna watu hata hawajui kama Mwinyi alishawahi kuwa Rais wa nchi hii, lakini enzi zake za ruksa alikuwa akipigiwa makofi na kila mtu, kwa sera zake tamu za kufungulia madirisha ya kumwaga mihela mitaani.

Power is everything in this world.
 
Ukiwa mkubwa kila mtu atakuunga mkono tu.

Hata ukiachia ushuzi hadharani, watu bado watapiga makofi tu, siku ukitoka madarakani wanakupotezea kama walivyompotezea JK na Mwinyi.

Kuna watu hata hawajui kama Mwinyi alishawahi kuwa Rais wa nchi hii, lakini enzi zake za ruksa alikuwa akipigiwa makofi na kila mtu, kwa sera zake tamu za kufungulia madirisha ya kumwaga mihela mitaani.

Power is everything in this world.
Wameunga mkono mapambano dhidi ya ufisadi mkuu mbona unakuwa mgumu kuelewa?
 
Hongera askofu Haule,kila la heri katika kazi yako ya kuliongoza kanisa Anglikan Ruvuma.
 
Ufisadi upi aliopambana nao?! LUGUMI? ESCROW? RICHMOND? PESA UGHAIBUNI? MIKATABA YA MADINI NA GESI? RUSHWA KWENYE UCHAGUZI? NYUMBA ZA SERIKALI? MV BAGAMOYO? MABEHEWA MABOVU? Upi hapo kapambana nao.?! Kama siyo kutuletea tarifa hewa(zisizoaminika) za watumishi hewa tu!
 
Back
Top Bottom